Friday, March 8, 2024

WANAWAKE WA WIZARA YA MAMBO YA NJE WALIVYOADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Watumishi Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wameungana na wanawake wengine duniani kote kuadhimisha siku ya wanawake leo Machi 8, 2024.

 

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yamefanyika kitaifa jijini Dodoma katika Wilaya ya Chamwino ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ambaye aliwakilishwa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima.

 

Pamoja na mambo mengine, uzinduzi wa Sera wa Taifa ya Maendeleo ya Wanawake umefanyika wakati wa maadhimisho hayo yenye kaulimbiu isemayo “Wekeza kwa Wanawake kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii”.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima (wa pili kulia) akiwasalimia Watumishi Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hawapo pichani) walipopita mbele ya jukwaa kuu wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika Wilayani Chamwino jijini Dodoma tarehe 08 Machi 2024. Kulia kwa Mhe. Dkt. Gwajima ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule
Sehemu ya Watumishi Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki waliopo Dodoma wakipita kwa furaha mbele ya jukwaa kuu wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani
Shamrashamra zikiendelea
Sehemu nyingine ta watumishi wanawake wa Wizara wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho hayo
Picha ya pamoja

Watumishi hao wakiwa na bango lenye kaulimbiu ya maadhimisho hayo

Shamrashara za maadhimisho ya siku ya waawake zikiendelea

Sehemu ya watumishi wanawake wa Wizara wakati wa maadhimisho hayo


Sehemu ya watumishi wanawake wa Wizara wakati wa maadhimisho hayo

Watumishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara za Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), Mpango wa Hiari wa Afrika wa kujipima kwa Vigezo vya Utawala Bora (APRM) na Kituo cha Usiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika jijini Dodoma

...Maadhimisho katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Sehemu ya Watumishi Wanawake wa Wizara waliopo Ofisi Ndogo za Wizara zilizopo jijini Dar es Salaam nao hawakubaki nyuma kushiriki maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kama wanavyoonekana pichani.

Watumishi hao wakiwa katika picha ya pamoja



 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.