Tuesday, May 9, 2023

NAIBU WAZIRI MKUU WA KWANZA WA UGANDA AWASILI NCHINI KIKAZI

Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Rebecca Kadaga amewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere. Mhe. Kadaga anatarajia kuwa na mkutano wa majadiliano baina yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) tarehe 10 May, 2023, katika Ofisi Ndogo ya Wizara, Jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kuwasili nchini, Mhe. Kadaga alipokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz pamoja Balozi wa Uganda nchini, Mhe. Kanali Mstaafu Fred Mwesigye.

Pamoja na mambo mengine, mazungumzo ya viongozi hao yatahusu kuimarisha ushirikino kati ya Tanzania na Uganda, pamoja na ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Rebecca Kadaga amewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Rebecca Kadaga amewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Rebecca Kadaga akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz (katikati) pamoja Balozi wa Uganda nchini, Mhe. Kanali Mstaafu Fred Mwesigye (kulia) baada ya kuwasili amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.