Tuesday, October 23, 2018

Umoja wa Mataifa kuadhimisha miaka 73 tokea kuanzishwa


Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza na Waandishi leo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere ikiwa ni matayarisho ya kusherehekea miaka 73 ya Siku ya Umoja wa Mataifa ambapo tarehe 24 Oktoba husherehekewa Duniani kote na kwa Tanzania yataadhimishwa jijini Dar es Salaam na Zanzibar,  kushoto ni Bw. Alvaro Rodriguez Mratibu  Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania  na kulia  Bw. Deusdedit  B. Kaganda Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa.

Bw. Deusdedit  B. Kaganda Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikianoano wa Kimataifa kulia akimkaribisha Bw. Alvaro Rodriguez Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kushoto kuzungumza na waandishi  wa habari katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere. Mkutano huo ulifanyika kufuatia tarehe 24 Oktoba, Umoja wa Mataifa utaadhimisha Miaka 73 ya tokea kuanzishwa kwake. Katikati Mhe. Dkt. Damas Ndumaro (Mb) Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Bw. Alvaro Rodriguez,  Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania aliyekaa kushoto alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere akilelezea juu ya maendeleo ya Umoja huo na kaulimbiu ya mwaka huu katika kuadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa tarehe 24 Oktoba iliyobeba ujumbe wa "Uwezeshaji  Vijana na Ubunifu kwa ajili ya malengo ya maendeleo endelevu" 
Baadhi wa waandishi wa Habari walioshiriki katika mkutano wa Waandishi wa Habari katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
 Add caption

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.