Monday, May 1, 2023

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI YASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI 2023


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouku (Mb.) wakijadili jambo muda mfupi baada ya kuhitimishwa ka Sherehe za Maadhimisho ya Mei Mosi 3023

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki terehe 1 Mei 2023 imeungana na maelfu ya Wafanyakazi nchini kusheherekea Maadhimisho ya Mei Mosi 2023 yaliyofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. 

Katika maadhimisho hayo ambayo mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyoongozwa na kauli mbiu isemayo “Mishahara Bora na Ajira za Staha ni Nguzo kwa Maendeleo ya Wafanyakazi”, mbali na Mheshimiwa Rais Samia kuzungumza na Wafanyakazi, sherehe za maadhimisho hayo ziliambatana na shughuli mbalimbali kama vile maandamano ya Wafanyakazi, burudani, na maandamano ya magari yaliyokuwa yakionesha huduma zinazotolewa na Taasisi mbalimbali. 

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika sherehe hizo iliwakilishwa na Waziri Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.), Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.), Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu Bi. Chiku Kiguhe na Wafanyakazi wengine wa Wizara.

Wakati huo huo Viongozi na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wametoa pongezi wa Bi. Mary Peter kwa kuwa mfanyakazi Hodari wa Wizara kwa mwaka 2023. Pongezi hizo kwa Bi. Mary Peter zimeambatana na zawadi ya kiasi cha shilingi milioni 5.

Mheshimiwa Rais Samia mbali na kuahidi kuendelea kutatua changamoto mbalimbali zilizo wasilishwa na Vyama vya Wafanyakazi na kuboresha maslahi ya Wafanyakazi, aliwahimiza Wafanyakazi wote nchini kuendelea kufanya kazi kwa kujituma zaidi kwa kuzingatia weledi, uaminifu na ubunifu ili kuendelea kuleta tija zaidi kwa Taifa. 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa na bango la Wizara kwenye Sherehe ya Maadhimisho ya Mei Mosi iliyofanyika Kitaifa mjini Morogoro.

Bw. Shaaban Maganga mfanyakazi wa Wizara akipokea cheti za ushiriki wa michezo ya Mei Mosi 2023


Sehemu ya wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye Sherehe ya Maadhimisho ya Mei Mosi iliyofanyika Kitaifa mjini Morogoro.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.