Monday, September 8, 2014

Waziri Membe apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi wapya wa Rwanda na Norway hapa nchini



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mpya wa Rwanda hapa nchini, Mhe. Eugene Sayore Kayihura. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ofinini kwa Mhe. Membe tarehe 08 Septemba, 2014.
Waziri Membe akizungumza na Balozi Kayihura mara baada ya kuwasilisha Nakala za hati za utambulisho. Katika mazungumzo hayo Mhe. Membe alimhakikishia ushirikiano Balozi huyo na kumwomba awe huru katika kutekeleza majukumu yake ya kazi wakati wote akiwa hapa nchini.
Balozi Kayihura akiwa na Maafisa Waandamizi wa Ubalozi wa Rwanda hapa nchini aliofutana  nao. Katikati ni  Bw. Sano Lambert na  Bw. Ernest Bugingo.
Mhe. Membe akimsikiliza Balozi Kayihura wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Membe akiagana na Balozi Kayihura.


.................Mhe. Membe akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Norway nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Norway hapa nchini, Mhe. Hanne-Marie Kaarstad. Hafla hiyo ilifanyika Ofisini kwa Mhe. Waziri tarehe 08 Septemba, 2014.
Mhe. Membe akizungumza na Balozi Kaarstad mara baada ya kupokea Nakala za hati za utambulisho za Balozi huyo

Balozi Kaarstad na ujumbe aliofuatana nao wakimsikiliza Waziri Membe (hayupo pichani)
Mhe. Membe akiagana na Balozi Kaarstad.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, anatarajiwa kuwasili nchini siku ya Jumatano asubuhi, tarehe 10 Septemba, 2014 kwa ziara ya kikazi ya siku moja.


Katika ziara hiyo nchini, Mhe. Museveni atakuwa na mazungumzo na mwenyeji wake, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ikulu, Dar es Salaam. Rais Museveni ataondoka baadaye siku hiyo hiyo kurejea nyumbani.



IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Waziri Membe apokea Hati za Utambulisho za Mratibu Mkazi mpya wa UN nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akipokea Hati za Utambulisho za Mratibu Mkazi mpya wa  Umoja wa Matiafa hapa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez.  Hafla hiyo fupi ilifanyika Ofisini kwa Mhe. Membe tarehe 08 Septemba, 2014.
Mhe. Membe akizungumza na  Bw. Rodriguez mara baada ya kupokea Hatiza ke za Utambulisho. ambapo alimhakikishia ushirikiano.
Bw. Rodriguez pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (katikati) na Bi. Hoyce Temu, Afisa kutoka Ofisi za Umoja wa Mataifa wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Mhe. Membe akiagana na Bw. Rodriguez mara baada ya mazungumzo yao.

Katibu Mkuu akutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Ireland

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje naUshirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ireland, Bw. Niall Burges mara baada ya kukutana kwa mazungumzo. Bw. alikuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya siku nne.
Bw. Haule na Bw. Burges wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ireland hapa nchini, Mhe. Fionnuala Gilsenan
Bw. Haule, Bw. Burges na Mhe. Gilsenan wakiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Idara za Ushirikiano wa Kimataifa na Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa kwanza kushoto) na Balozi Joseph Sokoine (wa kwanza kulia)

Wednesday, September 3, 2014

Naibu katibu Mkuu ashiriki hafla ya miaka 69 ya Taifa la Vietnam

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akisoma hotuba wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 69 ya Taifa la Vietnam iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 02 Septemba, 2014 na kuhudhuriwa na Mabalozi  wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wageni waalikwa.
Balozi wa Vietnam nchini Mhe. Vo Thanh Nam (kushoto) akiwa na Balozi wa Cuba nchini. Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo (wa tatu kushoto) pamoja na Bi. Samira Diria (wa kwanza kulia), Afisa Mambo ya Nje wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 69 ya Taifa la Vietnam.
Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Zakaria Anshar (kushoto) akiwa na Bw. Emmanuel Luangisa (katikati), Afisa Mambo ya Nje pamoja na Afisa kutoka Ubalozi wa Vietnam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 69 ya Taifa la Vietnam.
Sehemu ya Wageni waalikwa wakiwemo Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakimsikiliza Balozi Gahama akihutubia wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 69 ya Taifa la Vietnam iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam
Kaimu Murugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Nathaniel Kaaya akimpongeza Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Vo Thanh Nam kwa miaka 69 ya uhuru wa taifa lake.

Picha na Reginald Philip

Tuesday, September 2, 2014

Press Release

H.E. Truong Tan Sang, President of Vietnam

PRESS RELEASE

H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency Truong Tan Sang, President of the Socialist Republic of Vietnam.

The message reads as follows:-

“Excellency Truong Tan Sang,
  President,
  Socialist Republic of Vietnam
  HANOI.

Your Excellency and Dear Brother,

On the auspicious occasion of the 69th anniversary of the National Day of the Socialist Republic of Vietnam, the Government and the People of the United Republic of Tanzania join me in extending to you and through you to the Government and People of the Socialist Republic of Vietnam our heartfelt and sincere congratulations.

Tanzania and Vietnam have since the establishment of diplomatic relations demonstrated close friendship and solidarity in different spheres and supported each other at different international for a. Tanzania is determined to keep and further strengthen this relationship in the years ahead.

Please accept, Your Excelency and Dear Brother, the assurances of my highest consideration along with my personal best wishes for your continued good health and happiness as well as the progress and the prosperity of the people of Vietnam”.

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

02nd September 2014

Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai akutana na uongozi wa juu wa Hospital ya Iran ya Dubai


Mhe. Omar Mjenga akiwa katika picha ya pamoja na mwenyeji wake Dk. Asghar Fashad.
Mhe. Omar Mjenga akizungumza na Uongozi wa Juu wa Hospitali ya Iran, akiwemo Mkurugenzi Mkuu Dk. Asghar Fashad.

Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Iran Dkt. Asghar Fashad akizungumza.

===========================================

Mhe. Omar Mjenga, Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai, leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Iran ya Dubai, Dr. Asghar Fashad. Katika mazungumzo, Mhe. Mjenga alimuomba Dr asghar kuangalia uwezekano wa kuwa na makubaliano kati ya hospitali yake na Ubalozi Mdogo kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa Watanzania kwa gharama nafuu ukilinganisha na gharama zake za sasa. 

Baada ya mazungumzo na mashauriano ya muda wa saa moja, Uongozi wa Juu wa Hospitali, ulikubali ombi la Mhe. Mjenga la kupunguza gharama za matibabu kwa Watanzania kwa asilimia 40 (40%). Mwanzo, Uongozi ulipendekeza asilimia 20, ambayo Mhe. Mjenga aliwaeleza kuwa bado ilikuwa ni punguzo dogo na bado ingekuwa ni mzigo mkubwa kwa Watanzania. Hatmaye, ndio maafikiano hayo yakafikiwa ya asilimia 40.

Mpango wa huu utajumuisha Watanzania wote waishiyo UAE na wale wanaoishi nje ya UAE ikiwa ni pamoja na wale wanaoishi Tanzania. Hospital ya Irani ni moja ya hospitali zenye huduma za hali ya juu kwa hapa Dubai na UAE kwa ujumla.

Uongozi wa Hospitali umekubali kuanza kutoa Vitambulisho Maalum kwa ajili ya Watanzania wote kuanzia Jumapili tarehe 1 Septemba. Mkataba wa Makubaliano haya utatiwa saini Jumatatu tarehe 2 Septemba.

Aidha, Mhe. Mjenga, amemuomba Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hii, kuangalia uwezekano wa kujenga Hospitali kubwa yenye hadhi kama hii, nchini Tanzania. Kimsingi, Mkurugenzi Mkuu amekubali ombi hili, na ameahidi kumuomba Rais wa Hospitali kufanya ziara nchini Tanzania mwezi ujao ili kuona na uongozi husika na kuanza mazungumzo ya kuanzisha Hospitali kama hiyo. Ameeleza kuwa Tanzania na Iran na nchi marafiki wa siku nyingi, na hivyo Iran inafarijika sana kuwa karibu na Tanzania kimahusiano.


Monday, September 1, 2014

Wizara yapokea Computer ndogo 20 kutoka Ubalozi Mdogo wa Dubai

Mkuu wa kitengo cha Tecknolojia ya Habari na Mawasiliani (TEHAMA) Bw. Isaac Kalumuna akabidhi moja ya Computer ndogo kwa Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano ya Serikali Bi. Mindi Kasiga, Computer hizo ni jitihada kutoka kwa Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai Bw. Omar Mjenga

Picha na Reginald Philip

Mhe. Omar Mjenga akutana na Rais na Mtendaji Mkuu wa Dubai Chamber of Commerce

Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai Mhe. Omar Mjenga akutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Hamad Buamim, Rais na Mtendaji Mkuu wa Dubai Chamber of Commerce and Industry.
-----------------------------------------------------------------------


Mhe. Omar Mjenga, amekutana na Mhe. Hamad Buamim, Rais na Mtendaji Mkuu wa Dubai Chamber of Commerce and Industry na kufanya naye mazungumzo.

Katika mazungumzo, wamejadiliana uwezekano wa kuwa na ziara ya kibiashara kwenda Tanzania, kwa makampuni na viwanda vilivyopo Dubai, ili kukutana na wafantabiashara na wamilikiwa viwanda Tanzania, ilikujionea na kuibua furs za uwekezaji. Wamekubaliana ziara hiyo ifanyike mwanzoni mwa mwaka kesho na hivyo basi kuanza maandalizi mapema
Mwezi Novemba, kutakuwa na ziara ya kibiashara ya makampuni kutoka Flame ya Ajman.

Aidha, wamezungumzia kuhusu mkutano wa Africa Global Business Forum utakaofanyika tarehe 1 - 2 Oktoba 2014 hapa Dubai.
Mtukufu Sheikh Mohammed bin Rashid al Maktoum amemwalika Rais Kikwete kuhudhuria pamoja na marais wengine wa Mali, Ghana, Uganda, Mozambique, Ethiopia, Senegal, Burkina Faso, Sudan na Ivory Coast.

Mkutano huu hufanyika kila mwaka ambao huzungumzia njia muafaka wa ushirikiano kati ya Serikali ya Dubai na UAE kwa ujumla na nchi za Afrika.



Saturday, August 30, 2014

Dkt. Jabiri Bakari, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa E- Government na Ujumbe wake wa mtembelea Balozi wetu Mdogo Dubai

Mhe. Omar Mjenga, Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai akisalimiana na Dkt.Jabir Bakari, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa e-Government pamoja na ujumbe wake wakitokea New Delhi ambako walikuwa na mkutano na Wakala wenzao wa Serikali ya India. Katika mazungumzo yao, wamezungumzia jinsi ya kupata ufadhili kwaajili ya kujenga uwezo wa Wakala wa Serikali kwa njia ya Mtandao(e- Government)

Mhe. Omar Mjenga, Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai akiongea na Dkt. Jabir Bakari, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa e-Government pamoja na ujumbe wake.
Picha ya pamoja


Friday, August 29, 2014

Mhe. Omar Mjenga akutana na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai

Mhe. Mjenga akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Lootah mbele ya baadhi ya miradi inayojengwa na Nakheel.
Mhe. Mjenga akifanya mazungumzo kati Mwenyekiti Lootah, katika ofisi za Nakheel.
Mhe. Omar Mjenga akutana na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai (NAKHEEL) Bwa. Rashid Lootah.

Balozi Mdogo wa Tanzania- Dubai, mhe. Omar Mjenga, leo amemtembelea na kufanya mazungumzo na Bw. Rashid Lootah, Mwenyekiti wa Nakheel, Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai.

Katika mazungumzo yao, wamezungumzia ziara ya Mwenyekiti huyo pamoja na ujumbe wake kuitembelea Tanzania, itakayofanyika kuanzi tarehe 16-20 Septemba, ambako anatarajia pamoja na kuonana na baadhi viongozi wa Serikali, watafanya mazungumzo na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) yatakayowezesha kusainiwa makubaliano ya ushirikiano kwenye sekta ya nyumba kati ya mashirika hayo mawili.

Aidha, watapata fursa ya kukitembelea kituo cha uwekezaji - TIC ili kupata taarifa muhimu za uwekezaji.

Aidha, Mhe. Mjenga amemuomba Mwenyekiti huyo kufadhili mkutano wa Uwekezaji kwenye Sekta ya Utalii utakaofanyika Novemba hapa Dubai. Mkutano huo unaandaliwa na Ubalozi Mdogo kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii ya Tanzania-TTB pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan afanya ziara nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje kutoka Japan Mhe. Hirotaka Ishihara mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku tatu hapa nchini. Katika ziara hiyo Mhe. Ishihara amembatana na ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Japan.Anayeshuhudia katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Nathaniel Kaaya.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. hAULE  pamoja na Naibu  Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Ishihara wakimsikiliza Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaki Okada alipokuwa akiwaeleza jambo mara baada ya mapokezi ya Mhe. Ishihara.


Picha na Reginald Philip.

Thursday, August 28, 2014

Ziara ya Mhe. Naibu Waziri nchini Singapore

Mhe. Dkt.  Mahadhi Juma Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye mazungumzo na mwenyeji wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara Mhe. Kasiviswanathan Shanmugam, Waziri wa Mambo ya Nje wa Singapore. 
Mhe. Dkt.  Mahadhi Juma Maalim (wa pili kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye picha ya pamoja na Mhe. Kasiviswanathan Shanmugam, Waziri wa Mambo ya Nje wa Singapore (wa tatu kushoto), Balozi Mbelwa Kairuki (kulia) na Mhe. John Kijazi (kushoto), Balozi wa Tanzania nchini India na Singapore.  

Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (wa tatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mawaziri saba wa Mambo ya Nje wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara wakiwa na mwenyeji wa Mkutano huo Waziri wa Mambo ya Nje wa Singapore Mhe. Kasiviswanathan Shanmugam (wa tano kutoka kushoto). 
Mawaziri wa Mambo ya Nje wakiwa kwenye ziara kwenye mojawapo ya vyuo maalum nchini Singapore Institute of Technical Education ambapo Tanzania inashirikiana nacho kwenye kutoa mafunzo kwa walimu wa VETA. 

 ....Ufunguzi wa Ubalozi wa Heshima wa Tanzania nchini Singapore

Mhe. Dkt.  Mahadhi Juma Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (kushoto) akikata utepe kufungua rasmi ofisi za Ubalozi wa Heshima za Tanzania nchini Singapore akishirikiana na Mhe. S.S. Teo, Balozi wa Heshima. Kulia ni Mhe. John Kijazi, Balozi wa Tanzania nchini India ambaye pia anaiwakilisha Tanzania nchini Singapore.
Mhe. Dkt.  Mahadhi Juma Maalim (wa pili kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye picha ya pamoja na Mhe. John Kijazi (wa kwanza kushoto), Balozi wa Tanzania nchini India ambaye pia anaiwakilisha Tanzania nchini Singapore, Mhe.S.S. Teo, Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Singapore na Balozi Mbelwa Kairuki, Murugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa



Waziri Nagu asaini Kitabu cha Maombolezo Ubalozi wa Ireland

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Mhe. Dkt. Mary Nagu (Mb) akisalimiana na Balozi wa Ireland, Mhe. Fionnuala Gilsenan mara baada ya kuwasili kwenye Ubalozi wa nchi hiyo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Ireland, Hayati Albert Reynolds kilichotokea tarehe 21 Agosti, 2014.
 Mhe. Dkt.  Nagu (Mb) akisaini kitabu hicho cha maombolezo huku Balozi Gilsenan akishuhudia. 
Mhe. Dkt. Nagu na Balozi Gilsenan wakiwa katika mazungumzo.


Picha na Reginald Philip



President Shein meets new UNFPA Country Representative

President of the Revolutionary Government of Zanzibar, H.E. Dr. Ali Mohammed Shein welcomes Dr. Nathalia Kanem, a new Country Representative of United Nations Population Fund  (UNFPA) at the State House in Zanzibar when she paid a courtesy call  on Wednesday 27th August, 2014.
H.E. President Shein shake hands with the Director of Multilateral Cooperation Department in the Ministry of Foreign Affairs and International and Cooperation, Ammbassador Celestine Mushy during their visit with Dr. Kanem to the State House in Zanzibar.

H.E. President Shein welcomes one of  UNFPA Senior Officials who accompanied Dr. Kanem.
H.E President Shein in a discussion with Dr. Kanem and her team during their meeting at the State House in Zanzibar.
H.E. President Shein gives a present to Dr. Kanem during her visit to the State House in Zanzibar.


Wednesday, August 27, 2014

ANNOUNCEMENT FOR NOMINATION OF CANDIDATES FOR MEDIATION TEAM



ANNOUNCEMENT FOR NOMINATION OF CANDIDATES FOR THE DEPARTMENT OF POLITICAL AFFAIRS’ STANDBY TEAM OF MEDIATION AT THE UNITED NATIONS SECRETARIAT.
      
 We wish to inform the general public that the United Nations Secretariat, through the Department of Political Affairs (DPA) is seeking the nomination of candidates for the 2015 Standby Team of Mediation Experts to undertake mediation assignments effective from February 2015, for a one-year term. 

         The Team once duly constituted will be composed of eight experts whose work shall concentrate on the following thematic areas: (1) constitutional-making; (2) natural resources; (3) power-sharing arrangements; (4) gender and inclusion issues; (5) security arrangements; and (6) mediation and dialogue process design (three positions).   

         Please note that member of the Team are engaged on a full-time basis with the DPA, and deploy on short notice to the field in support of ongoing good offices and mediation work. In between deployments, the experts carry out research and analysis on mediation issues, as defined by DPA. 


          The deadline for submission of nomination (including the full name, title, contact details and resumes of the nominees) is 14 September 2014. Nomination of women with knowledge of French and Arabic languages is highly encouraged. Supplementary information about the Standby Team of Mediation may be retrieved from the following site: http://peacemaker.un.org/mediation-support/stand-by-team.