Sunday, October 28, 2018

UBALOZI WA TANZANIA, KOMORO WAADHIMISHA MIAKA19 YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

Balozi wa Tanzania Visiwani Komoro Mhe. Sylvester M. Mabumba akihutubia kwenye Kongamano la Mwalimu Nyerere, ambapo Ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na Diaspora ya Watanzania Visiwani Komoro (TADICO) pamoja na taasisi ya kijamii ya Komoro ijulikanayo kama Udjamaa wa Komori na Afrika Mashariki uliandaa Kongomano hilo la siku mbili kuanzia tarehe 26 – 27 Oktoba, 2018 kama sehemu ya kumenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Watanzania waishio Visiwani Komoro wakimsikilisha Mhe. Mabumba hayupo pichani.


Watanzania waishio Visiwani Komoro wakiwa kayika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa Kongamano hilo



UBALOZI WA TANZANIA, KOMORO WAADHIMISHA MIAKA19 YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE
TAREHE 26 – 27 Octoba, 2018

Katika harakati za kuendeleza kukuza na kuhuisha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Ubalozi wa Tanzania Visiwani Komoro kwa kushirikiana na Diaspora ya Watanzania Visiwani Komoro (TADICO) pamoja na taasisi ya kijamii ya Komoro ijulikanayo kama Udjamaa wa Komori na Afrika Mashariki uliandaa Kongomano la siku mbili kuanzia tarehe 26 – 27 Oktoba, 2018 kama sehemu ya kumenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Kongomano hilo lilifanyika katika ukumbi wa Bunge la Taifa la Komoro ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Elimu wa Komoro, Mhe. Salime Mohamed Abderemane. Aidha, kutoka Tanzania, Mhe. Pro. Mark Mwandosya alialikiwa kama mmoja ya watoa mada juu ya maisha ya Mwalimu Nyerere.
Wageni wengine mashuhuri walioshiriki katika Kongomano hilo ni pamoja na Mhe. Mohamed Msaidie, Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani wa Komoro, Mhe. Balozi Ahmed Thabeet, mmoja ya waazilishi wa Chama cha Ukombozi cha Komoro kujilikanacho kama MOLINACO. Aidha, Balozi wa Tanzania Visiwani Komoro, Mhe. Sylvester M. Mabumba naye pia aliweza kushiriki kikamilifu katika Kongomano hilo.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ubalozi wa Tanzania Visiwani Komoro kusheherekea kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Visiwani hapa. Lengo la Kongomano hilo ilikuwa ni kuelezea mchango wa Mwalimu Nyerere na Tanzania kwa ujumla katika harakati za ukombozi wa Visiwa vya Komoro kuanzia 1962 – 1975. Aidha, Kongomano hilo lililenga pia kuikurubisha Komoro katika ukanda wa Afrika Mashariki, kwa kuwa mda mrefu Visiwa hiyo vimeelekeza mahusiano yake katika nchi za Ulaya na Mashariki ya Kati.
Watoa mada mbalimbali waliweza kuelezea kwa kina mchango wa Mwalimu Nyerere katika harakati za ukombozi wa Visiwa vya Komoro na Afrika kwa ujumla. Prof. Mwandosya kwa upande wake alielezea mchango wa Mwalimu katika harakati zake za kudumisha umoja na kuwasihi wa Komoro kudumisha umoja wao hasa katika kipindi hiki ambapo nchi hiyo inapitia mageuzi makubwa ya kisiasa.
 Kongomano la kumuenzi Mwalimu Nyerere lilifana sana na imekuwa ni chachu kwa Wakomoro kuona umuhimu wa kudumisha mahusiano ya (Kusini-Kusini), South-South Cooperation. Ubalozi umedhimiria kuendeleza Kongomano la Mwalimu kwani imeonekana yanachangia sana kudumisha mahusiano mazuri yaliopo baina ya Tanzania na Komoro.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.