Thursday, July 18, 2013

Balozi Kairuki akutana na Wakurugenzi wa JETRO


Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mberwa Kairuki (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Biashara ya Nje ya Japan (Japan External Trade Organization-JETRO) ofisi ya Nairobi, Kenya, Bw. Hiroshi Komatsuzaki (kushoto). Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa JETRO ofisi ya Johannesburg, Afrika Kusini, Bw. Kimihiko Inaba. Wakurugenzi hao walionana na Balozi Kairuki jijini Dar es Salaam kuzungumzia ziara ya Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa Japan  itakayofanyika nchini mwezi Agosti, 2013.
 
picha ya pamoja ya ujumbe wa Tanzania na JETRO wakiwa katika mazungumzo


Maafisa wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Khatibu Makenga na Bibi Redemptor Tibaigana wakinuu masuala muhimu ya mazungumzo.

Ujumbe wa Japan katika mazungumzo hayo, kutoka kulia ni Bw. Kimihiko, Bw. Hiroshi na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya kati na Afrika wa JETRO, Bw. Shintaro Matoba.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.