Saturday, February 4, 2017

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


JPCC kati ya Tanzania na Malawi ni chachu ya kuimarisha mahusiano

Wajumbe wanaoshiriki katika Kikao cha 4 cha Tume ya Pamoja ya Kudumu ya  Ushirikiano (JPCC) kati ya Tanzania na Malawi kilichofunguliwa leo jijini Lilongwe, Malawi wamehimizwa katika majadiliano yao ya  siku tatu  kubuni mkakati utakaowezesha kutatua changamoto zinazojitokeza kutokana na muingiliano mkubwa wa ngazi mbalimbali za ushirikiano baina ya wananchi  wa  mataifa hayo mawili.

 Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya Wataalam, Balozi Ramadhan Mwinyi ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipokuwa anasoma hotuba ya ufunguzi.

"Kama mnavyofahamu kunapokuwa na maingiliano makubwa ya wananchi wa nchi mbili kama zilivyo nchi zetu, changamoto haziwezi kukosa kujitokeza. Hivyo ni jukumu letu sisi wataalamu kubuni mkakati wa kuhakikisha kuwa changamoto hizo zinashughulikiwa haraka iwezekanavyo".

Balozi Mwinyi alieleza kuwa kikao hicho ni fursa nzuri kwa Serikali za Tanzania na Malawi kujadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya nchi zao katika maeneo tofauti ikiwemo uchumi, uwekezaji, biashara, kutunza mazingira, elimu, Tehama, kilimo, uhamiaji, uchukuzi na masuala ya ulinzi na usalama, Hivyo alihimiza wajumbe wa pande zote mbili kuwa wabunifu katika majadiliano yao ili watoke na mipango inayotekelezeka kwa kuwa wananchi wanachohitaji ni maendeleo na sio mikakati inayoishia katika makabrasha.

Aidha, Balozi Mwinyi aliekeza kuwa watu wengi walistaajabu kusikia ujumbe wa Tanzania unakuja Malawi kushiriki kikao hiki kama walivyostaajabu kuona Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya mazungumzo hivi karibuni na Rais wa Malawi, Mhe. Prof. Peter Mutharika pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia. Alisema hakuna cha kustaajabisha hapo, isipokuwa ifahamike lengo kuu la pande zote mbili ni kuona uhusiano kati ya Tanzania na Malawi unaimarishwa na kwamba mkutano huo ni ushahidi kuwa nchi hizi mbili zipo karibu zaidi kuliko hapo awali.

Naibu Katibu Mkuu aliihakikishia Serikali ya Malawi kuwa Serikali ya Tanzania imedhamiria kushirikiana na nchi hiyo katika kuboresha mahusiano ya kidiplomasia, uchumi na kijamii, hivyo alisisitiza umuhimu wa yale yote yatakayoafikiwa katika mkutano huo yanatekelezwa katika muda uliopangwa.

Alishauri iundwe timu ya ngazi ya Makatibu Wakuu ambayo itakuwa inakutana kila baada ya miezi sita kutathmini utekelezaji wa maazimio ya kikao hicho.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Malawi, Dkt. Dalitso Kabambe alisisitiza umuhimu wa nchi hizi mbili kuweka mikakati itakayorahisisha wananchi kufanya biashara bila vikwazo. "Bisahara ni jambo muhimu lazima tuhakikishe kuwa Serikali zetu zinaweka mazingira mazuri ili wananchi wafanye biashara kwa wepesi".

Kikao hicho kinatarajiwa kufungwa rasmi na Mawaziri wa Mambo ya Nje siku ya Jumapili tarehe 05 Februari 2017 ambapo Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anatarajiwa kuwasili Malawi tarehe 04 Februari 2017. Mawaziri hao pia wataweka saini Mikataba mitatu ya ushirikiano katika mashauriano ya kisiasa na kidiplomasia, usafiri wa anga na utalii.

Wajumbe wa Tanzania katika kikao hicho wanatoka katika sekta mbalimbali wakiwemo wajumbe kutoka mikoa miwili ya Mbeya na  Ruvuma inayopakana na Malawi ambao wanaongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makalla.



Imetolewa na: Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Tarehe  03 Februari 2017


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Malawi na Mwenyekiti Mwenza wa Kikao cha JPCC kati ya Tanzania na Malawi, Dkt. Kalitso Kabambe akisoma hotuba ya iufunguzi na ukaribisho.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi akisoma houtuba ya ufunguzi wa kikao cha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPCC) kati ya Tanzania na Malawi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Malawi, Dkt. Dalitso Kabambe. Kikao hicho kinafanyika Lilongwe, Malawi kwa muda wa siku tatu kuanzia tarehe 03 Februari 2017.


Wajumbe wa Tanzania wakisikiliza hotuba za Makatibu Wakuu. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makalla, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Suleiman Salehe na Kaimu Mkurugenzi kutoka Mamlka ya Viwanja vya Ndege.


Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Ali Ubwa na mjumbe mwingine ambaye jina lake halikupatikana.


Bw. Kalitso Kabambe akiwa na Balozi wa Malawi nchini Tanzania.


Sehemu  ya ujumbe wa Malawi ukifuatilia hotuba za ufunguzi

Wajumbe wa pande zote mbili wakiwa katika kikao cha JPCC

Naibu Katibu Mkuu, Balozi Mwinyi akihojiwa na Mwandishi wa TBC, Bw. Hosea Cheo

Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Victoria Mwakasege akihojiwa na Mwandishi wa TBC

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makalla akifanya mahojiano na Mwandishi wa TBC

Friday, February 3, 2017

Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa  Kuwait nchini Mhe.Jasem Ibrahim Al Najem walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili namna ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo nchini itakayo fadhiliwa na serikali ya Kuwait ikiwemo uchimbaji visima vya maji, miradi ya kuendeleza elimu na kuboresha sekta ya afya.

Waziri Mhe. Mahiga akimsikiliza Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Najem

Waziri Mahiga na Balozi wa Kuwait nchini wakifurahia jambo

Waziri Mahiga apokea nakala za hati za utambulisho wa Balozi Mteule wa Oman

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Oman nchini Mhe.Ali A. Al Mahruqi alipowasili Wizarani kuwasilisha nakala za hati za utambulisho

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga na Balozi Mteule wa Oman nchini Tanzania Mhe. Mahruqi wakionesha nakala ya hati ya utambulisho

Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga akimsikiliza Balozi Mteule wa Oman nchini

Mazungumzo yakiendelea, Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdallah Abasi Kilima akifuatila mazungumzo

Picha ya pamoja

Waziri Mahiga apokea nakala za hati za utambulisho wa Balozi Mteule wa Iran


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Iran Nchini Tanzania Mhe.Mousa Ahmed Farhang aliwasili Wizarani kuwasilisha nakala za hati za utambulisho

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akizungumza mara baada ya kupokea nakala za hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Iran nchini Tanzania Mhe.Farhang. Kushoto ni Maafisa kutoka Ofisi za Ubalozi wa Iran nchini na Maafisa Kutoka Wizarani (kulia) wakifuatilia mazungumzo. Katika mazungumzo hayo Waziri alimkaribisha Balozi na kumhaidi kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati katika utekelezazi wa majukumu yake na kwa nchi ya Iran kwa ujumla, ili kuendeleza na kudumisha uhusiano wa Kidiplomasia uliodumu kwa muda mrefu kati ya Tanzania na Iran.


Waziri Mhe. Balozi Dk. Mahiga akizungumza na mgeni wake Mhe.Balozi Farhang

Balozi Mteule wa Iran Mhe. Farhang akizunguza mara baada ya kuwasilisha nakala za hati za utambulisho

Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga akipokea nakala za hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Iran nchini Tanzania Mhe. Farhang


Thursday, February 2, 2017

Naibu katibu Mkuu akutana na ujumbe kutoka Sweden


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Naje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wajumbe kutoka Sweden walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika kuendeleza ushirikiano wa Kiplomasia, shughuli za Kijamii na Kiuchumi baina ya nchi hizi mbili

Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza alipokutana na ujumbe kutoka Sweden, Kushoto ni Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mhe. Katarina Rangnitt
Mazungumzo yakiendelea

Mkurugenzi Mkuu wa Maendeleo ya Kimataifa kutoka Sweden Bw.Johannes Oljelund akizungumza alipokutana na Naibu Katibu Mkuu, Wa tatu kushoto Mkurugenzi Mkuu wa Biashara Bi.Karin Olofsdotter

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Balozi Joseph Sokoine (wapili kulia) akifuatilia mazungumzo, Wa kwanza kulia ni Afisa kutoka Wizarani Bi. Tunsume Mwangolombe

Watumishi wapewa semina ya maandalizi ya kuhamia Makao Makuu ya Serikali Dodoma

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga akifungua warsha ya kuwaandaa watumishi wa Wizara kuhamia Makao Makuu ya Serikali Dodoma hivi karibuni.

Mkurugenzi wa  Utawala na Usimamizi Rasmilimali watu Bw.Nigel Msangi akizungumza na watumishi (hawapo pichani) katika warsha hiyo.

Mwezeshaji wa warsha hiyo Bibi.Margaret Mussai kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto akizungumza na watumishi 

Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi, Bw. Darius Damas Kalijongo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto akitoa mada katika warsha hiyo

Mtumishi akichangia jambo wakati wa warsha

Monday, January 30, 2017

Balozi wa Indonesia nchini Tanzania aagwa baada ya kumaliza muda wake

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiani wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt.Susan Kolimba, Balozi wa Indonesia Nchini Tanzania Mhe. Zakaria Anshar (kushoto) na Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi wakijadili jambo kwenye hafla fupi ya kumuaga Balozi wa Indonesia aliyemaliza muda wake wa kuhudumu nchini

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bibi Justa Nyange (kulia) akifuatilia jambo kwenye hafla hiyo, kushoto ni Mke Balozi wa Indonesia Mhe. Anshar aliyemaliza muda wake wa kuhudumu nchini 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga akifurahia jambo wakati wa hafla hiyo, Kulia na Afisa kutoka Ubalozi wa Indonesia Bw. Nanang Eko K.P.P.

Naibu Waziri Mhe. Dkt. Susan Kolimba akimkabidhi picha ya baadhi vivutio vya kitalii vilivyopo nchini kwa Balozi wa Indonesia Mhe.Anshar na mke wake wakati hafla fupi ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kuhudumu nchini


Picha ya pamoja

Friday, January 27, 2017

India yaadhimisha miaka 68 ya Uhuru kwa kuzindua Jengo jipya la Ubalozi nchini

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa India. Maadhimisho hayo yaliyoenda sambamba na ufunguzi wa Jengo la Ubalozi mpya wa India yalifanyika kwenye Jengo hilo lililopo Mtaa wa Shaaban Robert Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Januari,
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Ausralasia, Bibi Justa Nyange wakifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa India


Sehemu ya wageni waalikwa wakiwemo Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa India
Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya nae akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa India
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa wakisikiliza hotuba ya Balozi wa India (hayupo nchini)

Balozi Baraka Luvanda, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na Naibu Balozi wa China, Bw. Gou Haudong na Bi. Sun kutoka Ubalozi wa China wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa China.
Wageni waalikwa
Wanafunzi wakiimba nyimbo za mataifa ya Tanzania na India wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa India
Kikundi cha Burudani kikitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miaka 68 ya Uhuru wa India
Makamu wa Rais, Mhe. Suluhu katika picha ya pamoja
==================================================

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

India yaadhimisha miaka 68 ya Uhuru

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan ameipongeza India kwa kuadhimisha miaka 68 ya Uhuru wa nchi hiyo. Pongezi hizo alizitoa jana wakati wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Uhuru wa nchi hiyo ambayo ilienda sanjari na ufunguzi wa jengo jipya la Ubalozi lililopo Mtaa wa Shaaban Robert Jijini Dar es Salaam.

Mama Samia Suluhu aliipongeza India kwa hatua kubwa ya maendeleo iliyopata katika nyanja mbalimbali tokea ilipopata uhuru kutoka kwa Mwingereza ambaye pia aliitawala Tanzania.

Makamu wa Rais aliitaja India kuwa sio tu ni rafiki mkubwa wa Tanzania bali ni ndugu wa karibu wanaounganishwa na bahari ya Hindi ambayo imekuwa kiunganishi kikubwa cha wafanyabiashara hata kabla ya uhuru.
Alieleza kuwa uhusiano kati ya Tanzania na India ni wa kuridhisha na umeimarika zaidi kufuatia ziara ya Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi iliyofanyika nchini mwezi Julai 2016. “Wakati wa ziara hiyo mikataba mbalimbali ilisainiwa kati ya nchi hizi mbili ambayo inalenga uedelezaji wa sekta tofauti kwa faida ya pande zote mbili”. 

Mama Samia aliendelea kueleza kuwa ushirika wa Tanzania na India ni wa kimaendeleo ambapo Tanzania imekuwa ikifaidika na misaada mbalimbali ya kimaendeleo ikiwa ni pamoja na msaada wa kuendeleza miundombimu ya maji katika mikoa ya Dar es Salaan na Pwani pamoja na Zanzibar; msaada wa kituo cha TEHAMA katika Chuo Kikuu cha Nelson Mandela mkoani Arusha na uimarishaji wa vyuo vya ufundi.

Mhe. Samia Suluhu alitumia fursa hiyo pia kuishukuru India kwa msaada iliyotoa wa zaidi ya Shilingi milioni 500 kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la Kagera lililotokea mwezi Septemba 2016. 

Kwa upande wake, Balozi wa India, Mhe. Sandeep Arya aliridhishwa na uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na India na kubainisha kuwa ziara ya Mhe. Modi mwezi Julai 2016 imeboresha na kuimarisha zaidi mahusiano hayo. Aliahidi kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali kama ilivyokuwa inafanya siku za nyuma. 

Alisema mahusiano ya kibiashara kati ya nchi hizo mbili ni makubwa na kwamba nchi yake imeisaidia Tanzania katika maeneo mengi ikiwemo mikopo ya masharti nafuu, mafunzo ya muda mfupi na mrefu, mafunzo ya ufundi, ujenzi wa vituo vya TEHAMA, na vifaa vya matibabu. 

Alizungumzia pia mahusiano ya asasi za kiraia za Tanzania na India, ushirikiano katika masuala ya utamaduni, ziara za Watanzania kwenda India kwa ajili ya matibabu na michezo ambapo aliitolea mfano wa ziara ya timu ya Taifa ya Serengeti Boys nchini India mwaka jana. 

Mhe. Balozi alihitimisha hotuba yake kwa kusifu uamuzi wa Tanzania na India kufuta viza kwa watu wenye Hati za Kusafiria za Kidiplomasia na zile za Serikali.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 27 Januari 2017.

Watanzania 14 washiriki maonesho ya Sanaa nchini Kenya

Maonesho ya sanaa za uchoraji ya Wasanii 14 kutoka Tanzania yameanza rasmi tarehe 25 Januari 2017 kwenye ukumbi wa maonesho wa Village Market Nairobi.
Watu waliotembelea maonesho hayo siku ya kwanza ni pamoja na Mabalozi na wadau mbalimbali wa sanaa kutoka Kenya na nchi za nje. Maonesho hayo yatachukua wiki mbili.
Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Bi. Talha Mohamed Waziri (kulia) akimkaribisha Balozi wa Msumbiji kwenye maonesho hayo.

Ofisa wa Ubalozi wa Venezuela Nairobi, Jose Gregorio Ayila Torres (katikati) akibadilishana mawazo na Kaimu Balozi wa Tanzania (kulia). Kushoto ni mmoja wa wasanii wa Tanzania, Raza Mohamed.
Raia wa Uswisi waliofika kwenye maonesho.

Wapenda sanaa wa Kenya wakikagua kazi za wasanii wa Tanzania

Wadau wa sanaa wakifurahia maonesho