Monday, July 29, 2013

Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati akutana na Wajumbe wa Umoja wa Vijana wa IYDU

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Simba Yahya akizungumza na Wajumbe wa Umoja wa Vijana wa Kimataifa wa masuala ya Demokrasia (IYDU) kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kuhusu nafasi ya Sera ya Mambo ya Nje katika kusimamia Demokrasia nchini. Vijana hao kutoka  nchi 19 za Mabara  yote Duniani wapo nchini kushiriki mkutano wa Bodi wa IYDU.Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam tarehe 29 Julai, 2013.

Baadhi ya Wajumbe wa IYDU  wakifuatilia kwa makini mada iliyokuwa inawasilishwa na Balozi Yahya (hayupo pichani).

Bw. Aris Kalafatis ambaye ni Mwenyekiti  wa Umoja wa Vijana wa Kimataifa wa Masuala ya Demokrasia (IYDU) akieleza madhumuni ya ziara yao hapa nchini.

Bw. Deogratias Munishi, Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA), akiwatambulisha kwa Balozi Yahya (hayupo pichani) Wajumbe aliofuatana nao kabla  ya mkutano kuanza.

Bw. John Heche Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA), akielezea jambo wakati wa mkutano huo ambapo pia aliitoa shukrani kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa kuupokea Ujumbe huo wa Vijana.

Mmoja kati ya Wajumbe walio hudhuria, akiuliza swali wakati wa mkutano wao na Balozi Yahya.

Balozi Simba Yahya, akibadilishana mawazo na mmoja wa Wajumbe mara baada ya mazungumzo.

Balozi Simba Yahya akiwa katika Picha ya Pamoja, na Wajumbe wa Umoja wa Vijana wa Kimataifa wa Maswala ya Demokrasia (IYDU) mara baada ya kumaliza mazungumzo nao. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.