Friday, April 12, 2019

Profesa Kabudi amekutana Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi alipofika kujitambulisha rasmi baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara hiyo. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi wa kwanza kulia akimwelezea jambo Prof. Palamagamba John Kabudi, wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi. 

Waziri wa Mabo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi wa Pili kutoka Kushoto akielezea msimamo wa Wizara yake katika kuzitangaza fursa za Uwekezaji zilizopo Zanzibar. Wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mwinyi.

Profesa Palamagamba John Kabudi wa Pili kutoka Kushoto akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
=====================

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi  (Mb.) amesema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuwa Taifa moja linaloendelea kudumu muda wote kutokana na misingi imara iliyowekwa na Waasisi wa Taifa hilo.
Amesema yapo Makabila mengi katika Mikoa na Wilaya mbali mbali Nchini lakini muungano wa lugha moja inayozungumzwa na Wananchi wake Bara na Zanzibar imekuwa mfano kwa Mataifa mengine Duniani.
Profesa Palamagamba John Kabudi ameeleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Vuga Mjini Zanzibar alipofika kujitambulisha baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ameongeza kuwa yapo Mataifa mengi Duniani yaliyowahi kuunganisha Nchi zao akitolea Mfano iliyokuwa Yugoslavia na sasa imesambaratika pia Senegal na Gambia kwa upande Afrika lakini zimeshindwa kuendeleza Muungano wao.
Waziri Palamagamba John Kabudi alisema wakati Serikali zote mbili zikiendelea kuheshimu kwa kuweka Kumbukumbu za Waasisi hao ambao ni Hayati Mzee Abeid Amani Karume na Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Vizazi vya sasa vinapaswa kujifunza tabia ya Viongozi hao walioacha misingi imara ya kitaifa. 

Akigusia suala la Diplomasia ya Uchumi ambayo kwa sasa Tanzania imeelekeza nguvu zake kupitia Balozi zake zilizoko nje ya mipaka ya Tanzania Profesa Palamagamba John Kabudi amesema Serikali inaendeleza mfumo wa kushawishi Wawekezaji ili kuunga mkono jitihada za Taifa za kuwa na Tanzania ya Viwanda ifikapo Mwaka 2025.
Amesema mkakati wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wa Kuimarisha Uchumi wake unapaswa kuungwa mkono na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika muelekeo wa kuelekea kwenye Maendeleo ya haraka.
Akigusia Sekta ya Utalii kufanya vyema Zanzibar, Waziri Palamagamba amesema Sekta hiyo ni muhimu hivi sasa kwa mapato ya Taifa na nilazima iwekewe utaratibu wa pamoja utakaosaidia kuuza haiba ya pande zote mbili za Muungano.
Alisema vipo vivutio vinavyopaswa kutangazwa kwa pamoja Bara na Zanzibar ambavyo vinaweza kutoa nguvu ya ushawishi wa Watalii kufanya ziara ya kutembelea sehemu zote mbili kwa wakati mmoja.
Waziri huyo wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alielezea faraja yake kutokana na Zanzibar kupiga hatua kubwa katika kuimarisha Sekta ya Utalii inayotoa ajira kubwa hasa kwa Vijana.
Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema ushawishi wa Uwekezaji ndani ya Visiwa vya Zanzibar unapaswa kuungwa mkono na Ofisi zote za Kibalozi za Tanzania zilizopo Mataifa mbali mbali Duniani.
Alisema Zanzibar ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ushawishi wake kwa Wawekezaji na Mataifa ya kigeni unawajibika kusimamiwa na Mabalozi wa Tanzania kupitia Wizara yake ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Balozi Seif alimueleza Profesa Palamagamba John Kabudi kwamba Zanzibar kupitia Viongozi wake wote waliopita na waliopo hivi sasa bado wanaendeleza sera na Mikakati iliyoachwa na Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Mzee Abeid Amani Karume.
Alisema uimarishaji wa Miundombinu ya Mawasiliano, Ujenzi wa Nyumba za Kisasa za Maendeleo, Afya, Elimu pamoja na huduma za Maji safi na salama ni miongoni mwa Sekta zinazoendelea kuimarishwa na Viongozi wote.
Balozi Seif Ali Iddi alimweleza Profesa Palamagamba John Kabudi, kuwa Miradi iliyobuniwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo ujenzi wa Miji Mipya kama ule wa Ng’ambo tuitakayo katika eneo la Kwahani na Mtaa wa Chumbuni imelenga kustawisha maisha ya Wananchi wake ili kuachana na matumizi mabaya ya Ardhi ndogo iliyopo visiwani humo.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
12 Aprili, 2019.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Mtaalam wa Uchumi kutoka Ujerumani


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza wakati wa kikao na Prof. Helmut Asche (kulia) ambaye ni Mtaalam wa Uchumi hususan masuala yanayohusiana na Ubia wa Kiuchumi kati ya Ulaya na Afrika (EPA) kutoka Ujerumani. Kikao hicho kilifanyika hivi karibuni jijini Dodoma.
Prof. Asche kutoka Ujerumani akizungumza kwenye kikao kati yake na Naibu Waziri, Mhe. Ndumbaro. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akimsikiliza Prof. Asche. 
Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Prof. Asche akifafanua jambo kuhusu EPA wakati wa kikao kati yake na Mhe. Dkt. Ndumbaro huku wajumbe wengine wakifuatilia. Kulia ni  Bw. Jestas Nyamanga, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Dkt. Mnyepe (kulia) akiwa na Dkt. Edwin Mhede (katikati), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wakifuatilia kikao. 
Kikao kikiendelea
Mhe. Dkt. Ndumbaro akiteta jambo na Prof. Asche mara baada ya mazungumzo kati yao
Mhe. Dkt. Ndumbaro akiwa na Prof. Asche na wajumbe wengine wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima ya Prof. Asche.


Thursday, April 11, 2019

Vivutio vya Utalii kutangazwa Malaysia, Ufilipino, Thailand na Indonesia

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Vivutio vya Utalii kutangazwa Malaysia, Ufilipino, Thailand na Indonesia

Dodoma, 11 Aprili 2019

Makampuni 20 ya Mawakala wa Utalii na Tiketi za ndege (Tour Operators & Travel Agents) pamoja na Waandishi wa Habari kutoka katika nchi za Malaysia, Indonesia, Ufilipino na Thailand walifanya ziara ya mafunzo ya kutembelea vivutio vya utalii nchini  kuanzia tarehe 1 – 7 Aprili 2019.

Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Malaysia kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) yalijumuisha washiriki 20 ambapo Malaysia ilitoa washiriki 5, Thailand washiriki 6, Philippines Washiriki 4 na Indonesia washiriki 5.

Washiriki hao walitembelea maeneo mbalimbali yakiwemo Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro, Mbuga ya Serengeti, duka Maarufu la kuuza madini ya Tanzanite, duka maarufu la zawadi la Arusha Cultural Heritage, sehemu ya historia ya masalia ya Binadamu wa Kale la Olduvai (Oldupai) Gorge na Kijiji cha Wamasai ili kujifunza uhalisia wa maisha yao. Wakiwa kwenye maeneo hayo, wageni walifanikiwa kuona wanyama maarufu watano- big five (Simba, Nyati, Faru, Chui na Tembo) na kushuhudia makundi ya Wanyama aina ya Nyumbu, Pundamilia, na Swala ambao hufanya ziara ya mzunguko maarufu kama Great Migration.

Wageni kabla ya kuagwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo pamoja na Bibi. Devotha Mdachi, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii waliahidi kuitangaza Tanzania kama eneo jipya la utalii kwa nchi zao.

Wakati huo huo, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Dkt. Ramadhani Dau amepokea nafasi 160 za ufadhili wa masomo ya elimu ya juu (scholarships) kwenye taaluma mbalimbali zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 1.9 sawa na Shilingi bilioni 4 za Tanzania. Ufadhili huo umetolewa na Chuo Kikuu cha Selangor (University of Selangor) ambacho pia kinajulikana kama UNISEL kilichopo katika Mkoa wa Selangor, Malaysia, unahusisha masomo ya Bachelors of Civil Engineering, Bachelors of Electrical Engineering, Bachelors of Mechanical Engineering, Bachelors of Occupational Health and Safety, Bachelors of Medical Laboratory, Bachelors of Industrial Biotechnology, Bachelors of Computer Science na Bachelors of Information Technology. Hivi karibuni Watanzania watafahamishwa utaratibu wa kuomba masomo hayo.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Rais na Makamu Mkuu wa Chuo cha Kikuu cha UNISEL, Prof. Dkt. Mohammad Redzuan Bin Othaman akimkabidhi barua yenye kuainisha ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kwa Watanzania kwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Dkt. Ramadhani Dau.
Dkt. Dau akiangalia miundombinu ya Chuo Kikuu cha UNISEL
Moja ya Vyumba vya madarasa

Dkt. Dau akipata maelezo kuhusu uendeshaji wa chuo hicho.
Wageni kutoka Malaysia, Indonesia, Thailand na Ufilipino walipowasili Tanzania kwa ajili ya ziara ya mafunzo kwenye vivutio vya utalii.
Wageni kutoka Malaysia, Indonesia, Thailand na Ufilipino wakipata chakula.
Balloon lililowabeba wageni kuwazungusha katika mbuga ya Serengeti.


Wednesday, April 10, 2019

Waziri Kabudi akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akimkaribisha Balozi wa Ufaransa nchini, Mheshimiwa Frédéric Clavier alipomtembelea ofisini kwake  jijini Dodoma tarehe 10 Aprili 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo baina yake na Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Frédéric Clavier. Katika mazungumzo hayo Tanzania na Ufaransa wamekubaliana kushirikiana katika kilimo cha zabibu, uzalishaji na uuzaji wa mvinyo katika nchi mbalimbali duniani na usafiri wa anga.
Mazungumzo yakiendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Palamagamba John Kabudi akiagana na Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Frédéric Clavier baada ya mazungumzo baina yao.


Prof. Kabudi azungumza na Uongozi wa Airtel jijini Dodoma.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa kampuni ya Simu ya Airtel, mazungumzo hayo yamefanyika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma Tarehe 10 Aprili,2019.
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Kampuni ya Simu za Mkononi Airtel nchini, wapili kutoka kushoto ni Mwanasheria wa Bharti Airtel Bw. Mukesh Bhavnani, wa kwanza kulia Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw. Sunil Colaso na wakwanza kilia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Bi. Beatrice Singano.


========================================


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) leo tarehe 10 Aprili,2019 Jijini Dodoma amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Kampuni ya Simu za Mkononi Airtel ukiongozwa na Bw. Mukesh Bhavnani, Mwanasheria wa Bharti Airtel, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw. Sunil Colaso na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Bi. Beatrice Singano.

Katika mazungumzo hayo, Uongozi wa Airtel umemuhakikishia Mheshimiwa Kabudi kuwa Kampuni ya Bharti Airtel itaendelea kuwa Mbia mzuri na Serikali na kwamba wataendelea kupanua wigo wa huduma zao katika maeneo yote nchini na kuhakikisha hudua hizo zinakuwa za viwango na nafuu kwa watumiaji. Na kwamba mpango wao wa uwekezaji na kupanua wigo wa huduma zao hususan maeneo ya vijijini utakuwa moja ya chachu ya maendeleo ya kiuchumi nchini.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Kabudi pamoja na kuwashukuru kwa kumtembelea ameihakikishia Bharti Airtel kuwa Serikali iko tayari kuendelea na ubia walionao na iko tayari kuendelea kushauriana na kushirikiana namna bora ya kuimarisha ubia huo ili kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakuwa na viwango na zinafika katika maeneo mengi nchini kwa gharama nafuu.

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano  wa Afrika Mashariki, Dkt.  Faraji Kasidi Mnyepe  alikutana   na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini, Mheshimiwa Frédéric Clavier. Mazungumzo yao yalifanyika hivi karibuni katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma. 

Mazungumzo yakiendelea

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano  wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, akiagana na Balozi wa Ufaransa nchini, Mheshimiwa Frédéric Clavier, mara baada ya mazungumzo kati yao.

Prof. Kabudi akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Belarus nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, tarehe 9 Aprili, 2019, alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Belarus nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mheshimiwa Dmitry Kuptel. Balozi Kuptel yupo nchini kwa ziara ya siku nne kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Belarus.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akimuonesha  Balozi Dmitry Kuptel ulipo mkoa wa Dodoma  wakati alipokuwa akimuelezea Balozi huyo kuhusu uamuzi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuhamia Dodoma.

Ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashiriki ambao unaohusisha Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Emmanuel Buhohela (wa kwanza kulia),  Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Bibi Caroline Chipeta (kushoto kwa Waziri) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mohamed Kamal (katikati)  wakimsikiliza Mhe. Waziri Kabudi wakati wa  mazungumzo yake na  Balozi wa Belarus (hayupo pichani)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe  wa Tanzania na Belarus ulioshiriki katika mazungumzo hayo.

Tuesday, April 9, 2019

Prof. Kabudi ahimiza wawekezaji kutoka nchi za Nordic kuja kuwekeza Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof.  Palamagamba John Kabudi (Mb.), leo tarehe 9 Aprili, 2019 akiwa jijini Dodoma amefungua rasmi Kongamano la kwanza la Uwekezaji pamoja na Mkutano wa mwaka wa Diaspora wa Tanzania linalofanyika nchini Sweden. Ufunguzi wa kongamano hilo ulirushwa moja kwa moja na  Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1). Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe.

 Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Kasidi Faraji Mnyepe, wakifuatilia kongamano hilo lililorushwa moja kwa moja na TBC 1 huku wao wakiwa Dodoma.

Kongamano likiendelea.

Monday, April 8, 2019

Tanzania na Romania zakubaliana kuimarisha ushirikiano



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Palamagamba John Kabudi(Mb.), akiwa katika mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Rais wa Romania katika Masuala ya Umoja wa Mataifa (UN),  Balozi Daniela Gitman. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John  Kabudi, akimwonesha Balozi Daniela Gitman (katikati) ulipo mkoa wa Dodoma katika ramani ya Tanzania
Mjumbe Maalum wa Rais Klaus Iohannis wa Romania katika Umoja wa Mataifa (UN)  Balozi Daniella Gitman (kushoto) akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) ujumbe maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Romania. Wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mona Mahecha.