Monday, October 15, 2012

Balozi wa Japan hapa nchini aongoza ujumbe kuonana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifafanua jambo kwa wageni waliofika kumtembelea Ofisini kwake leo. Kulia kwa Balozi Kairuki ni Mhe. Masaki Okada, Balozi wa Japan hapa nchini akifuatiwa na Bw. Yoshiyasu Mizuno, Mshauri wa masuala ya Maendeleo ya Viwanda kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara ya hapa nchini. Anayewatazama ni Bw. Takuya Osada kutoka Kampuni ya Global Business Division ya Japan.

Balozi Kairuki (katikati) akiwa na Balozi Okada (kushoto) na Bw. Mizuno wakimsikiliza Bw. Takuya (hayupo pichani) wakati ujumbe huo ulipofika kumtembelea Balozi Kairuki Ofisini kwake leo.

Bw. Takuya akimsikiliza kwa makini Balozi Kairuki (hayupo pichani) alipokuwa akimweleza masuala mbalimbali baada ya kumtembelea ofisini kwake. Anayendika ni Afisa kutoka Ubalozi wa Japan hapa nchini.


Balozi Kairuki akifurahia jambo na Bw. Mizuno wakati wa kuagana baada ya mazungumzo yao.

Mkurugenzi wa Asia akutana na Mwakilishi wa Heshima wa Australia hapa nchini

Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akimkaribisha Ofisini kwake Bw. Thiery Murcia, Mwakilishi wa Heshima wa Australia hapa nchini alipomtembelea leo.

Balozi Kairuki akiwa katika mazungumzo na Bw. Murcia.

Balozi Kairuki akimsikiliza kwa makini Bw. Murcia alipokuwa akizungumza nae.

Balozi Kairuki akipitia moja ya nyaraka muhimu alizokabidhiwa na Bw. Murcia wakati wa mazungumzo yao.

Saturday, October 13, 2012

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Ireland hapa nchini

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Fionnuala Gilsenan, Balozi mpya wa Ireland hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam jana.

Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Mhe. Balozi Gilsenan, Bibi Grace Shangali, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Anayeshuhudia pembeni mwa Bibi Shangali ni Bi. Felista Rugambwa, Afisa Mambo ya Nje.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Gilsenan mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Gilsenan mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo. Pembeni mwa Balozi ni Bw. Nicholas Michael, Afisa katika Ubalozi wa Ireland hapa nchini.

Mhe. Balozi Gilsenan akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais.

Mhe. Balozi Gilsenan akisikiliza na kufurahia wimbo wa Taifa lake ulipokuwa ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Wengine katika picha kulia kwa Balozi ni Bw. Shaaban Gurumo, Mnikulu na Bw. Japhet Mwaisupule, Kaimu Mkuu wa Itifaki.

Mhe. Balozi Gilsenan akisalimiana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi, Inspekta Billy Kachalle mara baada ya kumaliza kupiga nyimbo za mataifa ya Tanzania na Ireland kwa heshima ya Balozi huyo.

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Cuba hapa nchini

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo, Balozi mpya wa Jamhuri ya Cuba hapa nchini.Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam jana.

Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha Mhe. Mahadhi Juma Maalim (kushoto wanaosalimiana), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mhe. Balozi Tormo. Anayeshuhudia pembeni mwa  Mhe. Naibu Waziri ni Bibi Grace Shangali, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Mhe. Balozi Tormo mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho za Balozi huyo. Pembeni mwa Balozi ni Mke wake Bibi Maria Griselda Herviz.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Tormo na mkewe Bibi Herviz mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo.

Mhe. Balozi Tormo akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.

Mhe. Balozi Tormo akisikiliza Wimbo wa Taifa lake uliokuwa ukipigwa na Bendi ya Polisi (haipo pichani) kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Wengine katika picha ni Bw. Shaaban Gurumo (kulia kwa Balozi), Mnikulu na Bw. Japhet Mwaisupule (kushoto kwa Balozi), Kaimu Mkuu wa Itifaki.

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Korea hapa nchini

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisubiri kupokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Chung IL, Balozi mpya wa Jamhuri ya Korea hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam jana.

Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Mhe. Balozi  IL mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho za Balozi huyo. Kulia kwa BaLozi IL ni mkewe Bibi Junghwa Moon.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi IL na mkewe Bibi Junghwa Moon mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho za Balozi huyo.

Mhe. Balozi IL akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.

Mhe. Balozi IL akisikiliza Wimbo wa Taifa lake uliokuwa ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Wengine katika picha ni Bw. Shaaban Gurumo (kulia kwa Balozi) ambaye ni  Mnikulu na Bw. Japhet Mwaisupule (kushoto kwa Balozi), Kaimu Mkuu wa Itifaki.

Friday, October 12, 2012

Mhe. Naibu Waziri apokea Hati za Utambulisho za Mwakilishi wa UNICEF hapa nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (kushoto) akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Bw. Jama Gulalid, Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) hapa nchini.

Mhe. Naibu Waziri akifafanua jambo wakati wa mazungumzo  na Bw. Gulalid mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho.

Bw. Gulalid akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kukabidhi Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Naibu Waziri (hayupo pichani).

Mhe. Naibu Waziri akifurahia jambo wakati wa kuagana na Bw. Gulalid mara baada ya mazungumzo yao.

Naibu Waziri akutana na Balozi wa India hapa nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (kulia) akisalimiana na Balozi wa India hapa nchini, Mhe. Debnath Shaw aliyefika ofisini kwa Mhe. Naibu Waziri kwa lengo la kujitambulisha ambapo pia walizungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.

Mhe. Naibu Waziri (kulia) akizungumza masuala mbalimbali na Mhe. Balozi Shaw wakati Balozi huyo alipofika ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha.

Mhe. Balozi Shaw (kushoto) akizungumza  huku  Mhe. Naibu Waziri akimsikiliza kwa makini.

Mhe. Balozi Shaw akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili ofisini kwa Mhe. Naibu Waziri.

Mhe. Naibu Waziri akiendelea na mazungumzo na Mhe. Balozi Shaw. Wengine katika picha ni Bw. Charles Faini (kushoto kwa Mhe. Naibu Waziri), Afisa Mambo ya Nje na Bw. D.K. Pant (kulia kwa Mhe. Balozi) Afisa kutoka Ubalozi wa India hapa nchini.

Wednesday, October 10, 2012

Tanzania addresses the Third Committee of the UN General Assembly



H.E. Ambassador Tuvako Manongi, Permanent Representative of the United Republic of Tanzania to the United Nations, yesterday addressed the Third Committee (Social, Humanitarian and Cultural), of the 67th Session of the General Assembly on Agenda item 27:  Social Development.

During his Statement, Ambassador Manongi emphasized the linkage between poverty and disability, including the need to incorporate people with disabilities in development agendas.

 

 
Photo by Mrs. Maura Mwingira of the Tanzania Mission to the United Nations 
 
 
 

Coverage of the Main Committees of the General Assembly Meetings

 
 
          Chairman of the Fifth Committee for 67thsession of the United Nations General Assembly, H.E. Miguel Berger, Ambassador and Deputy Permanent Representative of Germany gives his opening remarks, where he welcomes new elected members of Bureau that includes himself as Chairman, Mr. João Augusto Costa Vargas of Brazil, Ms. Anna Reich of Hungary and Mr. Bilal Taher Muhammad Wilson of Saudi Arabia as vice-chairpersons and Mr. Justin Kisoka of the United Republic of Tanzania as Rapporteur. He also thanked the previous Bureau which was under the Chairmanship of His Excellency, Mr. Michel Tommo Monthé of Cameroon. 

During the discussion, the Committee pointed out the need for careful examination of all important agenda items, such as human resources management, the scale of assessments, Umoja/Enterprise Resource Planning and the International Public Sector Accounting Standards, the United Nations common system, Programme Planning, Capital Master Plan and the reports of the Board of Auditors (BOA); Joint Inspection Unit (JIU) and the Office of Internal Oversight Services (OIOS). Other items includes budget revised estimates such as financing the outcome on RIO+20, Economic and Social Council (ECOSOC), Human Right Council (HRC) and other main committee decisions.
 
 
Rapporteur of the Fifth Committee, Mr. Justin Kisoka (Tanzania) (left),listening to Ambassador Berger's remarks. Others are Mr. Collen Kelapile (center),Chair of the Advisory Committee on Administrative and Budgetary Questions (ACABQ) and Mr. Yukio Takaso (right), UN Under Secretary-General for Management.

Tanzania delegation is expected to be key players in number of the agenda items in this Session that include full involvement in the negotiation on programme planning, human resource management, UN Common system; oversight reports in particular the BOA, JIU and OIOS, UN pension system, scale of assessment, budgets for ICTR and International Residual Mechanism including construction project in Arusha in line with national priorities.
 
 
Mr. Kisoka (center) and Mr. Amos Tengu (left), Tanzania Delegates to the Fifth Committee chatting with Mr. Samakande, Representative of Zimbabwe Delegation to the Fifth Committee, during the opening session at the UN Headquarter in New York.
 
 
Mr. Elisha Suku (right), Legal Officer and Mr. Lucas Mayenga, Foreign Service Officer from the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation, closely following the deliberation of the Sixth Committee (Legal and Administrative) Meeting of the United Nations General Assembly.
 
 
Ms. Swahiba Mndeme, Foreign Service Officer from the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation, during her participation at the First Committee (Disarmament and International Security) Meeting of the UN General Assembly.
 
 
 
All photos by Tagie Daisy Mwakawago
 
 

 

Monday, October 8, 2012

UN’s Committee Meetings officially kick off




UN’s Committee Meetings officially kick off
By TAGIE DAISY MWAKAWAGO, New York
8 October, 2012
As the General Debate of the United Nations' 67th Session closed its Session last week (1 October, 2012), the Six Committees of the UN have commenced their meetings with Tanzania Delegation gearing for its full participation in all Committees.
The Six Committees are: First Committee (Disarmament and International Security), Second Committee (Economic and Financial), Third Committee (Social, Humanitarian and Cultural), Fourth Committee (Special Political and Decolonization), Fifth Committee (Administrative and Budgetary) and the Sixth Committee (Legal and Administrative).

Ambassador Tuvako Manongi, Permanent Representative of the United Republic of Tanzania to the United Nations, is expected to address the Third Committee on 9 October, 2012 where he will highlight the Government's position in its continued implementation on various national strategies programmes such as poverty reduction (MKUKUTA for Mainland and MKUZA for Zanzibar).   

Furthermore, the Ambassador will also speak on the challenges of high maternal and child mortality rates, including unemployment-related issues.

On 10 October, 2012 Ambassador Manongi is expected to address the First Committee where Tanzania will make pledge for full cooperation and support to attain total and complete disarmament. Tanzania will also call upon other nuclear states and possessors to embark on the path of total and complete disarmament of such weapons, in guaranteeing peace, security and development.

Participants for the Committees will also include Deputy Ambassador Ramadhan Muombwa Mwinyi, Deputy Permanent Representative of the United Republic of Tanzania to the United Nations and Mr. Nyandallo M. Mboyi, Acting Director of the Department of Policy and Planning in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.  
Others include Foreign Service Officers from the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation and the Tanzania Permanent Mission to the UN, Ministry of Health and Social Welfare, Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development, President’s Office - Planning Commission, Ministry of Finance, Ministry of Home Affairs and others.
All meetings are held at the United Nations Headquarters in New York, USA and are scheduled to last until December 2012.


End.


Saturday, October 6, 2012

Malawi rudini kwenye meza ya majadiliano:Membe


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) amewambia Waandishi wa Habari kuwa Malawi haiwezi kuipeleka Tanzania katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) ili iamue mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa unaozozaniwa baina ya nchi hizi mbili.

Mhe. Membe alibainisha hayo mbele ya Waandishi wa Habari jijini Dar es Slaam siku ya Jumamosi tarehe 06 Oktoba, 2012. “Tanzania ni mjumbe wa ICJ lakini bado haijatambua Mamlaka ya Mahakama hiyo, hivyo Malawi haiwezi kuipeleka Tanzania ICJ isipokuwa Tanzania inaweza kuipeleka Malawi”, alisema Mhe. Membe.

Mhe. Waziri aliitolea wito Malawi irudi katika meza ya majadiliano na kuiomba Serikali ya nchi hiyo kutuma wawakilishi katika kikao walichokubaliana kufanyika Dar es Salaam kuanzia tarehe 07 - 10 Oktoba, 2012. Kikao hicho kinakusudia kupendekeza msuluhishi ambaye atakubalika na pande zote baada ya kubainika kuwa Tanzania na Malawi zenyewe hazitaweza kusuluhisha mzozo huo.

Mhe. Waziri aliwafahamisha waandishi kuwa alipokea kwa mshtuko taarifa kwamba Malawi haitashiriki katika kikao kilichopangwa kufanyika Dar es Salaam kwa hoja kuwa lazima Serikali ya Tanzania itoe maelezo ya kina kuhusu boti ya kijeshi iliyoonekana kufanya doria kwenye Ziwa Nyasa ambayo inasemekana kuwaletea hofu kubwa wakazi wa maeneo ya Ziwa kwa upande wa Malawi. Aidha, Malawi inataka kupatiwa maelezo kuhusu toleo jipya la Ramani ya Tanzania lililotolewa na Mamlaka za Tanzania ambayo inaonyesha mpaka baina ya nchi hizo mbili umepita katikati ya Ziwa Nyasa.

Akitolea ufafanuzi masuala hayo, Mhe. Membe alisema kuwa toleo hilo jipya lilikuwa na lengo la kuionyesha Mikoa mipya minne na Wilaya mpya 19 katika ramani ya nchi, na kuonyesha mpaka kupita katikati ya Ziwa, hilo si jambo jipya kwani ndivyo ramani ya nchi yetu ilivyokuwa katika matoleo yote manne yaliyotolewa na Serikali kabla na baada ya uhuru.

Kuhusu boti ya kijeshi kufanya doria kwenye Ziwa Nyasa, Mhe. Waziri alisema taarifa hizo sio sahihi, ila kinachofanyika ni doria ya kawaida ambayo inaendeshwa na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kuwasaka wavuvi haramu na wale wanaotumia zana za uvuvi zilizopigwa marufuku.

Mhe. Waziri aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali ya Tanzania inapenda kuona mgogoro huo unamalizika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne inayongozwa na Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete na kitendo cha Malawi kutishia kugomea majadiliano hakitarudisha nyuma dhamira ya Serikali.

Alisema Serikali imejipanga vyema kuhakikisha kuwa inakuwa na hoja za kisayansi na kisheria ili ishinde katika mgogoro huo. Moja ya mikakati ya Serikali imeunda Kamati tatu ambazo zimeshaanza kazi na kazi yao inaendelea vizuri. Kamati hizo moja inahusika na utafutaji wa nyaraka kuhusu Ziwa Nyasa, ya pili inahusika na masuala ya kisheria na ya tatu inahusika na masuala ya majadiliano.

Alidokeza kuwa katika kufuatilia kesi zilizohukumiwa na ICJ hakuna nchi iliyodai umiliki wa ziwa lote au mto uliopo mpakani baina ya nchi mbili ilishinda kesi. Hivyo, aliwataka Watanzania wasiwe na wasiwasi kwani Serikali yao itaibuka mshindi katika mgogoro huo.

Alihitimisha mazungumzo yake kwa kuwataka Wananchi wanaoishi kando ya Ziwa Nyasa kufanya shughuli zao kama kawaida pasi na kuhofia chochote kwani hakuna tishio la vita kabisa baina ya Tanzania na Malawi. 

Habari na Ally Kondo.


Mkutano kati ya Waziri Membe na Waandishi wa Habari kuhusu mgogoro wa mpaka katika Ziwa Nyasa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati) akifafanua kwa  Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu hoja zilizotolewa na Serikali ya Malawi za kujitoa katika mazungumzo kuhusu mgogoro uliopo kati  ya Tanzania na Malawi kuhusu Ziwa Nyasa. Wengine katika picha kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule  na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju.

Baadhi ya Waandishi wa Habari kutoka Vyombo na Mashirika mbalimbali ya Habari hapa nchini wakimsiliza kwa makini Mhe. Waziri Membe.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikino wa Kimataifa, Bw. John M. Haule (aliyesimama) wakati akimkaribisha Mhe. Waziri Membe kuzungumza na  Waandishi wa Habari (hawapo pichani).

Mmoja wa Wanahabari  Bw. Florian Kaijage akiuliza swali wakati wa mkutano wao na Mhe. Waziri Membe.

Mhe. Waziri Membe akijibu swali kwa msisitizo aliloulizwa.

Mhe. Waziri Membe (waliokaa kushoto) akionesha kwa Waandishi wa Habari Ramani mpya ya Tanzania. Wengine katika picha (aliyekaa kulia) ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule akifuatiwa na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Selasie Mayunga na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria hapa Wizarani Balozi Irene Kasyanju.

Mhe. Waziri Membe akifafanua kwa Waandishi wa Habari kuwa mpaka katika ramani ya Tanzania umepita katikati ya Ziwa Nyasa na si ufukweni kama inavyodaiwa na Malawi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule,  akimsikiliza kwa makini Mhe. Waziri Membe wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiririkiano wa Kimataif, Balozi Irene Kasyanju akiwa makini kusikiliza ufafanuzi uliokuwa unatolewa na Mhe. Waziri Membe kwa Waandishi wa Habari kuhusu mgogoro wa Tanzania na Malawi juu ya Ziwa Nyasa.

Wageni waalikwa na baadhi ya waandishi wakimsikiliza Mhe. Waziri Membe.