Saturday, July 20, 2013

Miili ya Askari waliofariki mjini Darfur yawasili nchini


Sehemu ya Masanduku yenye miili ya askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliofariki dunia hivi karibuni mjini Darfur nchini Sudan wakati wakilinda amani, yawasili nchini leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.  

Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wanananchi wa Tanzania (JWTZ) wakiwa wamebeba moja ya masanduku saba yenye miili ya askari wa jeshi hilo waliofariki dunia mjini Darfur wakati wakilinda amani.  

Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wanananchi wa Tanzania (JWTZ) wakipakia moja ya masanduku saba yenye miili ya askari wa jeshi hilo waliofariki dunia mjini Darfur wakati wakilinda amani.  

Askari hao waliuwawa kwa shambulio la kushtukiza na kundi la waasi wakati wakiwa kwenye kazi yao ya kulinda amani nchini Sudan.  

Jeshi la JWTZ lilioa taarifa likisema kuwa tukio hilo ni pigo kubwa kwa nchi yetu ya Tanzania ikiwa ni la kwanza kutokea tangu Tanzania ilipoanza kuchangia walinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa mwaka 2007.


Picha na maelezo kwa hisani ya www.issamichuzi.blogspot.com




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.