Monday, July 15, 2013

Makamu wa Rais, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wahudhuria Mkutano wa Afrika kujadili magonjwa mbalimbali


Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na Mfalme Mswati wa Swaziland III, wakati wa Mkutano wa 12 wa Afrika unaojadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja +12) nchini Nigeria.  Mkutano huo ulifunguliwa rasmi na Rais wa Nigeria Dkt. Goodluck Jonathan tarehe 15 Julai 2013 mjini Abuja na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi za Afrika.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akishiriki katika Mkutano wa 12 wa Afrika unaojadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja + 12) nchini Nigeria.  Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Mhe. Mahadhi Juma Maalim (MB) (nyuma kulia), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 


Picha na OMR, kwa hisani ya michuzi blog 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.