Wednesday, July 17, 2013

Balozi Kairuki akutana na Mkurugenzi wa Masuala ya Afrika wa China


Mkurugenzi wa Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (kulia)akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa Masuala ya Afrika wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Bw. Lu Shaye. Bw. Lu ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya China ya  kufuatilia masuala yaliyokubaliwa wakati wa Mkutano wa FOCAC  alikutana na Balozi Kairuki kujadili namna Tanzania ilivyojipanga kuchangamkia ahadi zilizotolewa na China kwa nchi za Afrika wakati wa Mkutano wa FOCAC. 


Balozi Kairuki (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo hayo huku Bw. Lu akisikiliza kwa makini.


Picha ya pamoja kati ya  ujumbe wa Bw. Lu na ujumbe wa Balozi Kairuki wakiwa katika mazungumzo.
 Picha na Reginard P. Kisaka

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.