Wednesday, July 10, 2013

Tanzania na India zasaini Makubaliano ya Pamoja ya Mkutano wa JPC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Preneet Kaur wakisaini Makubaliano ya Pamoja ya Mkutano wa 8 wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission-JPC) kati ya Tanzania na India mara baada ya mkutano huo kumalizika tarehe 09 Julai, 2013.Wengine wanaoshuhudia ni Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. John Kijazi (wa kwanza kulia waliosimama nyuma ya Mhe. Membe) akifuatiwa na Bw. Omar Mjenga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia na Balozi wa India hapa nchini, Mhe.Debnath Shaw (wa kwanza kushoto)

Wajumbe mbalimbali wakishuhudia uwekwaji saini makubaliano hayo.

Wajumbe wa Sekrtarieti kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nao wakishuhudia tukio hilo la uwekaji saini makubaliano.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur wakibadilishana Makubaliano hayo mara baada ya kusaini.

Mhe. Membe na Mhe. Kaur wakionesha kwa Wajumbe na Waandishi wa Habari  (hawapo pichani) Makubaliano hayo mara baada ya kusaini.


Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.