Friday, March 15, 2024

WAZIRI BYABATO: IMARISHENI UHUSIANO WA TANZANIA NA KENYA, MASHIRIKA YA KIMATAIFA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.)  ametembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya na kuzungumza na watumishi wa ubalozi wa Tanzania jijini Nairobi 

Pamoja na mambo mengine, Mhe. Byabato amewataka watumishi wa ubalozi huo  kuendelea kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Kenya pamoja na Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo jijini Nairobi. 

Alipowasili nchini Kenya, Mhe. Byabato amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini huko, Mhe. Dkt. Bernard Kibesse.

Katika hatua nyingine, Waziri Byabato amekutana na kupata chakula cha jioni na Wabunge wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi katika Bunge la Afrika Mashariki. 

Aidha, Mhe. Byabato alitumia fursa hiyo kuwaasa na kuwakumbusha Wabunge kuendelea kuiwakililisha vyema Tanzania na kusimamia maslahi na misimamo ya nchi yetu. 

Waziri Byabato yupo Jijini Nairobi kushiriki Mkutano wa Tano Kikao cha Tatu cha Bunge la Afrika Mashariki linalofanyika Jijini Nairobi Kenya.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Bernard Kibesse alipowasili katika Ofisi za Ubalozi, Jijini Nairobi, Kenya


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato akizungumza na watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Bernard Kibesse

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Bernard Kibesse pamoja na watumishi wa ubalozi


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.