Monday, March 4, 2024

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE UJERUMANI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) amekutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani anayehusika na Afrika, Mhe. Katja Keul, jijini Dar es Salaam. 

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na Ujerumani. Uhusiano baina ya Tanzania na Ujerumani ni ya kihistoria na yanaonekana katika sekta za utalii, elimu, afya, utamaduni, biashara na uwekezaji pamoja na ushirikiano kupitia miji dada (Twin sister city relations).

Mhe. Keul aliwasili nchini tarehe 29 Februari 2024 kwa ziara ya kikazi ya siku nne (4) ambapo amehitimisha ziara yake nchini leo tarehe 04 Machi, 2024. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani anayehusika na Afrika, Mhe. Katja Keul, jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani anayehusika na Afrika, Mhe. Katja Keul, walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam

Kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani anayehusika na Afrika, Mhe. Katja Keul, kikiendelea jijini Dar es Salaam




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.