Wednesday, October 10, 2018

Maoni ya Muswada wa Sheria ya Madini wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kukusanywa

Mwenyekiti wa Kamati ya kukusanya maoni kuhusiana na muswada wa Madini wa Afrika Mashariki Bi. Uwumukiza Francise, akionyesha kitabu cha muongozo wa utekelezaji wa shughuli za kibunge za Bunge la Afrika Mashariki wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa kukusanya maoni kwa wadau wa kila nchi wanachama wa Afrika Mashariki, ili kuuboresha kabla bunge halijaupitisha.  Mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali, mkutano huo umefanyika kwenye Hotel ya Tiffany iliyopo jijini Dar es Salaam tarehe 10. 10. 2018 
Dkt. Abdullah H. Makame akichangia jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. 
Sehemu ya wadau waliohudhuria mkutano huo wakifuatilia kwa makini ufunguzi huo
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Josephine Sebastian Lemoyan naye alipata fursa ya kuchangia kwenye mkutano huo ambapo alisema wanawake bado ni wadhaifu katika sekta ya madini  kwakua wana fursa chache za mitaji ya Madini. 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Joachim Otaru naye akielezea jambo kwenye mkutano huo 
Maafisa kutoka Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kwa makini mkutano huo, katikati ni Bw. Amedeusi Mzee akichangia mada juu ya mswada huo wa madini, wa kwanza kulia ni Bw. Abel Maganya pamoja na Bi. Laila Kagombola ( wa kwanza kushoto) wakisikiliza kwa makini maoni yaliyokuwa yakitolewa.
Picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa Mkutano










No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.