Sunday, September 29, 2013

Matukio zaidi Mhe. Rais alipolihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akielekea kwenye Jukwaa la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuhutubia Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.


Mhe. Rais Kikwete akihutubia Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Mjini New York ambapo katika hotuba hiyo alielezea masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na nafasi ya Tanzania katika kuchangia walinzi wa Amani, Mageuzi katika Umoja wa Mataifa, Utekelezaji wa Malengo ya Milenia na pia alitoa salamu za rambirambi kwa Serikali ya Kenya kufuatia shambulio la kigaidi lililotokea tarehe 23 Septeba, 2013 mjini Nairobi.



 

Mhe. Membe akiwa na Mhe. Haroun Suleiman, Waziri wa Kazi na Utumishi wa Umma wa Zanzibar wkimsikiliza Mhe. Rais Kikwete alipolihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.



 

Mhe. Ramadhan Mwinyi, Naibu Balozi katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York akifuatilia hotuba ya Mhe. Rais kwa pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy huku Bw. Noel Kaganda, Afisa katika Ubalozi wa Tanzania, New York akisikiliza kwa makini hotuba hiyo.
 
Balozi Tuvako Manongi wa Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York akiteta jambo na Mhe. Membe.

Mhe. Membe akimpongeza Mhe. Rais Kikwete mara baada ya kumaliza kulihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Mama Dorcas Membe naye akifurahia mara baada ya kumpongeza Mhe. Rais Kikwete.

Balozi Manongi akimpongeza Mhe. Rais kwa hotuba nzuri.
 

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri, Wabung na Watendaji mbalimbali kutoka Serikalini mara baada ya kulihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
 

Mhe. Rais Kikwete katika mahojiano na Bw. Joseph Msami, Mtangazaji kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Radio ya Umoja wa Mataifa mara baada ya kulihutubia Braza Kuu la Umoja wa Mataifa.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.