Friday, May 26, 2023

SERIKALI YA TANZANIA YAPEWA TUZO NA DRC

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kupitia kwa Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani na Usalama, Mhe  Peter Kazadi ameikabidhi Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tuzo ya Heshima (Gardons notre amitié) - inayohusu KUDUMISHA UHUSIANO baina ya Nchi hizo mbili .Tuzo hiyo imepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini DRC, Mhe. Said J Mshana wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Umoja wa Afrika iliyoandaliwa kwa ajili ya Mawaziri wa SADC waliohudhuria Mkutano kuhusu Udhibiti wa Maafa.

Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe Said J Mshana akiongea jambo baada ya kukabidhiwa Tuzo na Serikali ya DRC

Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe Said J Mshana alimwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Bunge na Uratibu katika kikao cha Mawaziri wa SADC kilichohusu udhibiti wa maafa kilichofanyika jijini Kinshasa.
Hadi kufikia tarehe 25 Mei 2023, Nchi Wanachama sita kati ya kumi na sita zilikuwa zimesaini Mkataba wa Uendeshaji wa Kituo cha Operesheni na Huduma za Kibinadamu cha SADC.
Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe Said J Mshana katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mkutano wa Mawaziri wa SADC uliohusu udhibiti wa maafa uliofanyika jijini Kinshasa






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.