Wednesday, October 5, 2016

Rais Kabila aweka Jiwe la Msingi la Jengo la Bandari ya Dar es Salaam nchini Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe. Joseph Kabila Kabange akikata utepe pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (wa kwanza kulia), na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Pro. Makame Mbarawa (wa kwanza kulia) wakati wa kuweka jiwe la msingi katika Jengo la Mamlaka ya Bandari lililopo nchini Jijini Dar es Salaam. Mhe. Magufuli amatumia nafasi hiyo kumuhakikishia Mhe. Kabila kuwa wafanyabiashara kutoka Congo hawatopata matatizo kwa kutumia Bandari ya Dar es Salaam, kwa kuwa Serikali imerekebisha mapungufu yaliyokuwepo kipindi cha nyuma.
Rais Kabila na Dkt. Magufuli pamoja na Prof. Mbarawa wakifurahia kwa pamoja kwa kupiga makofi mara baada ya kumaliza uwekaji wa Jiwe la msingi la Jengo la Mamlaka ya Bandari Jijini Dar es Salaam
Marais wakiangalia michoro ya jengo jipya la Mamlaka ya Bandari
Mhe. Kabila pamoja na Mwenyeji wake Rais Magufuli wakipata maelezo juu michoro ya Ghorofa hilo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu Mhandisi, Deusdedit Kakoko (aliyeshikilia kipaza sauti).


Rais Kabila akipokea zawadi inayoonesha mwonekano wa Bandari ya Dar es Salaam 
Viongozi mbalimbali wa Serikalini wakishuhudia tukio la hilo la uwekwaji wa Jiwe la Msingi wa Jengo la Mamlaka ya Bandari. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Aziz Mlima.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo Mhe. Joseph Kabila Kabange pamoja na viongozi mbalimbali alioongozana nao. 

Tuesday, October 4, 2016

Rais Dkt. Magufuli akutana na Rais Kabila Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe. Joseph Kabila. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Oktoba, 2016. Mhe. Rais Kabila yupo nchini kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Mhe. Rais Magufuli akipeana mkono na Rais Kabila mara baada ya mazungumzo kati yao
Mhe. Rais Magufuli akizungumza na Waandishi wa  Habari (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano waliyokubaliana na Rais Kabila.
Mhe. Rais Kabila naye akizungumza na Wanahabari na Wageni waaalikwa
Wakuu wa Vyombo vya Usalama nchini wakifuatilia mkutano Ikulu
Balozi wa DRC nchini, Mhe. Jean Pierre Mutamba (kushoto) na wageni wengine waalikwa wakiwa Ikulu
Rais John Pombe Magufuli na Rais Joseph Kabila wakishuhudia uwekwaji saini wa Makubaliano kati ya Tanzania na DRC kuhusu Utafiti na Uendelezaji wa Utafiti wa Mafuta katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika.
Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Mhongo na Mwenzake wa DRC wakibadilishana Mkataba huo wa Makubaliano mara baada ya kuusaini
Mazungumzo rasmi
Mhe. Rais Magufuli akimpatia Rais Kabila zawadi ya Kinyago mashuhuri cha Umoja kinachoonesha Umoja na Mshikamano wa Watanzania.
Rais Kabila naye akimpatia Rais Magufuli zawadi
Picha ya pamoja
Rais Kabila akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga
Rais Kabila akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, . Dkt. Aziz Mlima
Rais Kabila akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo
Mhe. Rais Magufuli akiwa ameongozana na mgeni wake Mhe. Rais Kabila alipompokea Ikulu

Makamu wa Rais wa Cuba ahitimisha ziara yake nchini

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa akipungia wananchi wa Zanzibar waliojitokeza kumuaga katika uwanja wa ndege wa Abeid Aman Karume, Zanzibar. Mhe. Mesa aliondoka Zanzibar mapema leo asubuhi na kuwasili Dar es Salaam  ambapo alielekea Kibaha kutembelea mradi unaofadhiliwa na Cuba  nchini wa kuzalisha dawa za kuua viluwiluwi wa mbu wanaoeneza Malaria.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ameambatana na Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akiondoka nchini baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku tatu.

Makamu wa Rais wa Cuba atembelea Kiwanda cha Dawa za Mbu kilichopo Kibaha

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa akisalimiana na Dkt. Samuel Nyantahe,  Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha Dawa za Kuua Viluwiluwi wa Mbu kilichopo Kibaha, Pwani mara baada ya kuwasili Kiwandani hapo kwa ajili ya kukitembelea. Katikati yao ni Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu.
Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Bw. Mkucha akitoa taarifa fupi kuhusu Kiwanda hicho ambapo alisema kitaanza uzalishaji mwezi Oktoba, 2016 na tayari kimeajiri watu 126. Kiwanda hicho ambacho kimejengwa kwa ushirikiano wa Tanzania na Cuba kina uwezo wa kuzalisha lita milioni 6 za dawa ambazo zitatosheleza matumizi ya Tanzania na nchi nyingine jirani.
Sehemu ya Wananchi na Wageni waalikwa waliohudhuria tukio hilo
Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa akizungumza kuhusu umuhimu wa Kiwanda hicho katika kupambana na malaria na kwamba Serikali ya Cuba itaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania katika kupambana na ugonjwa huo.
Mhe. Mesa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Viongozi wa Wataalam kutoka Cuba wanaofanya kazi Kiwandani hapo
Mtaalam mwingine kutoka Cuba akitoa maelezo ya namna maabara kiwandani hapo zinavyofanya kazi
Mhe. Mesa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Wataalam wanaofanya kazi kiwandani hapo
Mhe. Mesa akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kiwanda hicho.



Monday, October 3, 2016

Makamu wa Rais wa Cuba awasili Zanzibar

Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Abed Aman Karume, Zanzibar. Mhe. Mesa alipokelewa na Makamu wa Rais wa Pili Mhe. Balozi Seif Ali Iddi. Mhe. Mesa anatarajia kuondoka Zanziba tarehe 4 Oktoba, 2016. 
Mhe. Mesa akikagua gwaride maalum mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Abed Aman Karume Zanzibar


Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Mesa (kushoto) alipomtembelea Ikulu Zanzibar
Rais Mhe.Dkt. Shein akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na ujumbe wa Mhe. Mesa
Mazunguzo yakiendelea Ofisini kwa Makamu wa Rais wa Pili  wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi.
Makamu wa Rais wa Pili  wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika picha ya pamoja
Makamu wa Rais wa Pili  wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akiaagana na  Mhe. Nyusi mara baada ya mazungumzo.
Naibu wa Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba (wapili kulia) akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Mesa (hawako pichani)  


Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika  Balozi Joseph Sokoine akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Mesa (hawako pichani)


Sunday, October 2, 2016

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa awasili Nchini


Makamu wa Rais wa Jumhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpokea Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mhe. Mesa atakuwa Nchini kwa ziara ya siku tatu kuanzia tarehe 2- 4 Oktoba, 2016.

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Mesa akipokea ua kutoka kwa mtoto Atkah Omary mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Friday, September 30, 2016

Makamu wa Rais wa Cuba kufanya ziara ya siku tatu nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu ziara ya Makamu wa Rais wa Cuba Nchini, Mhe.Salvador Antonio Valdes Mesa anayetarajiwa kuwasili nchini kwa ziara ya siku tatu kuanzia tarehe 2 hadi 4 Septemba 2016.

Mhe. Waziri Mahiga akiendelea kuzungumza na Waandishi wa Habari kama wanavyoonekana pichani.

=============================================




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ziara ya Makamu wa Rais wa Cuba nchini Tanzania

Makamu wa Rais wa Baraza la Taifa la Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 02 Oktoba, 2016 kwa ziara rasmi ya siku tatu. Lengo la ziara hiyo ni kukuza na kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo baina ya Tanzania na Cuba pamoja na kuangalia maeneo mapya ya ushirikiano. Nchi nyingine anazotarajiwa kuzitembelea ni pamoja na Uganda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Botswana na Zimbabwe.

Shughuli mbalimbali zitakazofanyika wakati wa ziara
Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Mhe. Valdes Mesa atapokelewa na mwenyeji wake Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tarehe 03 Oktoba, 2016 Mhe. Mesa atakutana kwa mazungumzo ya faragha na Mhe. Samia Suluhu Ikulu yakifuatiwa na mazungumzo rasmi kati yao na wajumbe waliofuatana nao.

Aidha, Mhe. Mesa atakutana kwa mazungumzo mafupi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli.

Baada ya mazungumzo hayo, Mhe. Mesa na Mhe. Suluhu watakuwa na mkutano wa pamoja na Waandishi wa Habari kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Cuba.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mesa atakutana kwa mazungumzo mafupi na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Y. Ndugai katika Hoteli ya Hyatt Regency. Baadaye siku hiyo hiyo, atakutana na Ujumbe wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Hotelini hapo kabla ya kushiriki Chakula rasmi cha Mchana, Ikulu kilichoandaliwa kwa heshima yake na Mwenyeji wake Mhe. Suluhu.

Mhe. Mesa ataondoka Dar es Salaam tarehe 03 Oktoba, 2016 alasiri kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kuendelea na ziara yake Visiwani humo. Akiwa Zanzibar, Mhe. Mesa ambaye atapokelewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi atakutana kwa mazungumzo rasmi na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Dkt.  Ali Mohamed Shein, Ikulu ya Zanzibar.

Tarehe 04 Oktoba, 2016 Mhe. Mesa akiwa ameongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba atarejea Dar es Salaam akitokea Zanzibar kwa ajili ya kuendelea na ziara yake ambapo atatembelea Makumbusho ya Taifa.

Uhusiano wa Tanzania na Cuba
Uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Cuba ulianzishwa zaidi ya  miaka 50 iliyopita  na Viongozi Waasisi wa mataifa haya mawili, Rais Mstaafu wa Cuba, Mheshimiwa Fidel Castro na Baba wa Taifa, Hayati Julius K. Nyerere. Tangu Tanzania ipate uhuru Cuba imekuwa ikitusaidia katika maeneo mbalimbali ikiwemo afya, utamaduni, elimu, michezo, utalii, nishati, teknolojia na kilimo.

Ushirikiano katika Sekta ya Afya
Tanzania na Cuba zimekuwa zikishirikiana kwenye sekta ya afya ambapo hadi sasa kuna jumla ya Madaktari 30 kutoka Cuba wanaofanya kazi kwenye Hospitali mbalimbali Tanzania Bara na Zanzibar. Kati ya Madaktari hao 10 wapo Bara na 20 wapo Zanzibar wakiwemo wanaofundisha katika Kitivo cha Tiba, Chuo Kikuu cha Zanzibar na kutibu katika Hospitali mbalimbali Zanzibar.

Aidha, katika jitihada za Serikali za kupambana na malaria Serikali ya Cuba na Tanzania zilikubaliana kujenga Kiwanda cha Viuatilifu vya Kuua Viluwiluwi vya Mbu ambacho kimejengwa kwenye eneo la Viwanda Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani na kuzinduliwa mwezi Julai, 2015.

Kiwanda hicho ambacho kilijengwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Kampuni ya LABIOFAM ya Cuba kimekamilika na kwa sasa kinazalisha dawa za majaribio. Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha lita milioni 6 za viuatilifu kwa mwaka ambazo zinatosheleza kwa matumizi ya Tanzania na hata kuuzwa nchi nyingine za Afrika.

Sekta ya Elimu
Katika Sekta ya Elimu Tanzania na Cuba zimekuwa zikishirikiana kwenye programu mbalimbali ikiwemo nafasi za ufadhili wa masomo nchini Cuba kwa wanafunzi kutoka Tanzania. Kuanzia mwaka 2008 hadi 2014 jumla ya Watanzania 64 walipata ufadhili wa mafunzo nchini Cuba katika fani mbalimbali ikiwemo udaktari, uchumi, TEHAMA na Michezo.

Pia Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Cuba ilianzisha Programu ya Elimu kwa Vijana na Watu Wazima ambayo hutolewa kwa kutumia vifaa vya kufundishia vinavyomwezesha mwanafunzi kusikia na kuona (audiovisual). Inatarajiwa kwamba zaidi ya vijana na watu wazima milioni 3 watakuwa wameshiriki programu hii ifikapo mwaka 2017. Mradi wa majaribio ya program hii ulizinduliwa mwaka 2014 katika Manispaa za Ilala, Temeke, Kinondoni, Ilemela, Mwanga, Bagamoyo, Mkuranga na Songea.

Sekta ya Michezo
Katika Sekta ya michezo Serikali ya Cuba wametupatia Wakufunzi wa Ngumi, Judo na Riadha. Hivi sasa wanatoa nafasi za mafunzo nne kila mwaka kwenye mafunzo ya michezo na utaalamu wa mazoezi ya viungo.

Hivyo, pamoja na kutumia fursa ya ziara hiyo kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizi mbili Tanzania itatumia nafasi hiyo kujikita katika kuanzisha ushirikiano kwenye maeneo mapya hususan biashara na uwekezaji.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 30 Septemba 2016.


Waziri Mkuu apokea msaada wa Waathirika wa tetemeko la ardhi Kagera

Waziri Mkuu akipokea hundi ya Shilingi milioni 80 ikiwa ni msaada kutoka Serikali y Pakstan uliokabidhiwa na Kaimu Balozi wa Nchi hiyo Nchini Bw. Amir Khan kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.Hafla iliyofanyika Hotel ya Hyatt Jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako wakipokea hundi ya shilingi Milioni 60 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa yaliyoathiriwa na tetemeko la ardhi Mkoani Kagera kutoka Kampuni ya Simu ya Huawei ya nchini China. Wakwanza kushoto ni Mkurugezi wa Kampuni hiyo Nchini Bw. Bruce Zhang
Kaimu Balozi wa Pakstan nchini, Bw. Amir Khan akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi misaada ya wahanga wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza katika hafla hiyo
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri, Mabalozi na wadau wengine waliohudhuria makabidhiano hayo
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia ,Balozi Mbelwa Kairuki akifuatilia hafla ya makabidhiano ya msaada wa wahanga wa tetemeko la  ardhi Mkoani Kagera iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Jijini Dar es Salaam