Thursday, March 21, 2024

NAIBU WAZIRI WA USHIRIKIANO WA MAENDELEO WA SWEDEN AZURU NCHINI


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akisalimiana na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana Janse alipomlaki katika uwanja wa ndege wa jijini Dodoma

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana Janse amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kuanzia tarehe 21 – 22 Machi, 2023 na kupokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa jijini Dodoma.

Lengo la ziara hiyo ni kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi uliopo kati ya Tanzania na Sweden. Pia kupitia ziara hiyo Serikali ya Sweden inatarajiwa kueleza dhamira ya kuongeza muda wa Mpango wa Maendeleo unaotarajiwa kafikia ukomo mwaka huu 2024.

Baada ya kuwasili Mhe. Janse amefanya mazungumzo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb.) ambapo katika mazungumzo yao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano katika sekta za viwanda, biashara, uwekezaji na ujenzi wa miundombinu hususan uendelezaji wa mradi wa mabasi yaendayo kasi (Bus Rapid Transit Project).

Viongozi wengine aliofanya nao mazungumzo jijini Dododma ni pamoja na, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (Mb.) na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb.)

Vilevile, Mhe. Janse anatarajia kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk tarehe 22 Machi 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Tanzania na Sweden zilianzisha ushirikiano tangu mwaka 1960 ambapo nchi hizo zimekuwa zikishirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta za nishati, tafiti, elimu, usimamizi wa mazingira, uchangiaji wa bajeti ya Serikali, biashara, viwanda, uwekezaji na miundombinu.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akisalimiana na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mhe. Charlotta Ozaki Macias wakati wa mapokezi ya Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana Janse jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akisalimiana na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana Janse alipomlaki katika uwanja wa ndege wa jijini Dodoma. Kando yao ni Balozi Swahiba Mndeme, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na America
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana Janse akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akijadili jambo na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana Janse alipowasili jijini Dodoma
Picha ya Pamoja
Mazungumzo baina ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb.) na  Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana yakiendelea jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana  Janse akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb.) yaliyofanyika jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Deogratius Ndejembi akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden, Mhe. Diana  Janse yaliyofanyika jijini Dodoma
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.