Friday, March 1, 2024

WAZIRI KEUL AZINDUA KITABU CHA MAISHA NA TAMADUNI ZA KICHAGA KILICHOANDIKWA KWA LUGHA YA KISWAHILI.

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Katja Keul akiwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Kisare Makore (kulia) na Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Utamaduni , Sanaa na Michezo  Dkt. Resani Mnata wakizindua  kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la wachaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili katika hafla iliyofanyika Old Moshi mkoani Kilimanjaro tarehe 01 Machi 2024.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Katja Keul akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la wachaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili

 

 

 Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Utamaduni , Sanaa na Michezo  Dkt. Resani Mnata akimkabidhi nakala ya kitabu mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi Naomi Zegezege katika hafla ya kuzindua kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la wachaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Hassan Mwamweta (katikati) aliposhiriki hafla ya uzinduzi wa  kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la wachaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili iliyofanyika Old Moshi mkoani Kilimanjaro



Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Katja Keul katika picha ya pamoja na baadhi ya wageni na washiriki wa hafla ya uzinduzi wa kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la wachaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili



Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Katja Keul akiwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Kisare Makore (wa kwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Utamaduni , Sanaa na Michezo  Dkt. Resani Mnata , Balozi wa Tanzania Ujerumani (wa pili kulia) wakitoa heshima katika kaburi la Mangi Meli aliyeuawa na wakoloni wa kijerumani wakati wa utawala wao
Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Katja Keul akiweka shada la maua katika kaburi la Mangi Meli aliyeuawa na wakoloni wa kijerumani  wakati wa utawala wao



wananchi wa kabila la Kichaga wakicheza ngoma za asili wakati wa hafla ya uzinduzi wa kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la wachaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili

 

 

 

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Katja Keul ameshiriki uzinduzi wa kitabu kinachoelezea maisha na tamaduni za kabila la kichaga kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

 

Wakati wa uzinduzi ambao umefanyika katika kigango cha Kidia,  Old Moshi, imeelezwa kuwa kitabu hicho ambacho kimetafsiri kazi ya mwandishi mchungaji Bruno Gutmann, kinalenga kutambua utumishi wa mchungaji huyo raia wa Ujerumani ambaye aliishi eneo hilo kwa miaka 28 na kushirikiana na wananchi wa maeneo hayo huku akieneza injili.

 

 

Kitabu hicho ni miongoni mwa vitabu 400 vilivyoandikwa kwa lugha ya Kijerumani na mchungaji huyo ambapo mpaka sasa vitabu vitano vimeandikwa kwa  lugha nyingine ikiwemo kichaga na kiswahili.

 

Uzinduzi huo pia umeshuhudiwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro  Mhe. Kısare Makore, Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Hassan Mwamweta na Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Resani Mnata.

 

Naibu Waziri Keul yuko nchini kwa ziara ya siku nne ya kikazi kuanzia tarehe 29 Februari hadi Machi 4 2024.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.