Tuesday, November 5, 2019

Rais Xi atembelea Banda la Tanzania Maonesho ya Pili ya Bidhaa za Nje.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Xi atembelea Banda la Tanzania Maonesho ya Pili ya Bidhaa za Nje.   
Dar Es Salaam, 05 Novemba 2019
Maonesho ya Pili ya Kimataifa ya Bidhaa za Nje (China International Importation Expo) yamefunguliwa na Rais wa China, Mhe Xi Jinping tarehe 05 Novemba 2019.  Maonesho hayo yamehudhuriwa na viongozi wa Mataifa 64 akiwemo Rais wa Ufaransa Mhe Emmanuel Macron, Mawaziri Wakuu wa Jamaica; Serbia na Greece. Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Innocent Bashungwa.

Baada ya kufungua maonesho hayo Rais wa China ametembelea Mabanda ya nchi tano likiwemo Banda la Tanzania.  Nchi nyingine ambazo Rais Xi ametembelea mabanda yao ni Ufaransa; Ugiriki; Serbia na Jamaica.

Katika ziara ya kutembelea Banda la Tanzania, Rais Xi Jinping alifuatana na Waziri Mkuu wa Jamaica; Greece na Serbia na kupokelewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe Innocent Bashungwa na alitumia muda wa dakika 10 katika banda la Tanzania.  Rais Xi na wageni wake walipata maelezo kuhusu bidhaa mbalimbali za kilimo na madini zinazopatikana nchini Tanzania na vivutio vya utalii. Vile vile, Rais Xi alipokea salamu salaamu za  Mhe Rais Dk John Pombe Magufuli.

Kwa upande wake Rais wa China ameipongeza Tanzania kwa kushiriki katika maonesho ya Pili ya Kimataifa ya Bidhaa za Nje na ametuma salaamu za pongezi kwa Mhe Rais Magufuli kwa kuimarisha mahusiano ya kiuchumi kati ya Tanzania na China.  Aidha, Rais Xi alivutiwa zaidi na bidhaa ya korosho za Tanzania na madini ya Tanzanite ambapo alitaka kufahamu zaidi juu ya upatikanaji wa bidhaa hizo katika soko la China na bei ya Tanzanite. Alipewa majibu ya kutosha.

Maonesho ya Kimataifa yataendelea hadi tarehe 10 Novemba 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Banda la Tanzania
Banda la Tanzania lilivyopendeza

Bidhaa za Tanzania katika Maonesho ya Kimataifa ya Bidhaa za Nje nchini China
Bidhaa za Tanzania zikiwa katika vifungashio bora kabisa zilivutia watu wengi katika maonesho hayo.

 



Monday, November 4, 2019

PROF. KABUDI AKUTANA NA MABOLOZI WA NCHI ZA AFRIKA NA NORDIC WALIOPO NCHINI, WAANDISHI WA HABARI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika kikao cha pamoja na mabalozi kutoka nchi za Afrika na Nordic wakizungumzia maandalizi ya mkutano wa 18 wa mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Nordic utakaofanyika tarehe 7 - 8 Novemba 2019 jijini Dar es Salaam
Baadhi ya mabalozi kutoka nchi za Afrika na Nordic wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Hayupo pichani) wakati alipokutana nao kuzungumzia maandalizi ya mkutano wa 18 wa mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Nordic utakaofanyika jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)  akizungumza na waandishi wa habari kuwaelezea maandalizi ya mkutano wa 18 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Nordic unaotarajiwa kufanyika tarehe 7 - 8 Novemba 2019 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe, kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)  akiwaelezea waandishi wa habari maandalizi ya mkutano wa 18 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Nordic unaotarajiwa kufanyika tarehe 7 - 8 Novemba 2019 jijini Dar es Salaam





Friday, November 1, 2019

Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa 18 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika, Nordic

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na Nordic (Norway, Denmark, Finland, Sweden na Iceland) unaotarajiwa kufanyika tarehe 08 Novemba 2019 kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Akiongea na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe alisema kuwa mkutano huu utafunguliwa rasmi na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ambapo hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huu mkubwa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000.
Kwa mujibu wa Dkt. Mnyepe, mkutano huu utajumuisha jumla ya mawaziri 34 wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Nordic pamoja na washiriki wengine ambao idadi yao inatarajiwa kufikia 250. Mawaziri watakaokuja kutoka nchi za Nordic ni wa nchi za Sweden, Norway, Denmark, Finland na Iceland. Kutoka nchi za Afrika watakuja Mawaziri wa Algeria, Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Burundi, Comoros na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC).
Nyingine ni pamoja na Misri, Ethiopia, Ghana, Kenya, Lesotho, Mali, Malawi, Morocco, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Niger, Rwanda, Senegal, Somalia, Afrika Kusini, Tunisia, Uganda, Zambia, Zimbabwe na sisi wenyeji Tanzania. Aidha, mkutano huo utajumuisha Mawaziri, Mabalozi wa nchi shiriki za Afrika katika nchi za Nordic, Mabalozi wa nchi za Nordic hapa nchini pamoja na watendaji wa Serikali. Kauli mbiu ya mkutano huu ni: "Ushirikiano kwa Maendeleo Endelevu"
"Mkutano huu unafanyika hapa Tanzania kutokana na ushirikiano kati ya Tanzania na nchi za Nordic ni wa kihistoria na wa kipekee. Ushirikiano huu ulianza hata kabla ya uhuru wa Tanganyika ambapo Wamisionari kutoka nchi hizo walikuja kufanya kazi hapa nchini kwenye sekta za afya na elimu. Katika sekta ya elimu, nchi hizo zilianzisha Kituo cha Kilimo cha Uyole na Kituo cha Elimu cha Kibaha kupitia Mradi wa Nordic-Tanganyika Project.

Ushirikiano wa karibu kati ya Tanzania na nchi za Nordic ulichangiwa kwa kiwango kikubwa na falsafa zilizokuwa zinafanana kuhusu maendeleo ya watu, ukombozi wa Afrika, urafiki miongoni mwa viongozi wetu na nafasi ya kimkakati ya Tanzania katika Bara la Afrika," alisema Dkt. Mnyepe
Katibu Mkuu aliongeza kuwa, "katika nchi za Afrika, Tanzania inapokea misaada mingi kutoka nchi za Nordic kuliko nchi nyingine yoyote. Kwa mfano kwa miaka mitano ya kuanzia mwaka 2013 hadi 2018, Tanzania imepokea takribani Shilingi za Kitanzania bilioni 900 kutoka nchi za Nordic. Nchi hizo zimekuwa zikisaidia sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo: elimu; afya; miundombinu; nishati; TEHAMA; utafiti; ukusanyaji wa kodi; bajeti; misitu; usawa wa jinsia; utunzaji wa mazingira; na ukuzaji wa sekta ya biashara,".

"Kufuatia ushirikiano huu wa kihistoria kati ya Tanzania na nchi za Nordic, nchi hizo ziliiomba Serikali ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa mwaka huu kutokana na mahusiano na mazuri yaliyopo na hatua za kasi za kimaendeleo zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Kutokana na urafiki na historia hiyo hiyo Serikali ya Tanzania ilikubali kuwa mwenyeji wa mkutano wa mkutano huo na utafunguliwa na Mheshimiwa Rais. Kauli mbiu ya mkutano wa mwaka huu ni, Ushirikiano kwa Maendeleo Endelevu," aliongeza Katibu Mkuu 
Aidha, mkutano huu, utajadili fursa za uwekezaji, biashara, amani na usalama na masuala mengine mtambuka, kama vile athari za mabadiliko ya tabianchi. Katika mkutano huu, tutazungumzia pia mahusiano baina yetu na nchi moja moja hususan ubia wa kimaendeleo. Kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Tano, wenzetu wa Afrika na Nordic watapenda pia kusikia uzoefu na mafanikio ya Tanzania kwenye sekta za afya, elimu, nishati, miundombinu, kilimo, utalii, ukusanyaji wa kodi, mafanikio ya vita dhidi ya rushwa, ujangili, madawa ya kulevya na maeneo mengine. 
Kwa upande wake Balozi wa Norway nchini Tanzania, Balozi Elisabeth Jacobsen alisema kuwa mkutano huu utatoa pia fursa ya mazungumzo ya uwili (bilateral meetings) kati ya nchi za Nordic na nchi za Afrika.
"Ni imani yangu kuwa kupitia mkutano huu tutaweza kujadilili mambo mbalimbali ikiwemo hatua za kimaendeleo zilizofikiwa katika sekta mbalimbali hususan afya, huduma za kijamii, elimu na mazingira kibiashara na uwekezaji kwani Tanzania imekuwa na mahusiano mazuri na nchi mbalimbali duniani zikiwemo za Nordic," alisema Balozi Elisabeth.  
Nae Balozi wa Sweden nchini, Balozi Anders Sjoberg alisema kuwa mkutano wa kwanza ulifanyika nchini Sweden mwaka 2001 ambapo baada ya hapo mikutano kama hii ilikuwa inafanyika kwa kupokezana kutoka Bara la Afrika na nchi za Nordic. 
"Kwanza kabisa naipongeza Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huu wa Mawaziri wa Mambo ya Nje, ni fursa kutumia mkutano huu kujadili masuala ya kibiashara, uwekezaji, amani na usalama kwa maslahi ya nchi za Afrika na Nordic," alisema Balozi Sjoberg. 

Waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe alipokuwa akiongelea Mkutano wa 18 wa mawaziri wa mambo ya nje wa Afrika na nchi za Nirdic jijini Dar es Salaam leo
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Balozi Elisabeth Jacobsen akiongea na waandishi wa habari wakati wa mkutano. Katikati ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe na kulia ni  Balozi wa Sweden nchini, Balozi Anders Sjoberg.  
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Mnyepe akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano. Kushoto ni Mkuu wa Itifaki Kanali Wilbert Augustine Ibuge, akifuatiwa na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Balozi Elisabeth Jacobsen. Kulia ni Balozi wa Sweden nchini, Balozi Anders Sjoberg. 
Balozi wa Sweden nchini, Balozi Anders Sjoberg akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano, katikati ni Balozi wa Norway nchini Tanzania, Balozi Elisabeth Jacobsen na kushoto ni Kushoto ni Mkuu wa Itifaki Kanali Wilbert Augustine Ibuge






Wednesday, October 30, 2019

NAIBU WAZIRI AONGOZA UJUMBE WA WIZARA KWENYE KIKAO CHA KAMATI YA BUNGE

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisoma taarifa kwenye kikao kati ya Wizara na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara  Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe

Naibu Waziri Mhe. Dkt. Ndumbaro leo ameongoza ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye kikao kati ya Wizara na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Bunge jijini Dodoma. 
Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Musa Azzan Zungu (MB), kwa pamoja wameipongeza Wizara kwa  kutekeleza vyema mapendekezo yaliyotolewa na kamati hiyo katika vikao vilivyopita, sambamba na utekelezaji mzuri wa vipaumbele na malengo ya Wizara.
 
Kikao hicho kilitoa fursa kwa Wizara kuwasilisha kwa kamati taarifa mbalimbali za utekelezaji wa majukumu yake. Aidha, kikao hicho hutoa fursa kwa kamati kupokea na kujadili taarifa za Wizara pamoja na kutoa mapendekezo yake kuhusu masuala mbalimbali.


Kikao cha Wizara na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kikiendelea.
Sehemu ya Waheshimiwa Wabunge (Wajumbe wa Kamati) wakifuatilia taarifa ya Wizara iliyokuwa ikiwasilishwa wakati wa kikao. 
Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Wabunge (Wajumbe wa Kamati) wakifuatilia taarifa ya Wizara iliyokuwa ikiwasilishwa wakati wa kikao. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Musa Azzan Zungu (MB), akichangia jambo wakati wa kikao.
Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Wabunge (Wajumbe wa Kamati) wakifuatilia kikao.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AfDB) KUIPATIA TANZANIA ZAIDI YA SHILINGI TRILIONI MOJA KWA AJILI YA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA MSALATO WA JIJINI DODOMA PAMOJA NA BARABARA ZA MZUNGUKO JIJINI HUMO.

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imepongeza uamuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli wa kuhamia Dodoma na kuahidi kuidhinisha kiasi cha dola za kimarekani milioni 455 sawa na zaidi ya shilingi za Kitanzania trilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa Msalato sambamba na ujenzi wa barabara za mzunguko Jijini  humo.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina ameyasema hayo katika Ofisi za Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Abijdan Nchini Ivory Coast wakati wa Mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na kuongeza kuwa benki hiyo itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Rais Dkt John Pombe Magufuli katika kipindi chake cha Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) lakini pia kwa Tanzania.

Amesema Benki hiyo tayari imeshaidhinisha kiasi cha dola za marekani milioni 180 kwa ajili ya ujenzi wa barabara za mzunguko jijini  Dodoma na kwamba kiasi kingine cha dola za marekani milioni 275 kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Msalato kinatarajiwa kuidhinishwa na mapema mwezi Novemba 2019.

Dkt. Adesina ameongeza kuwa Benki ya Maendeleo ya Afrika ina imani na mageuzi ya kiuchumi yanayotekelezwa chini ya Uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma za kijamii ikiwemo elimu bila malipo,afya na maji pamoja na mapambano dhidi ya rushwa na kuleta uwajibikaji katika taaisisi za uma na kwamba iko tayari kuunga jitihada hizo za serikali kwa kuwekeza katika sekta ya miundombinu..

Aidha Dkt. Adesina ameelezea nia yake ya kutaka kushudia bara la Afrika likipiga hatua kubwa za kimaendeleo sasa na kwa haraka na sio kusubiri baadae na kwamba katika kipindi chake cha uongozi katika Benki ya Maendeleo ya Afrika atapambana kuhakikisha azma hiyo inatekelezeka.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa ushirikiano inayoutoa kwa Tanzania hususani katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na rais Dkt. John Pombe Magufuli ambayo kimsingi yalikuwa ni maono ya Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere kwa nia ya kuiwezesha Tanzania kujitegemea kiuchumi na hatimae Bara zima la Afrika.

Prof. Kabudi ameongeza kuwa tayari Benki ya Maendeleo ya Afrika iko tayari kufadhili ujenzi wa reli ya kisasa yaani standard gauge railway ya kipande cha kutoka Isaka hadi Kigali nchini Rwanda na kuelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mara baada ya kukamilika mchakato wa utoaji wa fedha hizo ambapo mazungumzo ya awali kuhusu ufadhili huo yameanza.

Pia Prof. Kabudi amemtaka Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Dkt. Akinwumi Adesina kuimarisha ofisi za kanda za benki hiyo ili ziweze kutoa huduma zote za kibenki ili kusogeza huduma karibu na wanufaika wa benki hiyo sambamba na kuunga mkono miradi yote ya kimkakati inayounganisha nchi na nchi katika bara la Afrika ili kuboresha nakurahisisha huduma ya usafiri katika Bara la Afrika na hivyo kuwezesha biashara miongoni mwa nchi za Kiafrika na kujiletea maendeleo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi yuko Abijdan Nchini Ivory Coast kushiriki mkutano wa siku mbili wa dharura wa Mawaziri wa fedha uliondaliwa na Benki ya maendeleo ya Afrika (AfDB).


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Abidjan - Ivory Coast.
30 OCTOBER 2019



BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AfDB) KUIPATIA TANZANIA ZAIDI YA SHILINGI TRILIONI MOJA KWA AJILI YA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA MSALATO NA BARABARA MZUNGUKO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba  John Kabudi (Mb) akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Abidjan Nchini Ivory Coast.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba  John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina. Mazungumzo hayo yamefanyika Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Abidjan Nchini Ivory Coast.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba  John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina,mara baada mazungumzo yaliyofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Abidjan Nchini Ivory Coast.Wengine katika picha ni viongozi wa AfDB na Afisa kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wa Tanzania.


Monday, October 28, 2019

Mkutano wa kuvutia uwekezaji katika nchi za SADC Wafanyika JIANGSU

Mkutano wa kuvutia uwekezaji katika nchi za SADC kutoka Jimbo la Jiangsu umefunguliwa leo jijini Nanjing na Naibu Gavana wa Jimbo hilo Ndugu Ma Qiulin. Mkutano huo umehudhuriwa na Mabalozi 11 wa nchi za SADC na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa SADC ambaye pia ni Mkurugenzi wa Miundombinu wa Sekretariat ya SADC Bi Mapolao Mokolena.

Katika hafla ya ufunguzi wa mkutano huo Balozi wa Tanzania Mhe. Mbelwa Kairuki alitoa hotuba kwa niaba ya Jumuiya ya Mabalozi wa Nchi za SADC nchini China ambapo pamoja na mambo mengine aliyakaribisha makampuni ya SADC kuchangamkia fursa za uwekezaji katika nchi za SADC kutokana  na fursa za soko kubwa la SADC lenye idadi ya watu wanaokadiliwa kuwa milioni 345 na uchumi wa GDP 600 Billioni.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Miundombinu wa SADC Bi Makolane alipokuwa akitoa mada alielezea mazingira mazuri  yaliyopo ya biashara na uwekezaji katika nchi za SADC. Aidha, Mabalozi wa nchi za SADC walielezea fursa zilizopo katika nchi za SADC katika sekta za miundombinu, kilimo, viwanda; madini; utalii nk.  

Jiangsu ni jimbo la pili kwa ukubwa wa uchumi nchini China likiwa na GDP ya USD 1.2 Trillion na idadi ya watu milioni 80.  Jimbo hilo linaongoza nchini China katika sekta ya viwanda. Makampuni kutoka Jimbo la Jiangsu yamefanya uwekezaji nchini Tanzania katika sekta ya viwanda.

Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Afrika na wenyeji China mara baada kuhitimisha mkutano wa kuvutia uwekezaji katika nchi za SADC uliofanyika jimbo la Jiangsu nchini China
Mhe. Balozi Mbelwa Kairuki akitoa hutuba kwenye ufunguzi wa Mkutano wa kuvutia uwekezaji katika nchi za SADC ulifanyika Jiangsu, China
Mhe. Balozi Mbelwa Kairuki (mstari wa mbele katikati) akifuatilia Mkutano wa kuvutia uwekezaji uliokuwa ukiendelea 
Wajumbe kutoka chi za SADC na Wenyeji tao China wakifutilia Mkutano uliokuwa ukiendelea

Friday, October 25, 2019

TANZANIA YATAKA ZIMBABWE KUONDOLEWA VIKWAZO VYA KIUCHUMI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akihutubia katika kongamano maalumu la kujadili vikwazo vya kiuchumi na hatma ya Afrika: Uzoefu kutoka Zimbabwe.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza katika kongamano la kujadili vikwazo vya kiuchumi iliyowekewa Zimbabwe

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango (Mb) akitoa hotuba ya majumuisho na kufunga kongamano maalumu la kujadili vikwazo vya kiuchumi iliyowekewa Zimbabwe

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. John Jingu, akihutubia hadhara wakati alipowasilisha mada iliyolenga hali ya utawala na diplomasia ya uchumi Afrika katika kongamano maalumu la kujadili vikwazo vya kiuchumi iliyowekewa Zimbabwe.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika kongamano maalumu lililojadili vikwazo vya kiuchumi na hatma ya Afrika: Uzoefu kutoka zimbabwe.

Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Mstaafu Joseph Warioba (wa pili kutoka kulia) pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali, vyama vya siasa wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika kongamano maalumu

Baadhi ya mabalozi wateule pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika kongamano la kujadili vikwazo vya kiuchumi iliyowekewa Zimbabwe.

Vingozi, Mabalozi na wananchi wakifuatilia mdahalo wa kujadili jinsi ya kuiwezesha Zimbabwe kuondolewa vikwazo vya kiuchumi.

Wageni wa Meza kuu wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango (Mb) na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye pamoja na watoa mada wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wateule katika picha ya pamoja mara baada ya kuhitimishwa kwa kongamano

Mabalozi wa SADC, Qatar watoa wito kuiondolea vikwazo Zimbabwe.

Waheshimiwa Mabalozi wakiwa wanaendelea kutekeleza jukumu lao.
Baada ya kumaliza kazi wanapongezena kwa kushikana mikono ikiwa ni kiashiria cha mshikamamo hadi Zimbabwe inaondolewa vikwazo.


Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Rajab akiongea na Waheshimiwa Mabalozi wa Nchi za Eswatini na Afrika Kusini ambao wanaunda kundi la Mabalozi wa nchi za SADC nchini Qatar. Waheshimiwa Mabalozi walikuwa wanakamilisha mpango mkakati wa kutumia siku ya tarehe 25 Oktoba kama ilivyoamuliwa na Viongozi wa Nchi za SADC kupaza sauti kwa njia mbalimbali kutoa wito kwa nchi za Magharibi kuiondolea vikwazo vya uchumi ilivyowekewa Zimbabwe. Mabalozi hao wamepanga kupeleka Waraka wa Kidiplomasia Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar, Balozi za EU na Ubalozi wa Marekani pamoja na kutoa makala kwenye vyombo vya habari kuelezea athari za vikwazo katika uchumi wa Zimbabwe. 

WAZIRI KABUDI ASHIRIKI MAADHIMISHO YA 74 YA SIKU UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na Bw. Michael Dunford Kaimu Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini alipowasili katika uwanja wa Nyerere Square jijini Dodoma kushiriki maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa amesimama sehemu maalumu wakati wimbo wa Taifa ulipokuwa unapigwa kwenye sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa mbele ya parede maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akikagua parede maalumu liliondaliwa kwa ajili ya sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja Mataifa 
Sehemu ya hadhara iliyojitokeza katika uwanja wa Nyerere Square kushuhudia sherehe za maadhimisho 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (katikati) akifuatalia matukio yaliyokuwa yakiendelea wakati wa maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, akipokea zawadi kutoka Ofisi za Umoja wa Mataifa nchini iliyowasilishwa na Bw. Michael Dunford Kaimu Mratibu Mkazi, kwenye sherehe za maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika jijini Dodoma 
Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi Wafanyakazi wa Ofisi za Umoja wa Mataifa nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akihutubia  hadhira iliojitokeza kwenye maadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Taifa iliyofanyika jijini Dodoma katika uwanja wa Nyerere Square

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akihutubia  hadhira iliojitokeza (hawapo pichani) kwenye amaadhimisho ya 74 ya Siku ya Umoja wa Taifa iliyofanyika jijini Dodoma katika uwanja wa Nyerere Square


WAKATI HUO HUO MHE. PROF. KABUDI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA  BW. MICHAEL DUNFORD KAIMU MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwa na Bw.Michael Dunford Kaimu Katibu Makazi wa Umoja wa
Mataifa nchini, walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma. Wengine ni Bw. Deusdedit Kaganda Kaimu Mkurugenzi wa Ushikiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Bi.Glory Ngaiza Afisa Mambo ya Nje.
Waziri Mhe. Prof. Kabudi akilelezea jambo wakati wa mazungumzo na Bw. Michael Dunford Kaimu Katibu Makazi wa Umoja wa Mataifa nchini. Wawili hao wamejadili masuala mbalimbali ya kuendelea kudumisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Umoja wa Mataifa


VILEVILE WAZIRI MHE. PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akisisitiza jambo alipokutana wakati wa mazunguzo na Mkuu wa Shirika la Wahamiaji nchini Dr. Qasim Sufi walipokutana kwa mazungumzo katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Wawili hao wamejadili masuala mbalimbali ya kuendelea kudumisha ushiririkiano kwa lengo la kuongeza ufanisi katika kutoa huduma.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akimsikiliza Mkuu wa Shirika la Wahamiaji nchini Dr. Qasim Sufi walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma