Thursday, July 7, 2022

DIPLOMASIA KUENDELEA KUWA CHACHU YA KUKUZA NA KUBIDHAISHA KISWAHILI DUNIANI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ametoa rai kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuweka jitihada za makusudi za kukikuza Kiswahili nje ya mipaka ya Tanzania.

Rai hiyo imetolewa wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa Leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Mhe. Mpango akiwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo ameeleza kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeendelea kubeba jukumu la kizalendo ambapo, kupitia Balozi zake ilifanikiwa kushawishi majukwaa ya kimataifa kuitambua lugha ya Kiswahili na kupewa siku ya kuadhimishwa duniani ambayo inafanyika leo kwa mara ya kwanza.

“Ninatoa pongezi kwa Balozi zetu kwa jitihada wanazofanya za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili, nimeona mitandaoni jinsi Balozi zilivyojitoa kufanya makongamano na midahalo ya Kiswahili katika kusherehesha siku hii” alisema Mhe. Mpango.

Pamoja na kutolewa kwa pongezi kwa Wizara, Mhe. Mpango ametoa pongezi za kipekee kwa Mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha Jijini New York, Marekani, Mhe. Kennedy Gaston; Addis Ababa, Ethiopia, Mhe. Innocent Shio na Paris, Ufaransa, Mhe. Samuel Shelukindo kwa kukamilisha mchakato wa kutambulika kwa Kiswahili duniani.

Aidha, uwepo wa siku maalum ya kuadhimishwa lugha ya Kiswahili duniani kukupa nguvu ikiwa ni lugha rasmi ya kazi katika Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na kufanya jumuiya nyingine ambazo Tanzania ni mwanachana kuipa upekee lugha ya Kiswahili.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mwakilishi wa kudumu katika Umoja wa Afrika, Mhe. Balozi Innocent Shio ameeleza kuwa lugha ya Kiswahili ina nafasi kubwa katika kukuza na kuimarisha mtangamano kwa maendeleo ya Afrika kwakuwa, mawasiliano huleta amani na kuongeza mshikamano.

Pia, akaeleza wakati huu ambapo Umoja wa Afrika unaenda kutathmini Agenda 2030 na kutekeleza kikamilifu Agenda 2063 ya Umoja huo ni wakati sasa wa kukibidhaisha kiswahili ili kuunganisha mataifa ya Afrika na kuweza kuyafikia malengo ya mpango wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCTA) katika kukuza sekta za kiuchumi na kuinua pato la Wananchi na Taifa kwa ujumla.

“Lugha ni bidhaa hivyo ni muhimu kusimamia kikamilifu soko lake ili kuleta fursa zinazotarajiwa, mathalan ajira kwa Walimu, Wakarimali, huduma ya kutafsiri, utangazaji, uandishi wa vitabu vya Kiswahili, Sanaa ya uigizaji na uhariri” alisema Balozi Shio.

Tarehe 23 Novemba 2021, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) lilitangaza Siku Maalumu ya Kiswahili Duniani inayoadhimishwa tarehe 7 Julai kila mwaka.

Sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani, zimeandaliwa na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuhudhuriwa na Viongozi wa Wizara, Taasisi, Idara, sekta binafsi na taasisi ya za elimu nchini na Wananchi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Matsie Angelina Motshekga akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika tarehe 7 Julai 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mhe. Motshekga ameeleza kuwa Serikali ya Afrika Kusini ipo tayari kuingiza somo la lugha ya kiswahili katika shule za msingi na hivyo itaendelea kuhitaji usaidizi wa vitabu na maboresho ya mitaala kwa ajili ya kufundishia.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Afrika, Mhe. Innocent Shio akihutubia kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Fatma Rajab (aliyeshika bendera) akifuatilia sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Kushoto ni aliyekuwa Balozi wa Tanzania na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, Balozi Modest Mero na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bi Ellen Maduhu wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Kushoto Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda na Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Matsie Angelina Motshekga wakitia saini makubaliano ya kuanza kufundisha kiswahili katika elimu ya msingi nchini Afrika Kusini.

Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango akimshukuru Naibu Waziri wa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mabarouk Nassor Mbarouk baada ya kumlizika kwa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Afrika, Mhe. Innocent Shio akipokea tuzo ya ngao kutoka kwa Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Mphamed Mchengerwa kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Hafla ikiendelea.


Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa na wa Afrika Mashariki ukipigwa kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Waziri Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.

Picha ya pamoja meza kuuna viongozi Wakuu wa Wizara, Taasisi na Idara za Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) 

 

DKT. MWINYI AZISIHI NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUBUNI MBINU ZA KUENEZA KISWAHILI

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kubuni mbinu bora za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili katika ukanda huo na duniani kwa ujumla.

Dkt. Mwinyi ametoa wito huo wakati akifunga Kongamano la Kiswahili Duniani lililoanza jana na kuhitimishwa leo Zanzibar ambapo amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa zinashirikiana na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoa mafunzo ya Isimu na Fasishi katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa mikakati madhubuti ya kuendeleza lugha ya Kiswahili Duniani.

“Natoa wito pia kwa taasisi za elimu ya juu kushirikiana na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia lugha ya Kiswahili kama fursa kwa vijana wetu kwani lugha hii ni kama bidhaa,” amesema Dkt. Mwinyi.

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Mwinyi ameihakikishia Kamisheni ya Kiswahili na Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa zitaendelea kuunga mkono jitihada za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili duniani kote.

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote amesema Jumuiya ya Afrika Mashariki itaendelea kushirikiana na wadau wa Lugha ya Kiswahili ili kuweza kuanzisha mabaraza ya Kiswahili ikiwa ni njia moja wapo mahsusi ya kukuza na kuendeleza lugha hiyo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amesema kuwa ni lugha ya Kiswahili ni lugha ya kwanza kutumika katika shughuli rasmi za Umoja wa Afrika, pia ni lugha ya kwanza Afrika na ya nane duniani kuwa na siku maalum ya kuadhimishwa

“Kutumia lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  kutasaidia kuongeza umoja baina ya wananchi wa ukanda huo kuliko ilivyokuwa awali na kuongeza maelewano na baina ya nchi na nchi” amesema balozi Sokoine

Balozi Sokoine ameongeza kuwa, lugha ya Kiswahili ikitumika vizuri itasaidia kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika masuala mbalimbali yakiwemo masuala ya kisiasa, biashara, uchumi, elimu utamaduni na ustawi wa jamii.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Sokoine amezisisi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Masahriki kuongeza kasi ya kutangaza na kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki” 

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar (BAKIZA), Dkt. Mwanahija Ali Juma amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha kuwa wanakuza na kuendeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa kuanzisha mabaraza ya Kiswahili

Dkt. Mwanahija ameongeza kuwa njia nyingine ya kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili ni pamoja na nchi wanachama kuungana pamoja na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufanya tafiti za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili.

Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani limehudhuriwa na nchi wanachama sita kutoka ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jamhuri ya Kenya, Jamhuri ya Rwanda, Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Rwanda na Jamhuri ya Sudani kusini.

Novemba 23, 2021 Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) lilitangazwa rasmi kuwa tarehe 7 Julai ya kila mwaka ni siku maalumu ya kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani. Vilevile, Februari 2022, Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika katika Mkutano wake wa kawaida wa 35 walipitisha Kiswahili kama Lugha ya Kazi na mawasiliano mapana Barani Afrika.

Aidha, Mwezi Septemba, 2022 Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa  ulianza kuitangaza na kuisamba lugha ya Kiswahili, nchini Ufaransa kwa kushirikiana na Chama cha Watanzania Ufaransa (CCWU), ambapo ulianza kutoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa mwaka wa masomo 2021/22, ambayo yaliendeshwa na Kituo cha Utamaduni na Lugha cha Kitanzania (CCLT).

Washiriki wa matembezi kutoka ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakionesha baadhi ya Bendera za nchi wananchama wa Jumuiya hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika leo Zanzibar




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akipokelewa na viongozi mbalimbali alipowalisi kuhitimisha Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar

   
Washiriki wa Kongamano la Kiswahili Duniani wakifuatilia Hotuba ya Rais wa Zanzibaar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa kufunga kongamano hilo leo Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwasilisha Hotuba yake wakati wa kuhitimisha Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote akitoa hotuba yake katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililohitimishwa leo Zanzibar



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar




SERIKALI YA TANZANIA NA ETHIOPIA ZAKUTANA KWA KIKAO CHA PAMOJA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni wamefanya kikao cha pamoja na Balozi wa  Ethiopia nchini, Mhe. Shibru Kedida tarehe 06 Julai 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine kikao hicho kimejadili juu ya kuimarisha ushirikiano imara na wa kihistoria baina ya Tanzania na Ethiopia pamoja na changamoto za uhamiaji haramu nchini.

Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni akifafanua jambo wakati wa kikao hicho.

Kulia ni Kamishna wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka wa Idara ya Uhamiaji, Samwel Mahirane akifafanua jambo juu ya masuala ya  usimamizi wa mipaka wakati wa majadiliano ya kikao hicho, pembeni yake ni Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza nchini, ACP George Wambura.

Aliyesimama ni Naibu Kamishna Msaidizi wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka wa Idara ya Uhamiaji,Phabian Philo akifafanua jambo katika majadiliano ya kikao hicho.

Majadiliano yakiendelea.

Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara hiyo wakaijadiliana jambo na Kamishna Mahirane na Kamishna Philo wa Idara ya Uhamiaji baada ya kumalizika kwa mazungumzo. 

Picha ya Pamoja Waheshimiwa Mawaziri, Mhe. Balozi na Ujumbe walioambatana nao katika kikao hicho.

Waziri Mulamula akiagana na Mhe. Balozi Shibru Kedida baada ya mazungumzo.

 

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA TWAWEZA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokea jarida kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza nchini, Bw. Aidan Eyakuze alipomtembelea tarehe 6 Julai 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Waziri Mulamula akizungumza na Bw. Eyakuza ambapo pamoja na mambo mengine, Bw. Eyakuze alienda kujitambulisha kwa Mhe. Waziri pamoja na kueleza majukumu yanayotekelezwa na Taasisi ya TWAWEZA nchini.

Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula, Bw. Eyakuze pamoja na ujumbe ulioambatana nao katika mazungumzo hayo. 

 

Wednesday, July 6, 2022

TANZANIA NA ALGERIA KUFUNGUA MAENEO MAPYA YA USHIRIKIANO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akipokea barua kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje ya Algeria iliyowasilishwa na Balozi wa Algeria nchini, Mhe.Ahmed DJELAL leo tarehe 6 Julai 2022 jijini Dar es Salaam.

Mhe. Balozi Ahmed DJELAL akifafanua jambo kwa Mhe. Waziri Mulamula.
Mhe. Waziri  Mulamula akizungumza na Mhe. Balozi Ahmed DJELAL, katika mazungumzo yao viongozi hao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali zao hususan katika sekta za afya, nishati, elimu,miundombinu, usimamizi wa majanga, zimamoto na uokoaji.
Pia wamekubaliana kuanzishwa kwa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria ili maeneo hayo ya ushirikiano yasimamiwe kwa tija ya mataifa yao.

Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini, Algeria, Mhe. Maj. Gen. Jacob Kingu akitoa ufafanuzi wakati wa mazungumzo hayo, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga .

Mhe. Waziri Mulamula akiagana na Balozi Ahmed DJELAL baada ya mazungumzo.

 

VACANCY ANNOUNCEMENT


 

BALOZI MULAMULA: SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA WEZESHI KWA SEKTA BINAFSI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Wawakilishi wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) katika ofisi ndogo za Wizara leo tarehe 6 Julai 2022 jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo Waziri Mulamula amewahakikishia Wawakilishi hao kuwa Serikali inaendelea kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi ili kukuza sekta za uzalishaji kwa maslahi mapana ya Taifa.

‘’ Wizara kupitia Balozi zetu nje imeendelea kuhakikisha fursa mbalimbali zinazopatikana nchini zinatangazwa katika maeneo ya uwakilishi ili kuzihakikishia sekta hizo mageuzi makubwa ya  kiuchumi” alisema Balozi Mulamula.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TPSF, Bi. Angelina Ngalula pamoja na wajumbe alioambatana nao wameipongeza na kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweka mkazo wa kuinua sekta binafsi.

Akifafanua Bi. Ngalula ameeleza juu ya uwepo wa mafanikio katika sekta za biashara, Utalii, uwekezaji, kilimo, madini, huduma, uchukuzi na usafirishaji na ujenzi.

“Sisi sekta binafsi tunaishukuru Serikali yetu kwa kuboresha mazingira ya biashara, sasa tunashuhudia mipaka inafunguka sambamba na ongezeko la watalii kupitia jitihada za makusudi zinazofanyika katika kuitangaza filamu ya “Tanzania the Royal Tour” alisema Bi. Ngalula

Aidha, akafafanua matokeo yaliyopatikana kupitia ziara za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwamba kupitia ziara hizo mikutano na makongamano ya biashara yalifanyika katika nchi mbalimbali na yamesaidia kupatikana kwa washirika wa kibiashara kutoka mataifa hayo.

Kupitia mazungumzo hayo Waziri Mulamula na Wawakilishi wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi, wamekubaliana kuanzisha timu maalum ya uratibu na ufuatiliaji wa masuala mbalimbali ya kimkakati kitaifa, kwa lengo la kuimarisha na kukuza diplomasia ya uchumi nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (kati) akizungumza na Wawakilishi wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) leo tarehe 6 Julai 2022 katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya TPSF, Bi. Angelina Ngalula.


Waziri Mulamula akizungumza na Wawakilishi wa Bodi ya TPSF kutoka katika Sekta za Huduma, Sekta Umma, Sekta ya Wenye Viwanda Vidogo,Sekta ya Wafanyabiashara Wanawake, Sekta ya Uhandisi na Ujenzi, na ulioambatana, Uongozi wa TPSF uliokuwa umeambatana na Bi. Ngalula.

Kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga akifafanua jambo katika mazungumzo hayo.


Balozi Mulamula akimkabidhi  Mwenyekiti wa Bodi ya TPSF, Bi. Ngalula vitabu vya Diplomasia ya Uchumi.

Picha ya Pamoja.



VACANCY ANNOUNCEMENT


 

VACANCY ANNOUNCEMENT









 

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI ZATAKIWA KUKUZA, KUENZI KISWAHILI

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

Nchi za Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimetakiwa kuweka mikakati ya muda mrefu ili kukuza, kuendeleza na kueneza lugha ya Kiswahili duniani.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Bw. Khamis Abdalla Saidi aliyemwakilisha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mhe.Tabia Maulid Mwita katika Kongamano la kwanza la Siku ya Kiswahili Duniani lililoanza leo tarehe 6 Julai, 2022 Zanzibar. 

Kongamano hilo linalongozwa na Kauli Mbiu: “Kiswahili kwa Amani, Ustawi na Utangamano wa Kikanda” litahitimishwa kwenye siku ya Kilele cha Siku ya Kiswahili duniani tarehe 7 Julai 2022.

Katika hotuba yake, Bw. Saidi amesema kuenea kwa Kiswahili katika ukanda wa Afrika Mashariki na Mataifa mengine ni bidhaa ya bishara, hivyo umuhimu wa Kiswahili ni mkubwa katika kupiga hatua ya kimaendeleo. 

“Ni jukumu la kila mmoja wetu kukifuatilia Kiswahili katika kila hatua na kutafuta na kubuni njia na mikakati ya muda mrefu na ya kisasa ya kuikuza lugha hii adhimu ya Kiswahili,” amesema Bw. Saidi.

Bw. Saidi aliongeza Lugha ya Kiswahili inatakiwa itumike kama bidhaa inayouzwa na kupata tija. Kuna haja kubwa ya kuwekeza kuwasomesha wataalamu wa lugha kuwa na stadi na uwezo unaotakiwa katika kutoa huduma ya kufundisha, ukalimani, kutafrisi na kuandaa machapisho mbali mbali kwa Kiswahili.

“Ni jukumu la vyuo vikuu vya Afrika Mashariki kutilia mkazo mikakati ya muda mrefu ya uwekezaji wa kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili kwa kufanya tafiti mbalimbali za lugha,” ameongeza Bw. Saidi. 

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote amesema kuwa jumuiya ya Afrika Mashariki inapaswa kushirikiana kwa pamoja na wadau wa Lugha ya Kiswahili ili kuweza kupata uzoefu wa matumizi ya Kiswahili pamoja na kujadili changamoto za lugha hiyo ili kuimarisha utangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Matumizi sahihi ya lugha ya Kiswahili yataimarisha utangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuwa lugha hii ni lugha ya biashara hivyo tunapaswa kujivunia lugha hii adhimu kwa maslahi mapana ya jumuiya yetu,” amesema Mhandisi Mlote.

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa (MS TCDC), Bi. Yusta Mganga amesema licha ya kuimarika kwa matumizi ya Lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ukanda huo unapaswa kuchukua hatua madhubuti zaidi kwa ajili ya kuhakikisha lugha ya Kiswahili inakuzwa na kuendelezwa miongoni mwa nchi ambazo bado hazijaimarika katika matumizi ya Kiswahili. 

“Kuna njia mbalimbali za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili kama vile kufanya tafiti, uandaaji wa makongamano na semina mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya Kiswahili…….katika kuandhimisha siku hii muhimu ni vyema tukatafakari mafanikio ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya yetu ili kuimarisha amani na utangamano wa kikanda,” amesema Bb. Mganga

Novemba 23, 2021 Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) lilitangazwa rasmi kuwa tarehe 7 Julai ya kila mwaka ni siku maalumu ya kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani. 

Februari 2022, Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika katika mkutano wake wa kawaida wa 35 walipitisha Kiswahili kama Lugha ya Kazi na mawasiliano mapana Barani Afrika.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar, Bw. Khamis Abdalla Saidi akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani linalofanyika Zanzibar kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote akitoa hotuba yake katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar

Kaimu Katibu Mtendaji Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. James Jowi akizungumza na washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar 

Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar (BAKIZA), Dkt. Mwanahija Ali Juma akielezea mchango wa BAKIZA katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar 

Meza Kuu wakifuatilia kikundi cha ngoma za asili kutoka Zanzibar wakati wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar 

Washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani wakifuatilia kikundi cha ngoma za asili kutoka Zanzibar  

Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akitoa mchango wake katika Kongamano la Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar

Washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani wakiimba wimbo wa Taifa  

Washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani wakifuatilia Kongamano hilo lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar 

Meza Kuu katika picha ya pamoja na wawakilishi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar