Hafla ikiendelea. |
Picha ya pamoja meza kuuna viongozi Wakuu wa Wizara, Taasisi na Idara za Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) |
Hafla ikiendelea. |
Picha ya pamoja meza kuuna viongozi Wakuu wa Wizara, Taasisi na Idara za Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) |
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kubuni mbinu bora za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili katika ukanda huo na duniani kwa ujumla.
Dkt. Mwinyi ametoa wito huo wakati akifunga Kongamano la Kiswahili Duniani lililoanza jana na kuhitimishwa leo Zanzibar ambapo amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa zinashirikiana na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoa mafunzo ya Isimu na Fasishi katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa mikakati madhubuti ya kuendeleza lugha ya Kiswahili Duniani.
“Natoa wito pia kwa taasisi za elimu ya juu kushirikiana na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia lugha ya Kiswahili kama fursa kwa vijana wetu kwani lugha hii ni kama bidhaa,” amesema Dkt. Mwinyi.
Pamoja na mambo mengine, Dkt. Mwinyi ameihakikishia Kamisheni ya Kiswahili na Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa zitaendelea kuunga mkono jitihada za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili duniani kote.
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote amesema Jumuiya ya Afrika Mashariki itaendelea kushirikiana na wadau wa Lugha ya Kiswahili ili kuweza kuanzisha mabaraza ya Kiswahili ikiwa ni njia moja wapo mahsusi ya kukuza na kuendeleza lugha hiyo.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amesema kuwa ni lugha ya Kiswahili ni lugha ya kwanza kutumika katika shughuli rasmi za Umoja wa Afrika, pia ni lugha ya kwanza Afrika na ya nane duniani kuwa na siku maalum ya kuadhimishwa
“Kutumia lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutasaidia kuongeza umoja baina ya wananchi wa ukanda huo kuliko ilivyokuwa awali na kuongeza maelewano na baina ya nchi na nchi” amesema balozi Sokoine
Balozi Sokoine ameongeza kuwa, lugha ya Kiswahili ikitumika vizuri itasaidia kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika masuala mbalimbali yakiwemo masuala ya kisiasa, biashara, uchumi, elimu utamaduni na ustawi wa jamii.
Pamoja na mambo mengine, Balozi Sokoine amezisisi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Masahriki kuongeza kasi ya kutangaza na kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki”
Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar (BAKIZA), Dkt. Mwanahija Ali Juma amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha kuwa wanakuza na kuendeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa kuanzisha mabaraza ya Kiswahili
Dkt. Mwanahija ameongeza kuwa njia nyingine ya kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili ni pamoja na nchi wanachama kuungana pamoja na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufanya tafiti za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili.
Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani limehudhuriwa na nchi wanachama sita kutoka ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jamhuri ya Kenya, Jamhuri ya Rwanda, Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Rwanda na Jamhuri ya Sudani kusini.
Novemba 23, 2021 Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) lilitangazwa rasmi kuwa tarehe 7 Julai ya kila mwaka ni siku maalumu ya kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani. Vilevile, Februari 2022, Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika katika Mkutano wake wa kawaida wa 35 walipitisha Kiswahili kama Lugha ya Kazi na mawasiliano mapana Barani Afrika.
Aidha, Mwezi Septemba, 2022 Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa ulianza kuitangaza na kuisamba lugha ya Kiswahili, nchini Ufaransa kwa kushirikiana na Chama cha Watanzania Ufaransa (CCWU), ambapo ulianza kutoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa mwaka wa masomo 2021/22, ambayo yaliendeshwa na Kituo cha Utamaduni na Lugha cha Kitanzania (CCLT).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akipokelewa na viongozi mbalimbali alipowalisi kuhitimisha Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar |
Washiriki wa Kongamano la Kiswahili Duniani wakifuatilia Hotuba ya Rais wa Zanzibaar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa kufunga kongamano hilo leo Zanzibar |
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwasilisha Hotuba yake wakati wa kuhitimisha Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar |
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote akitoa hotuba yake katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililohitimishwa leo Zanzibar |
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar |
Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni akifafanua jambo wakati wa kikao hicho. |
Aliyesimama ni Naibu Kamishna Msaidizi wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka wa Idara ya Uhamiaji,Phabian Philo akifafanua jambo katika majadiliano ya kikao hicho. |
Majadiliano yakiendelea. |
Picha ya Pamoja Waheshimiwa Mawaziri, Mhe. Balozi na Ujumbe walioambatana nao katika kikao hicho. |
Waziri Mulamula akiagana na Mhe. Balozi Shibru Kedida baada ya mazungumzo. |
Waziri Mulamula akizungumza na Bw. Eyakuza ambapo pamoja na mambo mengine, Bw. Eyakuze alienda kujitambulisha kwa Mhe. Waziri pamoja na kueleza majukumu yanayotekelezwa na Taasisi ya TWAWEZA nchini. |
Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula, Bw. Eyakuze pamoja na ujumbe ulioambatana nao katika mazungumzo hayo. |
Mhe. Balozi Ahmed DJELAL akifafanua jambo kwa Mhe. Waziri Mulamula. |
Mhe. Waziri Mulamula akiagana na Balozi Ahmed DJELAL baada ya mazungumzo. |
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amefanya
mazungumzo na Wawakilishi wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF)
katika ofisi ndogo za Wizara leo tarehe 6 Julai 2022 jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo hayo Waziri
Mulamula amewahakikishia Wawakilishi hao kuwa Serikali inaendelea kuimarisha
ushirikiano na sekta binafsi ili kukuza sekta za uzalishaji kwa maslahi mapana
ya Taifa.
‘’ Wizara kupitia Balozi zetu
nje imeendelea kuhakikisha fursa mbalimbali zinazopatikana nchini zinatangazwa katika
maeneo ya uwakilishi ili kuzihakikishia sekta hizo mageuzi makubwa ya kiuchumi” alisema Balozi Mulamula.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya
TPSF, Bi. Angelina Ngalula pamoja na wajumbe alioambatana nao wameipongeza na
kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
kuweka mkazo wa kuinua sekta binafsi.
Akifafanua Bi. Ngalula ameeleza
juu ya uwepo wa mafanikio katika sekta za biashara, Utalii, uwekezaji, kilimo, madini,
huduma, uchukuzi na usafirishaji na ujenzi.
“Sisi sekta binafsi tunaishukuru
Serikali yetu kwa kuboresha mazingira ya biashara, sasa tunashuhudia mipaka
inafunguka sambamba na ongezeko la watalii kupitia jitihada za makusudi
zinazofanyika katika kuitangaza filamu ya “Tanzania the Royal Tour” alisema Bi.
Ngalula
Aidha, akafafanua matokeo
yaliyopatikana kupitia ziara za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Samia Suluhu Hassan, kwamba kupitia ziara hizo mikutano na makongamano ya
biashara yalifanyika katika nchi mbalimbali na yamesaidia kupatikana kwa washirika
wa kibiashara kutoka mataifa hayo.
Kupitia mazungumzo hayo Waziri
Mulamula na Wawakilishi wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi, wamekubaliana
kuanzisha timu maalum ya uratibu na ufuatiliaji wa masuala mbalimbali ya
kimkakati kitaifa, kwa lengo la kuimarisha na kukuza diplomasia ya uchumi
nchini.
Kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga akifafanua jambo katika mazungumzo hayo. |
Balozi Mulamula akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya TPSF, Bi. Ngalula vitabu vya Diplomasia ya Uchumi. |
Picha ya Pamoja. |
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
Nchi za Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimetakiwa kuweka mikakati ya muda mrefu ili kukuza, kuendeleza na kueneza lugha ya Kiswahili duniani.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Bw. Khamis Abdalla Saidi aliyemwakilisha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mhe.Tabia Maulid Mwita katika Kongamano la kwanza la Siku ya Kiswahili Duniani lililoanza leo tarehe 6 Julai, 2022 Zanzibar.
Kongamano hilo linalongozwa na Kauli Mbiu: “Kiswahili kwa Amani, Ustawi na Utangamano wa Kikanda” litahitimishwa kwenye siku ya Kilele cha Siku ya Kiswahili duniani tarehe 7 Julai 2022.
Katika hotuba yake, Bw. Saidi amesema kuenea kwa Kiswahili katika ukanda wa Afrika Mashariki na Mataifa mengine ni bidhaa ya bishara, hivyo umuhimu wa Kiswahili ni mkubwa katika kupiga hatua ya kimaendeleo.
“Ni jukumu la kila mmoja wetu kukifuatilia Kiswahili katika kila hatua na kutafuta na kubuni njia na mikakati ya muda mrefu na ya kisasa ya kuikuza lugha hii adhimu ya Kiswahili,” amesema Bw. Saidi.
Bw. Saidi aliongeza Lugha ya Kiswahili inatakiwa itumike kama bidhaa inayouzwa na kupata tija. Kuna haja kubwa ya kuwekeza kuwasomesha wataalamu wa lugha kuwa na stadi na uwezo unaotakiwa katika kutoa huduma ya kufundisha, ukalimani, kutafrisi na kuandaa machapisho mbali mbali kwa Kiswahili.
“Ni jukumu la vyuo vikuu vya Afrika Mashariki kutilia mkazo mikakati ya muda mrefu ya uwekezaji wa kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili kwa kufanya tafiti mbalimbali za lugha,” ameongeza Bw. Saidi.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote amesema kuwa jumuiya ya Afrika Mashariki inapaswa kushirikiana kwa pamoja na wadau wa Lugha ya Kiswahili ili kuweza kupata uzoefu wa matumizi ya Kiswahili pamoja na kujadili changamoto za lugha hiyo ili kuimarisha utangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
“Matumizi sahihi ya lugha ya Kiswahili yataimarisha utangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuwa lugha hii ni lugha ya biashara hivyo tunapaswa kujivunia lugha hii adhimu kwa maslahi mapana ya jumuiya yetu,” amesema Mhandisi Mlote.
Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa (MS TCDC), Bi. Yusta Mganga amesema licha ya kuimarika kwa matumizi ya Lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ukanda huo unapaswa kuchukua hatua madhubuti zaidi kwa ajili ya kuhakikisha lugha ya Kiswahili inakuzwa na kuendelezwa miongoni mwa nchi ambazo bado hazijaimarika katika matumizi ya Kiswahili.
“Kuna njia mbalimbali za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili kama vile kufanya tafiti, uandaaji wa makongamano na semina mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya Kiswahili…….katika kuandhimisha siku hii muhimu ni vyema tukatafakari mafanikio ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya yetu ili kuimarisha amani na utangamano wa kikanda,” amesema Bb. Mganga
Novemba 23, 2021 Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) lilitangazwa rasmi kuwa tarehe 7 Julai ya kila mwaka ni siku maalumu ya kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani.
Februari 2022, Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika katika mkutano wake wa kawaida wa 35 walipitisha Kiswahili kama Lugha ya Kazi na mawasiliano mapana Barani Afrika.
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote akitoa hotuba yake katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar |
Meza Kuu wakifuatilia kikundi cha ngoma za asili kutoka Zanzibar wakati wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar |
Washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani wakifuatilia kikundi cha ngoma za asili kutoka Zanzibar |
Washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani wakiimba wimbo wa Taifa |
Washiriki wa Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani wakifuatilia Kongamano hilo lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar |
Meza Kuu katika picha ya pamoja na wawakilishi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililofanyika kuanzia tarehe 6 – 7 Julai, 2022 Zanzibar |