Wednesday, September 6, 2023

RAIS WA SENEGAL AWASILI NCHINI KUHUDHURIA AGRF 2023

Rais wa Jamhuri ya Sénégal Mhe.Macky Sall  amewasili nchini kuhudhuria Mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika unaofanyika nchini kuanzia tarehe 5-8 Septemba 2023.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam Mhe. Sall alilakiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki.

Mhe.Sall  ni miongoni mwa Wakuu wa Nchi na Serikali, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Marais na Mawaziri Wakuu wastaafu kutoka barani Afrika wanaohudhuria mkutano huo mkubwa unaojadili mifumo ya chakula duniani








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.