Tuesday, May 24, 2016

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mipango wa Korea Kusini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Mipango na Uratibu kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Korea, Mhe. Balozi Paik Ji-ah. Mazungumzo yao yalijikita katika kukuza mahusiano baina ya Tanzania na Korea Kusini katika nyanja za   miundombinu, biashara na afya. Waziri Mahiga alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi Paik kwa ushirikiano wanaouendeleza katika kuisaidia Tanzania ikiwemo mchango wao kwenye ujenzi wa Daraja la Malagarasi huko Kigoma na miradi mingine ya barabara.Mhe. Balozi Ji-ah yupo nchini kwa ziara ya siku tatu.
Ujumbe ulioambatana na Mhe. Balozi Paik Ji-ah nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi  Ji-ah. Kulia ni Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Song Geum-young.
Balozi Ji-ah akiendelea kuelezea jambo huku Waziri Mahiga akimsikiliza kwa makini.
Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Song Geum-young (kulia) akichangia jambo katika mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Naibu Balozi Mhe. Paik Ji-ah kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Korea Kusini
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) pamoja na Afisa Mambo Nje Bi. Bertha Makilagi nao wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea.
Waziri Mahiga akiagana na mgeni wake Balozi Paik Ji-ah mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Dkt. Mahiga akiagana na Balozi Geum-young.
Dkt. Mahiga na wageni wake wakiwa katika picha ya pamoja.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.