Tuesday, May 3, 2016

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati akutana na Balozi wa Palestina

 Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Abdalah Kilima akimkaribisha Balozi wa Palestina nchini, Mhe. Hazem Shabat alipomtembelea na kufanya naye mazungumzo katika ofisi za Wizara.
Mabalozi walizungumza juu ya kudumisha na kuimarisha mahusiano na ushirikiano uliopo baina ya Serikali ya Tanzania na Mamlaka ya Palestina.
Kushoto ni Afisa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Bw. Tahir Khamis akifuatilia mazungumzo hayo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.