Monday, March 4, 2013

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa azungumza na Balozi mpya wa Uingereza hapa nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, akimkaribisha Wizarani Balozi mpya wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Dianna Melrose alipofika kuzungumza naye kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kimataifa ikiwa ni pamoja na maandalizi ya mkutano wa 39 wa G8 unaotarajiwa kufanyika nchini Uingereza mwezi Juni, 2013.

Balozi Mushy akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Melrose.
Balozi Mushy katika mazungumzo na Balozi Melrose huku Bw. Julian Chandler, Naibu Balozi wa Uingereza akifuatilia mazungumzo hayo.

Mhe. Balozi Melrose akimweleza jambo Balozi Mushy wakati wa mazungumzo yao.


Balozi Mushy akifafanua jambo kwa Balozi Melrose huku Bw. Chandler(kushoto) na Bw. Amos Tengu (kulia), Afisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wakisikiliza kwa makini.








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.