Tuesday, October 30, 2018

Waziri Mwijage awa Mgeni rasmi maadhimisho ya Taifa la Uturuki.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage(Mb.), akihutubia kwenye hafla ya maadhimisho ya Taifa la Uturuki, katika hotuba yake Mhe. Mwijage aliishukuru Uturuki kwa kuendelea kuwa mshirika mkubwa wa jitihada za Serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuwaletea Watanzania maendeleo. Maadhimisho hayo yalifanyika katika makazi ya Balozi wa Uturuki jijini Dar Es Salaam Tarehe 29 Octoba, 2018.
Viongozi kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania wakisikiliza kwa makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mhe. Mwijage
Mhe. Mwijage akiendelea kuhutubia.
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Mhe. Ali Davutoglu naye akihutubia wakati wa maadhimisho ya Taifa la Uturuki, Mhe. Davutoglu, alisema Uturuki itaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano za kubadalisha maisha ya watu masiikini.
Mhe. Mwijage (wa kwanza kushoto), na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Jestas Nyamanga (wa pili kutoka kushoto) wakimsikiliza Balozi Davutoglu wakati akihutubia.
Mhe. Mwijage akigonganisha glasi na Balozi Davutoglu kwa kuwatakia afya njema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Joseph Magufuli na Rais Recep Tayyıp Erdoğan wa Uturuki. 
Mhe. Mwijage akisalimiana na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mhe. Monica Patricio walipokutana kwenye maadhimisho ya Taifa la Uturuki
Bw. Jestas Nyamanga akizungumza na Balozi wa Uturuki Mhe. Davutoglu 








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.