Tuesday, July 30, 2013

Waziri Mkuu wa Thailand awasili nchini kwa ziara ya siku tatu

Waziri Mkuu wa Thailand, Mhe. Bibi Yingluck Shinawatra akiteremka kwenye ndege mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku tatu hapa nchini.
Mhe. Shinawatra akiwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili nchini kwa ajili ya ziara ya siku tatu.

Mhe. Shinawatra akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe, Said Mecky Sadick mara baada ya kuwasili nchini huku Mhe. Rais Kikwete, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Maharage wakishuhudia.

Mhe. Shinawatra akikagua Gwaride la Heshima.

Mhe. Shinawatra na mwenyeji wake Rais Kikwete wakisiliza nyimbo za mataifa yao zilipopigwa kwa heshima ya mgeni huyo.

Mhe. Shinawatra na Mwenyeji wake Rais Kikwete wakiangalia burudani ya ngoma iliyotolewa na moja ya kikundi kilichokuwa Uwanjani hapo wakati wa mapokezi.

Mhe. Shinawatra  kwa pamoja na Mhe. Rais Kikwete wakisalimiana na raia wa Thailand waliopo hapa nchini waliojitokeza kumlaki Waziri Mkuu huyo alipowasili katika Hoteli ya Hyatt Regency.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. John Haule (kulia)  akiwa pamoja na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Maharage (kushoto),  Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbwelwa Kairuki na Afisa Mambo ya Nje, Bw. John Pangipita wakibadilishana mawazo kuhusu ziara ya Waziri Mkuuu wa Thailand hapa nchini.


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.