Thursday, March 7, 2013

Waziri Mkuu wa Denmark awasili Mkoani Arusha kuendelea na ziara yake

Waziri Mkuu wa Denmark, Mhe. Helle Thorning-Schmidt akisalimiana na viongozi  mbalimbali wa Mkoa wa Arusha mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mkoa huo akitokea Dar es Salaam. Mhe. Thorning-Schmidt yupo nchini kwa ziara ya siku nne kauanzia tarehe 5 hadi 8 Machi, 2013.


Mhe. Waziri Mkuu wa Denmark akiwa amefuatana na Mhe. Mary Nagu (Mb.), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji pamoja na Mhe. Magesa Mulongo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha mara baada yakuwasili mkoani Arusha akitokea Dar es Salaam

Mhe. Thorning-Schmidt pamoja na wenyeji wake wakifurahia burudani kutoka moja ya kikundi cha ngoma ya Kimasaai iliyokuwepo Uwanjani hapo wakati wa mapokezi.


Mhe. Thorning-Schmidt akilakiwa kwa shangwe na baadhi ya kina mama wa Mkoa wa Arusha



Mhe. Waziri Mkuu wa Denmark kwa pamoja na Mhe. Waziri Nagu na Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakipata picha ya pamoja na kikundi cha ngoma wakati wa mapokezi yake Arusha


Mhe. Thorning-Schmidt akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) iliyopo Jijini Arusha

Rais wa Mahakama ya ICTR, Mhe. Jaji Vagn Joensen akitoa taarifa fupi ya utendaji wa Mahakama hiyo kwa Mhe. Thorning-Schmidt (hayupo pichani)

Mhe. Thorning-Schmidt akizungumza na uongozi wa Mahakama ya ICTR (hawapo pichani) mara baada kupokea taarifa kuhusu utendaji wa mahakama hiyo.


Mhe. Thorning-Schmidt akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Mahakama ya ICTR mara baada ya mazungumzo nao.  Wengine katika picha ni Mhe. Waziri Nagu (watatu kutoka kulia), Mhe. Mulongo (mwenye tai nyekundu) na Bw. Jacob Msekwa (kulia), Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania katika nchi za Nordic ikiwemo Denmark.


Mhe. Waziri Mkuu, Thorning-Schmidt akivalishwa Vazi Rasmi linalovaliwa na kina mama wa Kimasai mara baada ya kuwasili katika Kijiji cha Wamaasai cha Lepurko kilichopo Wilayani Monduli.


Mhe. Waziri Mkuu, Thorning-Schmidt akisaini kitabu cha wageni  alipowasili kijijini Lepurko

Moja ya shughuli maalum iliyompeleka Mhe. Thorning-Schmidt kijijini Lepurko ni kuzungumza na kina mama na kusikiliza matatizo na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika maisha yao ya kila siku kama anavyoonekana.

Mmoja wa kina mama katika Kijiji cha Lepurko akimweleza Mhe. Thorning-Schmidt matatizo yanayowakabili wanawake wa kikiji hicho ikiwa ni pamoja na uhaba wa maji na elimu bora kwa watoto wao.


Moja ya nyumba  maarufu kama "Boma" zilizopo kijijini hapo

Mhe. Thorning-Schmidt akimsikiliza mmoja wa watoto wa kike ambaye ni mwanafunzi katika kijiji hicho

Mhe. Thorning-Schmidt akihutubia wananchi (hawapo pichani) wa Kijiji cha Lepurko

Mhe. Thorning-Schmidt akiangalia bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa kwa shanga na kina mama wa kijijini hapo

Mmoja wa kina mama wa Kijiji cha Lepurko akimvisha ushanga Mhe. Thorning-Schmidt

Sehemu ya Wananchi wa Kijiji cha Lepurko wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Thorning-Shmidt (hayupo pichani) ambapo aliahidi kuwasaidia katika kutatua tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama.

Mhe, Thorning-Schmidt akitoka ndani ya nyumba "Boma" aliyoitembelea kijijini hapo.

Mhe. Thorning-Schmidt akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowassa  mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika kijiji cha Lepurko.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.