Saturday, March 23, 2024

TANZANIA –KENYA ZAKUBALIANA KUONDOA VIKWAZO VYA KIBIASHARA

Tanzania na Kenya zimekubaliana na kutia saini makubaliano ya kuondoa vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru ili kuruhusu raia kutoka nchi hizo kufanya biashara baina yao kwa urahisi na kwa manufaa ya pande zote mbili. 

Makubaliano hayo yamefikiwa na kutiwa saini na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Kenya Mhe. Rebbecca Miano wakati wa Mkutano wa nane (8) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya katika ngazi ya Mawaziri uliofanyika Kisumu,Kenya tarehe 22/03/2024. 

Mkutano huo ulianza kwa ngazi ya watalaam kisha ngazi ya Makatibu Wakuu ambapo zaidi ya vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru zaidi ya 14 vilijadiliwa na kuwekewa mpango wa kuendelea kuviondoa vyote. Tanzania na Kenya ni wabia wakubwa wa biashara na hivyo kuondolewa kwa vikwazo hivyo vitasaidia kuongezeka mara dufu kiwango cha kifanyika kwa biashara baina ya mataifa hayo.

Viongozi wengine walioshiriki katika Mkutano huo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masala ya EAC Balozi Stephen P. Mbundi, Waziri wa Afrika Mashariki na Maendeleo ya Kikanda wa Kenya Mhe. Peninah Malonza, Makatibu Wakuu wanaohusika na masuala ya uwekezaji, viwanda, biashara na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Dkt. Bernard Yohana Kibese na Balozi wa Kenya nchini Tanzania Mhe. Isaac Njenga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Kenya Mhe. Rebbecca Miano wakionesha hati za makubalino ya kuondoa vikwako vya biashara visivyo vya kiforodha kwenye mkutano uliofanyika mjini Kisumu baina ya Tanzania na Kenya tarehe 22/03/2024. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Kenya Mhe. Rebbecca Miano wakisaini makubalino ya kuondoa vikwako vya biashara visivyo vya kiforodha kwenye Mkutano wa nane (8) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya katika ngazi ya Mawaziri uliofanyika Kisumu,Kenya tarehe 22/03/2024. 
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Benjamin Mwesiga akichangia hoja kwenye Mkutano wa nane (8) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya uliofanyika Kisumu,Kenya tarehe 22/03/2024. 
Wajumbe wakifuatilia Mkutano wa nane (8) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya katika ngazi ya Mawaziri wa kuondoa vikwako vya biashara visivyo vya kiforodha uliofanyika Kisumu,Kenya tarehe 22/03/2024.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.