Saturday, March 2, 2013

Naibu Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Mwakilishi wa Brazil katika WTO

Balozi Rajabu Gamaha, Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika mazungumzo na Balozi Roberto Azevedo, Mwakilishi wa Serikali ya Brazil katika Shirika la Biashara Duniani (WTO) lenye Makao yake Makuu mjini Geneva, Uswisi, alipofika Wizarani tarehe 2 Machi, 2013 kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe maalum. Balozi Azevedo pia ni mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo.

Mhe. Balozi Azevedo akiwa na ujumbe aliufuatana nao  wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao. Kulia kwa Balozi Azevedo ni Mhe. Fransisco Carlos Luz, Balozi wa Brazil hapa nchini.

Balozi Gamaha akiendelea na mazungumzo na wageni wake.

Balozi Gamaha akimsikiliza Balozi Azevedo wakati wa mazungumzo yao.

Balozi Azevedo akiendelea na mazungumzo na Balozi Gamaha. Wengine katika picha ni Balozi Celestine Mushy (kushoto kwa Bal. Gamaha), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Lucas Mayenga (kulia), Afisa katika Idara hiyo.


Balozi Gamaha akifafanua jambo kwa Balozi Azevedo wakati wa mazungumzo yao

Mhe. Fransisco Carlos Luz (wa kwanza kulia), Balozi wa Brazil hapa nchini pamoja na wajumbe wengine kutoka Brazil wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) alipozungumza nao
Wajumbe wote kwa pamoja wakimsikiliza Balozi Gamaha.
 

Balozi Gamaha akiagana na Balozi Azevedo mara baada ya mazungumzo yao.

Picha ya pamoja.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.