Thursday, September 28, 2023

WAZIRI BYABATO AKOSHWA NA MRADI WA MABADILIKO YA TABIANCHI WILAYANI MAGU


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) ameeleza kuridhishwa kwake na utekelezaji wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa Victoria (Adapting to Climate change in Lake Victoria Basin – ACC – LVB)kupitia Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) unaotekelezwa katika kijiji cha Ng’haya, Wilayani Magu.

Naibu Waziri Byabato ameeleza hayo alipokuwa ziarani katika Kijiji cha Ng’haya Wilayani Magu tarehe 27 Septemba 2023 ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi katika Kanda ya Ziwa ambapo anatembelea na kuona ufanisi wa miradi mbalimbali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayotekelezwa kupitia LVBC. 

Akipokea taarifa ya utelekezaji wa mradi huo uliogharimu kiasi cha Shilingi 656,785,965 iliyowasilishwa na Watendaji wa Wilaya ya Magu ambapo pia alipata nafasi ya kutembelea miradi hiyo ameleza namna alivyofarijika kuona mradi huo ulivyochangia ustawi wa kiuchumi kwa wananchi wa kijiji cha Ng’haya. 

“Nimefarijika sana na namna mradi huu ulivyowanufaisha wananchi kwa kuwaongezea kipato kupitia miradi iliyotajwa kwenye taarifa yenu ambayo pia muda mfupi ujao nitaenda kuitembelea. Natoa pongezi sana kwa Uongozi na safu nzima ya Watendaji wa Wilaya kwa namna mlivyosimamia utekelezaji wa mradi huu na kufikia malengo mliyojiwekea” Alieleza Naibu Waziri Mhe.Byabato

Utekelezaji wa Mradi huu wa kuhimili mabadiliko ya Tabianchi katika kijiji cha Ng’haya unalenga kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi kwa jamii inayoishi katika bonde la Ziwa Victoria kwa nchi za Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda. Vilevile kujenga uwezo wa jamii inayoishi katika maeneo hayo kuweza kuhimili mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia teknolojia za uvunaji wa maji ya mvua, maji chini ya ardhi, kilimo kinachohimili mabadiliko ya Tabianchi, mbinu zinazozingatia mifumo ya ikolojia katika shughuli zao za kijamii na kiuchumi.

Shughuli zingine zinazotekelezwa Wilayani Magu kupitia mradi huo kwa lengo la kuongeza kipato kwa jamii kupitia kilimo cha kisasa cha bustani na mboga mboga (kupitia vitalu nyumba) vikundi vya ufugaji wakuku, kondoo, unenepeshaji wa ng’ombe, ushonaji nguo na ufugaji wa nyuki. 

Kwa upande wake mwakilishi wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria Bw. Amos Ndoto ameeleza kuwa kwa tathmini iliyofanywa na Kamisheni hiyo imebainisha kuwa Tanzania ndio nchi iliyofanya vizuri zaidi katika utekelezaji wa mradi huo ukilinganisha na nchi wanachama wanaonufaika na mradi, hivyo kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuendelea kunufaika na mradi katika awamu inayofuata.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Byabato alipata fursa ya kutembelea Shule ya Sekondari Ng’haya, Wilayani Magu ambayo inatekeleza Kilimo bora kinachotumia mbinu za kuhimili mabadiliko ya tabianchi (Climate Smart Agriculture) kupitia mradi huo ambao umewawezesha katika ujenzi wa kitalu nyumba kimoja kinachotumika kutoa mafunzo ya kilimo bora kwa vitendo kwa wanafunzi. 

Mradi huu ni wa Majaribio wa Kikanda wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi katika Bonde la Ziwa Victoria unatekelezwa katika Nchi 5, ambazo ni; Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda. Mradi huu ni ulikuwa ni wa miaka 3, ambapo ulianza kutekelezwa mwaka 2019 hadi 2022 kwa ufadhili wa Adaptation Fund (AF)/UNEP) chini ya uratibu wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC). Kwa upande wa Tanzania mradi huu unatekelezwa katika kijiji cha Ng’haya, Wilayani Magu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akisaini kitabu cha wageni alipowasili Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Magu
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akielekeza jambo kwa Viongozi na Watendaji wa Wilaya ya Magu (hawapo pichani) alipokuwa ziarani wilayani humo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akitazama moja ya miundombinu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa unaotekelezwa katika kijiji cha Ng’haya, Magu
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akimsikiliza mratibu wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa Bw. Ngussa Buyamba
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akiwasili kwenye moja ya mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa katika kijiji cha Ng’haya, wilayani Magu
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akielekeza jambo alipotembelea mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa katika kijiji cha Ng’haya, wilayani Magu
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akizungumza na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ng’haya, wilayani Magu Bi.Glory Sulungu Daudi alipotembelea shule hiyo kwa lengo la kujionea mradi wa Kilimo bora kinachotumia mbinu za kuhimili mabadiliko ya tabianchi
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akizungumza na wanafunzi wa Sekondari ya Ng’haya, wilayani Magu
Picha ya pamoja
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akiwa picha ya pamoja na wanafunzi wa Sekondari ya Ng’haya, wilayani Magu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akipanda mti kwenye Shule ya Sekondari ya Ng’haya, wilayani Magu 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.