Tuesday, February 18, 2020

Katibu Mkuu Mwaluko azitaka sekta zishirikiane kukabili maafa


Na. OWM, ZANZIBAR

“Tatizo la athari za maafa yanayotokana na majanga ya asili linahitaji ushiriki wa sekta zote ili kukabiliana nalo ipasavyo, katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)” Mwaluko.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Zanzibar na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko wakati alipokuwa anafungua kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ambaye yeye ni mwenyekiti.

 Mwaluko amesema nchi zote za SADC zina uzoefu wa masuala ya maafa, hivyo ni matarajio yake kuwa kazi waliyopewa ya kuandaa nyaraka kwa ajili ya mkutano wa Mawaziri wenye dhamana ya maafa utakaofanyika siku ya Ijumaa tarehe 21 Februari 2020,  uweze kufikia malengo yake.

Katika kikao hicho, Makatibu Wakuu wataandaa nyaraka itakayo ainisha mikakati na programu za kukabiliana na maafa na mpango unaobainisha namna nchi za SADC zilivyojipanga kukabiliana na maafa yanapotokea katika ukanda huo.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mtendaji wa SADC wa Masuala ya Ushirikiano wa Kikanda, Dkt. Thembinkosi Mhlongo  alieleza kuwa athari za maafa zikiwemo vifo, uharibifu wa mali na miundombinu zimezikumba takribani nchi zote za SADC. Hivyo amesisitiza umuhimu wa nchi hizo kushirikiana kwa pamoja kuandaa mikakati ya menejimenti ya maafa.

Naye, Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar, Bw. Abdallah Hassan Mitawi amewaeleza  wajumbe wa kikao hicho kuwa nchi za SADC zimelipa umuhimu mkubwa suala la kukabiliana na athari za maafa na hilo linadhihirishwa na ushiriki wa nchi 15 kati ya 16 wanachama wa SADC katika mkutano huo.

Mkutano huo unaofanyika kwenye Hoteli ya Madinat AL Bahir iliyopo Mbweni, nje kidogo ya mji wa Zanzibar unatarajiwa kuhitimishwa kwa kikao cha ngazi ya Mawaziri tarehe 21 Februari 2020 ambapo Mgeni Rasmi atakuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein.

“Ushiriki wa kisekta kwenye Kupunguza madhara  ya maafa ni njia  bora ya kujenga Uhimili  katika ukanda wa nchi wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)”
MWISHO.


Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akifafanua umuhimu wa ushiriki wa kisekta kwenye Kupunguza madhara ya maafa, wakati akifungua kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa katika ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ambapo yeye ni mwenyekiti wa kikao hicho, leo tarehe 18 Februari 2020, Zanzibar.

Naibu Katibu Mtendaji wa SADC wa Masuala ya Ushirikiano wa Kikanda, Dkt. Thembinkosi Mhlongo akifafanua umuhimu wa Nchi  za SADC kuwa na mikakati ya kukabili maafa yanayo zikabili, wakati wa kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa katika ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC, leo tarehe 18 Februari, 2020, Zanzibar
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar, Bw. Abdallah Hassan Mitawi akifafanua namna ya nchi za SADC zinavyoathirika na maafa ya asili, wakati wa kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa katika ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC, leo tarehe 18 Februari, Zanzibar


Baadhi ya makatibu wakuu kutoka Tanzania, wakifuatilia kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa katika ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC, leo tarehe 18, Februari, 2020, Zanzibar, (katikati), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi,anayeshughulikia Mifugo,  Profesa Olesante Ole Gabriel (kulia kwake), Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dkt. Faraij Mnyepe,  na Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio.

Baadhi ya maafisa waandamizi kutoka ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), wakifuatilia kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa, leo tarehe 18 Februari, 2020, Zanzibar.


Baadhi ya maafisa waandamizi kutoka ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), wakifuatilia kikao cha SADC cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa, leo tarehe 18 Februari, Zanzibar, Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali, Jimmy Matamwe,(kulia), Mkurugenzi wa Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa, Zanzibar , Makame Khatibu Makame na Naibu Mkurugenzi wa Kamisheni hiyo, Muhidin Ali Muhidin
Makatibu Wakuu wenye dhamana ya maafa katika ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC,wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo, leo tarehe 18, 2020, ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni “Ushiriki wa kisekta kwenye Kupunguza madhara  ya maafa ni njia  bora ya kujenga Uhimili  katika ukanda wa nchi wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)”
Makatibu Wakuu na maafisa waandamizi wenye dhamana ya maafa katika ukanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC,wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo, leo tarehe 18, Februari, 2020, ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni “Ushiriki wa kisekta kwenye Kupunguza madhara  ya maafa ni njia  bora ya kujenga Uhimili  katika ukanda wa nchi wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)”


NAIBU WAZIRI DKT.NDUMBARO AHITIMISHA ZIARA YAKE KATIKA ENEO LA USHOROBA WA MTWARA


Sunday, February 16, 2020

WAZIRI KABUDI: WATUMISHI FANYENI KAZI KWA BIDII NA USHIRIKIANO


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amewataka Watumishi wa Wizara hiyo kuchapa kazi kwa bidii na kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Katibu Mkuu mpya, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge.

Mhe. Prof. Kabudi ametoa rai hiyo jana jijini Dodoma wakati wa kikao na Watumishi wa Wizara ambapo pamoja na mambo mengine, kikao hicho kilitoa fursa ya kutakiana heri ya mwaka mpya 2020 na kumkaribisha Wizarani Katibu Mkuu Mpya, Balozi Kanali Ibuge.

Aidha, Mhe. Prof. Kabudi aliwaeleza watumishi hao kuwa, mwanzo wa mwaka ni kipindi kizuri cha kujipanga na kuweka mikakati ya namna bora ya kutekeleza majukumu  kwa ajili ya maendeleo ya Taifa ikiwa ni pamoja na kufahamu vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Joseph Pombe Magufuli.

Kadhalika amewataka kufanya kazi kwa bidii, kujitambua na kujenga umoja  na ushirikiano katika kutekeleza majukumu hayo kikamilifu.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge ameahidi ushirikiano kwa watumishi wa Wizara na kuwakumbusha kuwa kila mmoja ana wajibu mkubwa wa kuchangia maslahi mapana ya Taifa ilimradi kila mmoja atekeleze wajibu wake kwa kuendelea kujituma, kuwa tayari kurekebishwa, kuwa watiifu na kuwa tayari kupokea maelekezo.

"Watumishi wenzangu, kila mmoja hapa ana mchango mkubwa kwa maslahi ya Taifa letu. Ninasisitiza kuwa mwendelee kujituma, kufanya kazi kwa weledi, kuwa watiifu, kuwa tayari kurekebishwa na kuwa tayari kupokea maelekezo. Binafsi nitaendelea kutoa usikivu kwenu kama ilivyokuwa kwa watangulizi wangu" alisema Balozi Ibuge.

Kuhusu changamoto mbalimbali zinazoikabili Wizara, Balozi Kanali Ibuge amewataka Watumishi wote kushirikiana kuzitatua kwani hakuna changamoto ya kudumu endapo Watumishi wote watakuwa kitu kimoja.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongea na Watumishi wa Wizara wakati wa kikao kilichofanyika jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akiongea na watumishi wa wizara wakati wa kikao kilichofanyika jijini Dodoma

 Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao kilichofanyika jijini Dodoma 




NAIBU WAZIRI DKT.NDUMBARO AHITIMISHA ZIARA YAKE KATIKA ENEO LA USHOROBA WA MTWARA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amehitimisha ziara yake katika Mikoa  inayopitiwa na mradi wa maendeleo wa kuboresha miundombinu ya Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (Mtwara Corridor). Mradi huu unahusisha ujenzi wa bandari ya Mtwara (ambao unaendelea kwa kasi), ujenzi wa barabara katika kiwango cha lami kuanzia Bandari ya Mtwara hadi bandari ya Mbamba Bay iliyopo Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma sambamba na ujenzi wa bandari hiyo.

Lengo la ziara hii ilikuwa ni kuangalia hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa miundombinu ya bandari na barabara katika ushoroba huo, kufanya mazunguzmzo na viongozi wa Serikali za Mikoa na Wilaya, ambapo Mheshimiwa Ndumbaro alitumia nafasi hiyo kuhimiza Mamlaka za Mikoa na Wilaya, kulinda na kuboresha uhusinao wa kidipolomasia na nchi tunazopakana nazo katika ukanda huo ili kujenga mazingira rafiki ya kibiashara, wakati huu ambao Serikali ya Awamu ya Tano imeboresha miundombinu inayowezesha kuzifikia nchi hizo kiurahisi zaidi.

Ujenzi wa miundombinu katika Ukanda wa Kusini mwa Nchi unachochea ukuaji wa biashara katika ukanda huo kwa kurahishisha usafirishaji na mawasiliano na kuzifikia kiurahisi Nchi jirani za Malawi, Kaskazini mwa Msumbiji na Zambia.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Mambo Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Ndumbaro aliambatana na Balozi wa Malawi nchini Mhe.Glad Chembe Munthali, ambaye amefurahishwa na kuridhishwa na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujenga mazingira rafiki ya kibiashara na nchi jirani kwa kuboresha miundombinu inayoziwezesha nchi hizo kunufaika na huduma za bandari nchini kiurahisi na kwa gharama nafuu. 

Kadhalika, nia ya Mhe. Munthali Balozi wa Malawi nchini, katika ziara hiyo ilikuwa ni kuangalia kwa namna gani wafanyabiashara kutoka nchini kwake watanufaika na uboreshwaji wa miundombinu ya ushoroba wa Mtwara katika kusafirisha bidhaa zao kwa muda mfupi na gharama nafuu. 

Aidha, kwa nyakati tofauti Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Christina Mndeme na Mkuu wa Wilaya Nyasa Mhe. Isabela Chilluba wameelezea utayari wao wa kuratibu na kusimamia shughuli na fursa za biashara zinazotokana na maboresho ya miundombinu katika ukanda huo.

Ziara hii ni mwendelezo wa jitihada zinazofanywa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa  kushirikiana na Mamlaka mbalimbali za ndani katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kukuza biashara na kuvutia uwekezaji nchini.   

Ujenzi wa barabara ya Mtwara hadi bandari ya Mbamba Bay kwa kiwango cha lami unafikia ukingoni, mkandarasi anaendelea na ujenzi wa sehemu iliyosalia (Mbinga hadi Mbamba bay) ambapo anataraijia kukabidhi barabara hiyo Septemba, 2020.

Ujenzi wa miundombinu katika ushoroba wa Mtwara umeleta mapinduzi makubwa ya maendeleo ya uchumi na kijamii katika Mikoa ya Kusini mwa Tanzania sambamba na kuliongezea Taifa mapato.  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa (kulia) wakiwa kwenye mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa akielezea jambo kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kwa kutumia kielelezo cha ramani, walipokuna kwa mazungunzumzo wakati wa ziara ya Dkt.Ndumbaro katika ushoroba wa Matwara. 
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa (kulia) na Balozi wa Malawi nchini Mhe.Glad Chembe Munthali (kushoto) wakiwa katika mazungumzo walipokutana wakati wa ziara ya Mhe. Dkt. Ndumbaro katika Mkoa huo
Kutoka kulia ni Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi wa Malawi nchini Mhe.Glad Chembe Munthali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius G. Byakanwa, Bw. Alfayo Kidata Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, na Mhe. Evod Mmanda Mkuu wa Wilaya ya Mtwara wakiwa katika picha ya pamoja.
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  akisalimiana na Wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara alipotembelea Ofisi za Bandari hiyo wakati wa ziara yake mkoani humo.
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza na wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara (hawapo pichani). Aliwahimiza kujituma na kuongeza ubunifu ili kuongeza  ufanisi na tija wa bandari hiyo ambayo ukarabati wa kuiboresha unaendelea.
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na Watendaji wa Bandari ya Mtwara na Viongozi wa Mkoa alipotembelea eneo la bandari ya Mtwara
Kutoka kushoto; Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Christina Mndeme Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, na Mhe.Glad Munthali Chembe Balozi wa Malawi nchini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma. 
Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na Mhe. Isabela Chilluba Mkuu wa Wilaya ya Nyasa alipowasili wilayani humo kwa ziara ya siku moja
 Mkuu wa Wilaya Nyasa Mhe. Isabela Chilluba akitoka maelezo kwa Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  na Ujumbe wake katika moja ya fukwe na eneo la bandari ya Mbamba Bay iliyopo katika Ziwa Nyasa. 
Picha ya pamoja 


Wednesday, February 12, 2020

BALOZI IBUGE AKUTANA, AFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI WA SHIRIKA LA IOM


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Uhamaji (IOM), kanda ya Kusini mwa Afrika Bw. Charles Kwenin katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Pamoja na mambo mengine, mazungumzo hayo yalijadili mambo mbalimbali ikiwemo maandalizi ya Majadiliano kuhusu Uhamaji katika kanda ya Kusini mwa Afrika yanayotarajia kufanyika chini ya uenyekiti wa Tanzania kama Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).

Majadiliano hayo yanatarajiwa kufanyika kabla ya mwezi Agosti, mwaka 2020 hapa nchini yakiwa na dhamira ya kujadili usimamizi wa masuala ya uhamiaji ili kuwezesha uundwaji wa sera zenye uwiano miongoni mwa nchi wanachama wa SADC.

Aidha, Balozi Ibuge amewahakikishia wajumbe wa IOM, utayari wa Tanzania kuwa nchi mwenyeji wa Majadiliano hayo.




Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Uhamaji (IOM), kanda ya Kusini mwa Afrika Bw. Charles Kwenin akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akiwaelezea jambo Mkurugenzi wa Shirika la (IOM), kanda ya Kusini mwa Afrika Bw. Charles Kwenin akiongea pamoja na Mwakilishi wa IOM hapa nchini Dkt. Qasim Sufi leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa (IOM), Bw. Charles Kwenin, Mwakilishi wa IOM nchini Dkt. Qasim Sufi pamoja na Afisa Uhusiano na Sera wa IOM, Bi. Naomi Shiferaw. Wengine kulia mwa Katibu MKuu ni watumishi wa Wizara, Bw. Hangi Mgaka na Gloria Ngaiza.  






Tuesday, February 11, 2020

BALOZI KANALI IBUGE AKUTANA,KUFANYA MAZUNGUMZO NA SEKRETARIETI YA SADC

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Pamoja na mambo mengine, Katibu Mkuu alipokea taarifa ya ziara ya Sekretarieti ya SADC na kuwahakikishia ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hususan Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika kufanikisha mikutano yote ya SADC kipindi cha Uenyekiti wa Tanzania.

Ujumbe huo wa Sekretarieti ya SADC una wajumbe watano ukiongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa SADC, Bibi. Bodo Tanrely Radaody Ravarosy ambao wapo nchini kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa SADC unaotarajiwa kufanyika tarehe 10 - 11 Machi, 2020, Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, ujumbe huo ulipata fursa ya kukutana na Katibu Mkuu Balozi Ibuge na kumpa taarifa ya maandalizi ya mkutano huo.

Mwezi Augosti, 2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli alipokea rasmi Uenyekiti wa SADC katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi wanachama.

Aidha, hatua hiyo ilifuatiwa na mikutano mbalimbali ya kisekta iliyofanyika na inayoendelea kufanyika hapa nchini kwa kipindi cha kuanzia mwezi Septemba 2019 hadi Agosti, 2020 ambapo hadi sasa imeshafanyika mikutano mitatu ya kisekta.

Mikutano hiyo ni pamoja na Mkutano wa Mawaziri wa SADC wenye dhamana ya masuala ya Tehama, Habari, Uchukuzi na hali ya Hewa, Mkutano wa Pamoja wa Mawaziri wa Sekta ya Afya na VVU na UKIMWI pamoja na mkutano wa pamoja wa Mawaziri wa Mazingira, Maliasili na Utalii.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akiongea na Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa SADC, Bibi. Bodo Tanrely Radaody Ravarosy leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya SADC pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akiagana na Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa SADC, Bibi. Bodo Tanrely Radaody Ravarosy

DKT. NDUMBARO, BALOZI IBUGE WASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA RAIS MSTAAFU WA KENYA HAYATI DANIEL ARAP MOI

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) pamoja na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge wamesaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Kenya nchini kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Kenya, Daniel Arap Moi aliyefariki 4 Februari, 2020.   

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akitoa salamu za pole kwa baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi wa Kenya Jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Kenya, Hayati Daniel Arap Moi

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Kenya Jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Kenya, Hayati Daniel Arap Moi

 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wizara hiyo, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Kenya Jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Kenya, Hayati Daniel Arap Moi

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) pamoja na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi wa Kenya Jijini Dar es Salaam mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo



Monday, February 10, 2020

DKT. NDUMBARO AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WANAOWAKILISHA KUNDI LA UFC

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wa nchi tano (5) hapa nchini wanaowakilisha kundi la Uniting for Consensus (UfC) la Mageuzi ya Baraza la Usalama ya Umoja wa Mataifa.

Dkt. Ndumbaro amekutana na mabalozi hao leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam ambapo ujumbe huo umewahusisha, Balozi wa Italia nchini Mhe. Balozi Roberto Mengoni, Balozi wa Hispania nchini Mhe. Balozi Fransisca Pedros, Balozi wa Canada nchini Mhe. Pamela O’Donnel, Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Balozi Ali Davutoglu, pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Tae-ick Cho.


Pamoja na mambo mengine, majadiliano hayo yalijikita kujadili masuala mbalimbali yanayohusu ulinzi na usalama wa Umoja wa Mataifa.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), akisalimiana na Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Balozi Ali Davutoglu wakati mabalozi wanaowakilisha kundi la Uniting for Consensus (UfC) la Mageuzi ya Baraza la Usalama ya Umoja wa Mataifa wakati walipomtembelea na kufanya nae mazungumzo leo katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), akiwaeleza jambo mabalozi wanaowakilisha kundi la Uniting for Consensus (UfC) la Mageuzi ya Baraza la Usalama ya Umoja wa Mataifa wakati walipomtembelea na kufanya nae mazungumzo leo 
Balozi wa Italia nchini Mhe. Balozi Roberto Mengoni akimueleza jambo Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), wakati mabalozi hao walipomtembelea Naibu Waziri na kufanya nae mazungumzo

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), akiwa ktk picha ya pamoja na mabalozi wanaowakilisha kundi la Uniting for Consensus (UfC) la Mageuzi ya Baraza la Usalama ya Umoja wa Mataifa 




KATIBU MKUU MPYA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI AKABIDHIWA OFISI RASMI


Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge amekabidhiwa Ofisi rasmi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Faraji K. Mnyepe kufuatia uteuzi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 06 Februari, 2020. Kabla ya uteuzi huo Balozi Kanali Ibuge alikuwa Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocol). 


Aidha, Balozi Ibuge anachukua nafasi ya Dkt. Faraji K. Mnyepe ambaye alihamishwa wizara kwa kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Dkt. Mnyepe amechukua nafasi ya Dkt. Frolens Turuka ambaye amestaafu.

Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akipokea baadhi ya nyaraka za Ofisi kutoka kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Faraji K. Mnyepe. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akimpa mkono aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Faraji K. Mnyepe mara baada ya makabidhiano rasmi ya Ofisi.

Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Ramadhani Mwinyi baada ya kumtembelea ofisini kwake leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas D. Ndumbaro (Mb) akiwa na Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge alipomtembelea Ofisini kwake leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Sunday, February 9, 2020

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ASHIRIKI MKUTANO WA 33 WA UMOJA WA AFRIKA ADDIS ABABA,ETHIOPIA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akiwa katika Mkutano wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika unaoendelea Addis Ababa,Ethiopia. Nyuma yake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na Balozi wa Tanzania Nchini Ethiopia Mhe. Naimi Aziz.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akipitia baadhi ya nyaraka wakati akishiriki katika Mkutano wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika unaoendelea Addis Ababa,Ethiopia. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete walipokutana katika ukumbi wa mkutano wa Umoja wa Afrika Addis Ababa, Ethiopia.

Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika ukumbi wa Mkutano wa Umoja wa Afrika Addis Ababa,Ethiopia. Anayeshuhudia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan 

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika anayemaliza muda wake Mhe. Abdel Fattah el-Sisi ambae pia ni Rais wa Misri akikabidhi Uenyekiti kwa Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika Mhe. Cyril Ramaphosa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiteta jambo na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe Yoweri Kaguta Museveni walipokutana katika jengo la Umoja wa Afrika wakati akisubiri kumpokea Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan Mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Friday, February 7, 2020

MKUTANO WA 7 WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI WA MAZINGIRA NA USIMAMIZI WA MALIASILI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAFIKIA TAMATI JIJINI DODOMA

Meza Kuu ikifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea wakati wa Mkutano wa Saba (7) wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Dodoma. Mkutano huu uliofanyika kwa kipindi cha siku 5 (tarehe 3-7 Februari, 2020) umefanyika katika ngazi tatu nazo ni; ngazi ya wataalamu, ngazi ya Makatibu Wakuu na ngazi ya Mawaziri. 
Mawaziri kutoka nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakisaini taarifa kwenye Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Dodoma, Ijumaa tarehe 7 Februari, 2020
Mawaziri kutoka nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakisaini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada kusaini taarifa ya Mkutano 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu wakijadili jambo kwenye Mkutano wa 7 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Dodoma.  
Mawaziri walioiwakilisha Tanzania wakishikishana jambo kwenye Mkutano wa 7 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Mazingira na Usimamizi wa Maliasili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Dodoma.

TANZANIA YAISHAURI ETHIOPIA KUTAFUTA KIINI CHA TATIZO LA RAIA WAKE KUONDOKA NCHINI HUMO BILA KUFUATA UTARATIBU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Dkt Workneh Gebeyehu walipokutana kwa ajili ya mazungumzo Mjini Addis Ababa,Ethiopia Kando ya Mkutano wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika. 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Dkt Workneh Gebeyehu (Katikati) akiwa na ujumbe wake katika mazungumzo baina yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (hayupo pichani).Mazungumzo hayo yamefanyika Mjini Addis Ababa,Ethiopia Kando ya Mkutano wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa na ujumbe wake katika mazungumzo baina yake Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Dkt Workneh Gebeyehu (hayupo pichani) kushoto aliyevaa kilemba ni Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe Naimi Azizi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Dkt Workneh Gebeyehu. Mazungumzo hayo yamefanyika Mjini Addis Ababa,Ethiopia Kando ya Mkutano wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika.