Sunday, September 10, 2023

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI WATUMIA SIKU YA AFRIKA KUTANGAZA FURSA NA UTAMADUNI WA TANZANIA


Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola (mwenye nguo yenye nakshi za bendera ya Tanzania) akimshuhudia Waziri wa Viwanda na Biashara wa Malawi, Mhe. Simplex Chithyola akionja chakula cha kitanzania wakati wa maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika yaliyofanyika jijini Lilongwe tarehe 09 Septemba 2023. Ubalozi wa Tanzania umeshiriki maadhimisho hayo kwa kutangaza fursa za uwekezaji, utalii kupitia Filamu ya The Royal Tour na kuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili.
 Mhe. Chithyola akifurahia chakula cha kitanzania alipotembelea banda la Tanzania wakati wa  Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika yaliyofanyika jijini Lilongwe hivi karibuni. Wengine katika picha ni Mhe. Balozi Kayola na wageni wengine waliotembelea Banda la Tanzania.

   
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja

========================================

Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  nchini Malawi umeshiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika yaliyofanyika jijini Lilongwe tarehe 9 Septemba, 2023. 

 

Katika kutangaza Diplomasia ya Uchumi, Ubalozi wa Tanzania ulitumia fursa hiyo kutangaza fursa za Uwekezaji, kuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili na kutangaza vivutio vya Utalii kwa kuonesha Filamu ya The Royal Tour. 


Kadhalika Ubalozi ulishirikiana na Watanzania Diaspora wanaoishi Malawi kuonesha  Utamaduni wa Tanzania ikiwemo vyakula vya asili. 



Banda la Ubalozi wa Tanzania lilitembelewa na wageni wengi ambao walipendezwa na vyakula vya asili kutoka Tanzania. 

 

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa  Waziri wa Viwanda na Biashara wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Simplex Chithyola.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.