Friday, July 12, 2013

Mhe. Membe amuaga Balozi wa Uholanzi hapa nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akiongea kwa msisitizo wakati wa hafla ya kumuaga Mhe. Ad Koekkoek ambaye ni Balozi wa Uholanzi aliyemaliza muda wake wa kazi hapa nchini. Hafla hiyo  ilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Julai, 2013.

Baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini akiwemo Mhe. Alfonso Lenhardt (kulia), Balozi wa Marekani hapa nchini.

Mhe. Balozi Koekkoek naye akizungumza wakati wa hafla ya kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.


Wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano, Balozi Dora Msechu akizungumza machache wakati wa hafla hiyo.

Mhe. Membe akizungumza na Mhe. Balozi Koekkoek wakati wa hafla ya kumuaga Balozi huyo.

Mhe. Membe akimwonesha Mhe. Balozi Koekkoek zawadi ya picha ya kuchora ya Twiga aliyomkabidhi.

Mhe. Balozi Koekkoek akifurahia zawadi aliyokabidhiwa na Mhe. Membe.

Balozi Msechu akibadilishana mawazo na Mhe. Balozi Koekkoek.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.