Friday, May 6, 2016

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Balozi wa China nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa China hapa nchini Balozi Lu Youqing alipofika Wizarani kwa mazungumzo yao yaliyojikita kwenye kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizi mbili hususan katika masuala ya Biashara, Uchumi na Elimu. Katika mazungumzo hayo Balozi Mlima alimshukuru Balozi Youqing kupitia nchi yake kwa kuisaidia Tanzania kwenye ujenzi wa miundombinu. 
Balozi Youqing naye akizungumza na kumweleza Balozi Mlima kuwa nchini yao itaendelea kuboresha mahusiano ya kihistoria yaliyopo kati ya Tanzania na China.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) na Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia kwa makini mazungumzo hayo kati ya Balozi Mlima na Balozi Youqing (hawapo pichani)   
Mazungumzo yakiendelea
Katibu Mkuu Balozi Aziz Mlima akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Lu Youqing

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.