Thursday, March 30, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje apokea Nakala za Utambulisho za Mabalozi Wateule kutoka Ethiopia na Vietnam nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Vietnam nchini,  Mhe. Nguyen Kim Doanh. Tukio hilo limefanyika Wizarani tarehe 30 Machi, 2017.
Dkt. Kolimba akizungumza na Balozi Mteule wa Vietnam, Mhe. Nguyen Kim Doanh mara baada ya  kupokea nakala zake za hati za utambulisho
Balozi Mteule Mhe. Nguyen Kim Doanh naye akizungumza.
Dkt. Kolimba na Balozi Mteule Mhe. Nguyen Kim Doanh wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Magabilo Murobi na Afisa kutoka Ubalozi wa Vietnam nchini
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini, Mhe. Dina Mufti Sid.Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 30 Machi, 2017.
Dkt. Kolimba akizungumza na Balozi Mteule wa Ethiopia nchini, Mhe. Dina Mufti Sid.
Picha ya pamoja.

SADC yahamasisha raia wa nchi wanachama kujisajili katika masuala ya ulinzi wa amani Barani Afrika

Mratibu wa Mafunzo kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Bi. Eliet Magogo akiwasilisha mada katika warsha ya kuhamasisha raia kujiunga katika jeshi la ulinzi wa amani la jumuiya hiyo iliyofanyika leo katika Hotel ya Serena Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Watumishi kutoka katika Wizara, Idara na Taasisi za Serikali. Katikati ni Mkuu wa Kitengo kinachoshughulikia raia katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Bw. Ernest Kantchentche na kushoto ni Bi. Caroline Chipeta, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Sehemu ya Maafisa waliohudhuria warsha hiyo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kutoka kulia ni Bi. Felista Rugambwa, Bw. Deogratius Dotto na Bw. Abdallah Mrisho.
Sehemu nyingine ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa.
Warsha ikiendelea
Picha ya pamoja.

Friday, March 24, 2017

Balozi Kairuki awasilisha Hati za Utambulisho

Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mberwa Kairuki akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping wakati wa hafla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho iliyofanyika  Ikulu kwenye Ukumbi wa Great hall of the people siku ya Ijumaa tarehe 17 Machi 2017.
Balozi Kairuki (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa China, Mhe. Xi Jinping
Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Mbelwa Kairuki amewasilisha rasmi Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping tarehe 17 Machi 2017. 

Hafla hiyo iliyofanyika katika Ikulu ya China (Great Hall of the People) ilihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi na maafisa waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China. 

Katika mazungumzo mafupi baada ya kuwasilisha hati, China na Tanzania zimekubaliana kukuza zaidi mahusiano ya kiuchumi kupitia mpango maalum wa China wa kuhamishia viwanda vyake nje ya China (Production Capacity Cooperation Programme) pamoja na programu ya kukuza ushirikiano wa biashara na ujenzi wa miundombinu ijulikanayo kama Maritime Silk Road initiative. 

Aidha, Tanzania imeihakikishia China kuendelea kuunga mkono sera yake ya ONE CHINA POLICY sambamba na kuunga mkono mtazamo wa China kuhusu mgogoro wa Bahari ya Kusini mwa China.

Thursday, March 23, 2017

Katibu Mkuu Mambo ya Nje apokea vifaa vya kuendesha mikutano kwa njia ya Video


Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (Kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuendeshea Mikutano kwa njia ya Video Wizarani Jijini Dar es Salaam tarehe 23 Machi, 2017. Makabidhiano yanakamilisha sehemu ya vifaa vilivyotolewa na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bi. Awa Dabo ambavyo vilikabidhiwa tarehe 2 Februari, 2017 ili kuiwezesha Wizara kufanya kazi kwa ufanisi zaidi sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji wa ofisi.
Katibu Mkuu akimpongeza Balozi Mushy kwa jitihada zake za kuimarisha mahusiano mazuri na wadau wa maendeleo sambamba na kuhakikisha shughuli za kiutendaji za Wizara zinaenda na kasi ya maendeleo ya teknolojia.
Katibu Mkuu na Balozi Mushy wakipokea maelezo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eric Kombe kuhusu namna vifaa hivyo vinavyoweza kurahisisha Mawasiliano.

Mhe. Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Hungary nchini, Mhe. Laszlo Eduard Mathe mwenye makazi yake Nairobi, Kenya. Hafla hiyo fupi imefanyika tarehe 23 Machi, 2017, Ikulu, Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Mathe akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Aziz Mlima huku Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (wa kwanza kulia), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mary Matari wakishuhudia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Guinea nchini, Mhe. Sidibe Fatoumata KABA mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. Hafla hiyo fupi imefanyika tarehe 23 Machi, 2017, Ikulu, Dar es Salaam.
Mhe. Sidibe Fatoumata KABA (katikati) akiwa ameongozana na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin (kushoto) na Mnikulu, Bw. Ngusa Samike.
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha Balozi Kaba kwa Waziri Mahiga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Belarus nchini, Mhe. Dmitry Kuptel mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. Hafla hiyo fupi imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 23 Machi, 2017.
Mhe. Dmitry Kuptel akisikiliza wimbo wa taifa lake kutoka Bendi ya Polisi kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais Magufuli
Mhe. Dmitry Kuptel akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Botswana nchini, Mhe. Lebonaamang Thanda Mokalake mwenye makazi yake Lusaka, Zambia. Hafla hiyo fupi imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 23 Machi, 2017
Balozi Mokalake akisikiliza wimbo wa taifa lake kutoka Bendi ya Polisi kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin na kushoto ni Mnikulu, Bw. Ngusa Samike
Mhe. Rais Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi Mokalake, Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu na Maafisa kutoka Ubalozi wa Botswana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho  kutoka kwa Balozi Mteule wa Niger nchini, Mhe. Adam Maiga ZAKAKARIAOU mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia.
Balozi ZAKAKARIAOU akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho  kutoka kwa Balozi  wa Mauritius nchini, Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake Maputo, Msumbiji.
Bendi ya Polisi ikipiga wimbo wa taifa wa Mauritius kwa heshima ya Mhe. Balozi Jean Pierre Jhumun.

Wednesday, March 22, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Wateule

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Mauritius nchini, Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake Maputo, Msumbiji.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Nepal nchini, Mhe. Amrit Rai mwenye makazi yake Pretoria, Afrika Kusini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ecuador nchini, Mhe. Benys Toscano Amores mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Congo Brazaville nchini, Mhe. Guy Nestor Itoua mwenye makazi yake Kigali, Rwanda.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa New Zealand nchini, Mhe. Michael Gerrard Burrel mwenye makazi yake Pretoria, Afrika Kusini.

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi Mteule wa Oman nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (kulia) akizungumza na Balozi Mteule wa Oman nchini, Mhe. Ali Abdullah Mahruqi alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika suala la Makao Makuu ya Serikali kuhamia Dodoma na namna Ofisi za Ubalozi huo zinavyoweza kutumia fursa hiyo kuwashauri wafanyabiashara wa Oman kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu pamoja na huduma nyingine za biashara ambazo bado hazijawa za uhakika katika mji huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi (kushoto) akiwa na Bi. Patricia Kiswaga, Afisa Mambo ya Nje.
Mazungumzo yakiendelea.
Balozi Mlima akiagana na Balozi Al Mahruqi

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Wateule nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) leo tarehe 22 Machi, 2017 amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Mabalozi Wateule 7 wanaowakilisha nchi zao nchini kutoka Hungary, Belarus, Guinea, Botswana, Niger, Cyprus na Bangladesh. Pichani Balozi Mahiga akipokea nakala za hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Hungary nchini, Mhe. Laszlo Eduard Mathe mwenye makazi yake Nairobi, Kenya.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akipokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Belarus nchini, Mhe. Dmitry Kuptel mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa na Balozi Mteule wa Guinea nchini Mhe. Sidibe Fatoumata KABA mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia mara baada ya kupokea Nakala zake za Hati za Utambulisho.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Botswana nchini, Mhe. Lebonaamang Thanda Mokalake mwenye makazi yake Lusaka, Zambia.
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Mokalake mara baada ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin.
Mazungumzo yakiendelea kushoto ni Maafisa wa Ubalozi wa Botswana ambao waliambatana na Mhe. Mokalake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Niger nchini, Mhe. Adam Maiga ZAKAKARIAOU mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. 
Waziri Mahiga akiagana na Mhe. ZAKAKARIAOU mara baada ya kuwasilisha Nakala za Utambulisho.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Cyprus nchini, Mhe. Andreas Panayiotou mwenye makazi yake Muscat, Oman.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Bangladesh nchini, Mhe. Meja Jenerali Abul Kalam Mohammad ahaumayun KABIR mwenye makazi yake Nairobi, Kenya. 
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. KABIR.Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin na kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Bangladesh ambaye aliambatana na Mhe. KABIR.