Wednesday, October 24, 2018

Dkt. Mahiga azungumza na Watanzania wanaoishi Italia

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa kwenye  Taasisi ya kidini ya Mt.Egidio Padri Angelo Romano, Tukio hilo lilifanyika kwenye Ofisi ya Taasisi hiyo tarehe 24 Oktoba, 2018 jijini Roma. Dkt. Mahiga yupo Italia kwa ajili ya kuhudhuria mikutano mbalimbali ikiwemo Mkutano wa Pili wa Mawaziri wa Mambo ya Nje kutoka Afrika na Italia ambao utafanyika tarehe 25 Oktoba,2018 pamoja na kukutana na Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendedelo ya Kilimo (IFAD) tarehe 26Oktoba,2018.

Dkt. Mahoiga akiagana na Padri Angelo Romano mara baada ya kumaliza mazungumzo.


=====Dkt. Mahiga akutana na Watanzania nchini Italia=====

Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. George Madafa leo tarehe 25 Oktoba,2018 akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Dkt. Augustine Mahiga(Mb), kwenye kikao na Watanzania waishio nchini Italia. Kikao hicho kilifanyika Ubalozi wa Tanzania nchini Italia.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Italia Bw.Andrew Mohele akitoa salamu za wanadiaspora kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga. Mkutano huo ulifanyika tarehe 25 Oktoba, 2018 kwenye Ubalozi wa Tanzania jijini Rome, Italia.
Baadhi ya Watanzania waishio Italia wakiwa kwenye mkutano huo



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.