Monday, March 4, 2024

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NJE ASHIRIKI MKUTANO WA KAMATI YA KUDUMU YA MAKATIBU WAKUU WA SADC


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu Mussa ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kinachofanyika jijini Luanda, Angola tarehe 4 – 5 Machi, 2024.

Kikao hicho kitafuatiwa na kikao cha Kamati ya Fedha tarehe 6 Machi, 2024 ambapo kwa pamoja vikao hivyo ni maandalizi ya Baraza la Mawaziri litakalofanyika tarehe 10 - 11 Machi, 2024 jijini Luanda, Angola.

Aidha, pamoja na mambo mengine vikao hivi vya awali vitapokea na kujadili taarifa zifuatazo: Tathmini ya utekelezaji wa maamuzi ya Mikutano iliyopita, Hatua iliyofikiwa katika kugharamia utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Maendeleo wa SADC wa 2020–2030, Taarifa  ya Kamati ya Fedha, Taarifa ya Kamati ya Rasilimali Watu na Utawala, Hatua iliyofikiwa katika kutafsiri nyaraka muhimu za SADC kwa lugha ya Kiswahili na nyinginezo.

Kauli mbiu ya Baraza la Mawaziri la mwaka huu ni ‘’Rasilimali Watu na Fedha: Nyenzo muhimu kwa ukuaji Endelevu wa Viwanda katika Kanda ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)”.


      Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kinachofanyika jijini Luanda, Angola tarehe 4 – 5 Machi, 2024.

       Meza kuu ikiongoza majadiliano katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika jijini Luanda, Angola tarehe 4 – 5 Machi, 2024. Katikati ni Katibu Mtendaji wa SADC, Bw. Elias Magosi na kushoto ni Naibu Katibu Mtendaji wa SADC, Bi. Angele  Makombo N’tumba

   Ujumbe kutoka Eswatin ukifuatilia Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)

Kikao kikiendelea.

     Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa (wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu wa SADC wanaoshiriki Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kinachofanyika jijini Luanda, Angola tarehe 4 – 5 Machi, 2024.







No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.