Wednesday, March 6, 2013

Waziri Mkuu wa Denmark awasili nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku nne

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimkaribisha nchini Mhe. Helle Thorning-Schmidt, Waziri Mkuu wa Denmark mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tarehe 05 Machi, 2013 kwa ziara ya kitaifa ya siku nne.

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Mary Nagu (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji pamoja na Mhe. Said Meck Sadick, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati wa mapokezi ya Waziri Mkuu wa Denmark.

Mhe. Helle Thorning-Schmidt, Waziri Mkuu wa Denmark akisalimiana na  Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika wakati wa mapokezi ya kiongozi huyo alipowasili nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku nne.

Mhe. Thorning-Schmidt akiwa na Mhe. Rais Kikwete akiwafurahia akina mama  wa Dar es Salaam waliofika kumpokea mara baada ya kuwasili.
Mhe. Thorning-Schmidt akiwa na Mhe. Rais Kikwete wakati wakisikiliza nyimbo za mataifa yao zikipigwa kwa heshima ya kiongozi huyo

Mhe. Thorning-Schmidt akiwa na Mhe. Rais Kikwete.

Mhe. Thorning-Schmidt akiongozana na Jenerali Davis Mwamunyange kukagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa kwa heshima yake.

Mhe. Thorning-Schmidt na Mhe. Rais Kikwete wakifurahia kikundi cha burudani kilichokuwepo uwanjani hapo wakati wa mapokezi ya kiongozi huyo


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.