Monday, July 22, 2013

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa New Zealand

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza masuala mbalimbali katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na New Zealand alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Mhe. Murray McCully tarehe 22 Julai 2013. Mhe. McCully na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 21  na 22 Julai, 2013.
Mhe. McCully nae akimweleza Mhe. Membe masuala ya msisitizo katika kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili ikiwemo ushirikiano katika masuala ya biashara na kilimo.

Mhe. Membe na wajumbe kutoka Tanzania na New Zealand wakimsikiliza Mhe. McCully.

Mhe. Membe  akimkabidhi Mhe. McCully zawadi ya kinyago mara baada ya mazungumzo yao.


Mhe. Membe akiagana na mgeni wake mara baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.