Wednesday, September 25, 2013

Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kosovo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kosovo, Mhe. Enver Hoxhaj walipokutana Mjini New York kwa mazungumzo kuhusu ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Mhe. Membe akizungumza na Mhe. Hoxhai.
Ujumbe wa Tanzania uliofuatana na Mhe. Membe wakati wa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kosovo. Kulia ni Grayson Ishengoma, Afisa Mambo ya Nje, Bi. Tully Mwaipopo, Afisa katika Ubalozi wa Tanzania, New York na Bw. Tolani Mavura, Msaidizi wa Waziri.
Mhe. Hoxhaj akizungumza na Mhe. mhe. Membe ambapo aliishukuru Tanzania kwa kuitambua nchi yake na kuomba ushirikiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili uimarishwe.
Mazungumzo yakiendelea.
Mhe. Membe akiagana na Mhe. Hoxhaj mara baada ya mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.