Friday, July 19, 2013

Mhe. Membe akutana na Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu wa China


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Watu wa China, Bw. Liu Jiayi alipofika Wizarani na Ujumbe wake kwa mazungumzo kuhusu Serikali hizi mbili kushirikiana kwa kubadilishana uzoefu katika masuala ya ukaguzi wa hesabu za serikali.
Bw. Liu Jiayi (wa kwanza kulia) na ujumbe wake akiwemo Balozi wa China hapa nchini, Mhe.Lv Youqing (wa tatu kutoka kulia) wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo nae.
Bw. Liu Jiayi akimweleza jambo Mhe. Membe aliyekuwa akisikiliza kwa makini.

Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Ludovick Utoh na ujumbe wake wakimsikiliza Bw. Lui Jiayi (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo na Mhe. Membe.

Mhe. Membe na wajumbe kutoka Tanzania na China kwa pamoja wakimsikiliza Bw. Liu Jiayi.

Mhe. Membe na Bw. Utoh wakimsikiliza Bw. Liu Jiayi alipokuwa akifafanua jambo katika moja ya taarifa za ukaguzi za nchini kwake alizomkabidhi Mhe. Membe.

Bw. Adam Isara, Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Bw. Liu Jiayi.
Mhe. Membe katika picha ya pamoja na Bw. Liu Jiayi na Mhe. Balozi Lv Youqing.

Mhe. Membe akiagana na Bw. Liu Jiayi.





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.