Tuesday, July 30, 2013

Tanzania na Thailand zasaini mikataba minne ya ushirikiano


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Ikulu na Waziri Mkuu wa Thailand, Mhe. Bibi Yingluck Shinawatra tayari kushuhudia uwekaji saini mikataba mbalimbali ya ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

Waziri wa Fedha, Mhe. William Mgimwa (kulia) kwa pamoja na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Thailand, Mhe. Dkt. Surapong Tovichakchaikul wakisaini Mkataba wa Kukuza na Kulinda Uwekezaji kati ya Tanzania na Thailand.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Thailand na Tanzania wakishuhudia uwekaji saini wa mikataba mbalimbali.

Mhe. Mgimwa na Mhe. Surapong wakibadilishana Mkataba mwingine kuhusu Ushirikiano wa Kitaalamu.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Perreira Ame Silima (Mb.) (kulia) akipata maelekezo kutoka kwa Bibi Naomi Zegezege, Afisa Mambo ya Nje katika Kitengo cha Sheria kabla ya kuanza kusaini Mkataba wa Kubadilishana Wafungwa kati ya Tanzania na Thailand. Pia Mhe. Dkt. Surapong akipokea maelekezo kama hayo kutoka kwa Afisa wa masuala ya Sheria kutoka Thailand.

Mhe. Silima na Mhe. Surapong wakibadilishana mkataba huo mara baada ya kusaini.

Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Bw. Eliakim Maswi kwa pamoja na Bibi Pornsawat Wathanakui, Mkurugenzi Mkuu kutoka Thailand wakisaini Mkatabakuhusu masuala ya Jiolojia na Usimamizi wa Rasilimali ya Madini.

Bw. Maswi na Bibi Wathanakui wakibadilishana mkataba mara baada ya kusaini huku Mhe. Rais Kikwete na Waziri Mkuu wa Thailand, Mhe. Shinawatra wakishuhudia.
 
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.