Monday, July 8, 2013

Mhe. Membe afungua Mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akifungua rasmi Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission-JPC) kati ya Tanzania na India unaofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro kuanzia tarehe 08 hadi 09 2013. Mkutano huo unaowashirikisha Wadau kutoka sekta mbalimbali za hapa nchini na India utajadili pamoja na mambo mengine masuala ya ushirikiano katika sekta za Uchumi, Ufundi, Sayansi na Teknolojia, Elimu, Afya, Utalii, Kilimo na Nishati na Madini.

Wadau kutoka sekta mbalimbali za hapa nchini  wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi huo.

Wadau wengine wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.

Wadau kutoka India.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya India, Mhe. Preneet Kaur akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.

Wadau wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Kaur (hayupo pichani)

Wadau zaidi.

Meza kuu kabla ya ufunguzi.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza machache kabla ya ufunguzi rasmi wa mkutano huo. Anayeonekana pembeni ni Mhe. John Kijazi, Balozi wa Tanzania nchini India.

Wajumbe wa Sekretarieti wakati wa mkutano huo.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur wakizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur walioketi, katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Omar Mjenga (kulia) akiwa na Mjumbe kutoka India wakati wa Mkutano huo.


Picha na Reginald Philip na Olga Chitanda.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.