Monday, October 29, 2018

Tanzania na China zaadhimisha miaka 50 ya ushirikiano katika sekta ya afya

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akihutubia kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Ushirikiano kati ya Tanzania na China katika sekta ya afya ambapo Dkt. Mahiga ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya watu wa China kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika sekta ya Afya, ambapo imeendelea kuleta Madaktari wakujitolea katika Hospitali mbalimbali zilizopo nchini zikiwemo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Aidha, Tanzania na China zimekuwa na mahusiano katika sekta ya Afya, tangu mwaka 1968 ambapo madaktari kutoka jimbo la Shandong wamekuwa wakija Tanzania kutoa Huduma za Afya katika mikoa mbalimbali nchini.

Madhimisho hayo yalihudhuriwa na Dkt. Salim Ahmed Salim, Waziri Mkuu Mstaafu na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalim,
maadhimisho hayo yamefanyika katika Ubalozi wa Jamhuri ya watu wa China nchini.
Dkt. Salim Ahmed Salim (kulia) akisikiliza kwa makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na Dkt. Mahiga
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Prof. Mohammed Janab (kushoto) akisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Waziri

Balozi wa Jamhuri ya watu wa China, Mhe. Wang Ke, akihutubia kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya ushirikiano kati  ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa China katika sekta ya afya ambapo ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuendelea na kuimarisha sekta ya afya. Mhe. Balozi Wang Ke kwa kutambua umuhimu wa sekta hiyo na kutokana na mahusiano mazuri waliyonayo imeendelea kuleta nchini madaktari bingwa watakao kuwa wanatoa matibabu bure kwenye mikoa mbalimbali nchini. 
Juu na chini ni sehemu ya wageni waliohudhuria maadhimisho hayo wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa 
Dkt. Mahiga akiendelea kuhutubia.

Wakikata keki ya maadhimisho ya miaka 50 ya Ushirikiano kati ya Tanzania na China kwenye sekta ya Afya. 
Picha ya pamoja na Madaktari Bingwa kutoka Jamhuri ya Watu wa China.









No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.