Monday, May 23, 2016

Utaratibu wa matumizi ya Wimbo na Bendera ya Afrika Mashariki

TAARIFA KWA UMMA


Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kutoa utaratibu wa matumizi ya Bendera na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  kama ilivyotangazwa hivi karibuni.

Utaratibu huo ni kwamba  Bendera ya Taifa itaanza kupeperushwa ikifuatiwa na Bendera ya  Jumuiya ya Afrika Mashariki, vivyo hivyo Wimbo wa Taifa utaanza kupigwa ukifuatiwa na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Itakumbukwa kuwa hivi karibuni, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilitatangaza kuhusu matumizi ya Bendera na Wimbo wa  Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Wizara, Idara, Mashirika na Taasisi mbalimbali za Serikali pamoja na Taasisi Binafsi.

Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unapatikana katika tovuti ya Wizara ambayo ni www.foreign.go.tz.

Aidha, kwa mujibu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki  vipimo maalum vya kutengeneza Bendera hiyo ni kama vinavyoonekana hapa chini.






Imetolewa na,
 Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 23 Mei, 2016.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.